Nashauri Mawaziri, RC DC na DED wapelekwe Semina Elekezi kama enzi za JK. Fikiria wakati tunazungumzia Utekaji DC anadai Kuna Kitu alifanya Maporini!

Semina ya mikakati ya kudanganya umma (propaganda)? Interesting 🤔
 
Haya maneno mawili,yana maana pana sana "......kwenye mapori...... .....washachakata kwenye vitongoji,kata na vijiji vyote........" Huyu naona yupo kamati moja na Nape,kila siku wanazidi kuzihirisha kwamba sanduku la kura si chochote.

Ila huko kwenye mapori,wanafanyaga nini.........? Ila ninavyo wajua wnasiasa wanaweza kukwambia wanaendaga kukata gogo.
 
Mkuu kama hizo “alizoropoka” DC zina quality ya siri za nchi then we are living in one hell of a sthl* country! (*Courtesy of D Trump).
 
Mkuu kabla ushauri wako haujafanyiwa KAZI ni vizuri huyu DC afikishwe MBELE ya Sheria akaulizwe na akina Madeleka huko poloni kilifanyika Nini?
Kumbuka hata sativa aliokotwa polini.
 
Nduli aliondoa wafanyakazi wenye vyeti fake akaleta wenyeviti wa vijiji,madiwani na wabunge fake. Ukute na Mzungumzaji wa bunge naye ni kanyaboya!
 
Mkuu fuatilia wasimamia uchaguzi ni akina nani?
Wana sofa zipi? Kumbuka wengi wao ni walimu na miongoni mwao wapo wanaojielewa na Huwa hawachukuliwi kabisaaa!!!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…