N'yadikwa
JF-Expert Member
- Aug 10, 2014
- 7,427
- 10,905
Wakati nikikua mchezo wa kuruka kwa upondo na ule wa kuruka kawaida sambamba na mchezo wa kurusha mkuki na vitu vizito ilikuwa inafanyika na watu walikuwa wanafanya vizuri.
Ukizingatia kwamba Wakenya tayari wamejitambulisha kwa mchezo wa riadha; sisi hapa kwetu Tanzania bado hatujakuwa na mchezo unaotutambulisha vema; nashauri sasa tujaribu michezo hii kwa serikali kuitilia mkazo ikiwa ni pamoja na kujenga viwanja vyake vikubwa hasa kwenye miji mikubwa kama Mwanza Dar Dodoma Arusha na Mbeya japo kwa kuanzia.
Tuseme ukweli Tanzania kwenye diplomasia ya michezo bado hatufanyi vizuri kwa kuwa hatuna timu za mchezo wowote zinazoenda wala kushinda medali kwa kiwango chochote cha kuridhisha tangu enzi zile za riadha ya kina Nyambui na Filbert. Serikali uchaguzi ukiisha tafadhali mliweke hili kwenye ajenda, tunapenda kuwa na vizazi vyenye furaha na umoja kwani michezo hutuleta pamoja. Na michezo sio soka pekee. Kuna watu wanapenda aina hiyo na michezo; ipatiwe kipaumbele bila kusahau mieleka.
Nawasilisha.
Ukizingatia kwamba Wakenya tayari wamejitambulisha kwa mchezo wa riadha; sisi hapa kwetu Tanzania bado hatujakuwa na mchezo unaotutambulisha vema; nashauri sasa tujaribu michezo hii kwa serikali kuitilia mkazo ikiwa ni pamoja na kujenga viwanja vyake vikubwa hasa kwenye miji mikubwa kama Mwanza Dar Dodoma Arusha na Mbeya japo kwa kuanzia.
Tuseme ukweli Tanzania kwenye diplomasia ya michezo bado hatufanyi vizuri kwa kuwa hatuna timu za mchezo wowote zinazoenda wala kushinda medali kwa kiwango chochote cha kuridhisha tangu enzi zile za riadha ya kina Nyambui na Filbert. Serikali uchaguzi ukiisha tafadhali mliweke hili kwenye ajenda, tunapenda kuwa na vizazi vyenye furaha na umoja kwani michezo hutuleta pamoja. Na michezo sio soka pekee. Kuna watu wanapenda aina hiyo na michezo; ipatiwe kipaumbele bila kusahau mieleka.
Nawasilisha.