Nashauri Wanajeshi mnapokuja kwenye biashara za kiraia msije kikundi na kuvaa magwanda

Nashauri Wanajeshi mnapokuja kwenye biashara za kiraia msije kikundi na kuvaa magwanda

Ubabe wa kijinga ndo unafanya baadhi yao wanadundwa au kuchomwa visu mtaani...
 
Wale jamaa ukiwauzia kitu kizuri huwa wanaambiana wanakuja kundi kama wanafunzi kununua. Ila hakikisha unawauzia mali nzuri hivyo hivyo hata kama unawapiga bei kubwa.
Tena wasipokyja wengi atakuja mwingine anunue bidhaa hata zaidi ya mahitaji yake. Wako loyal ila usiwauzie mabomu. Na wengi hawajui bargain
 
Mimi binafsi naona ni ubabe wa usiofaa wa baadhi ya wanajeshi, mtu anakuja ofisini kwako kavaa kiraia.

Mnafanya biashara vizuri, Ikitokea biashara imeenda kinyume siku akija kueleza matatizo anakuja na kikundi cha wenzake wawili au watatu huku amevalia nguo za kijeshi na vitisho kibao, kwanini uje unitishie? kawa yawezekana wanunue maduka ya wanajeshi wenzao au huko kambini na si kuja kuleta ubabe mtaani.

Mfano kaja na subaru yake kanunua spare, anaenda anafunga kisha baada ya muda anarudi kama mbogo akidai umempa kitu sio kizuri, na haji kwa maelezo mazuri bali ubabe na kikundi cha wenzake.

Kama ulikuja kiraia basi urudi kiraia tuyazungumze, ubabe hausaidii kitu na si kila mtu anakubbali kuonewa kirahisi rahisi.
Mkuu mwambie na ww unauziwa ndyo uje kuuza ww syo kiwanda wakuzalisha hzo spears
 
Back
Top Bottom