Mammamia wewe ni kaka, kwa mtazamo wako (tokana na a man's perspective) na sababu your field applies unadhani hapa tatizo ni nini? Kwa nini baadhi ya wanaume (tena wengi tu) hupenda na kutamani wanafunzi?
Katika hili nitaomba pia
Mpatanishi (habari ya siku kaka) na
Azimio Jipya (please apply your psychology here and narrow it down kama inawezekana),
Roulette (want to see your angle alter) wanisaidie.
Ingawa wengi tumezungumza kwa utani, kejeli na kulaani tabia ya ndugu yetu huyu
Kowan, ukweli ni kuwa haya ni matatizo ya kisaikolojia kama ambavyo wengine hupata ashki kama hiyo kwa wajawazito, wenye maungo maumbo makubwa au madogo, vikongwe na wengine hadi kwenda makaburini kufukua maiti na kuwafanyia tendo la ngono.
Kuhusu sare na mavazi, nimepata kuwasikia wengine wakivutiwa na wanawake wanaovaa sare za hospitali, katika magwanda ya jeshi au polisi hadi wale wanaojisitiri sana (mfano kama katika avatar yako - lol). Kwa hivyo siwezi shangaa kuwa huyu kijana wetu yeye kaathirika na wanaovaa sare za shule, na kueleza wazi kuwa hasa ni zile zisizositiri sana miili yao.
Katika uchaguzi wa kile mtu anapenda sidhani kama kuna kosa isipokuwa pale anapovuka mipaka, kama lile la kufanya ngono na maiti na wanafunzi. Kama nimefahamu vyema bandiko lake ni kuwa wanaovaa sare mara nyingi ni wanafunzi hadi sekondari, na hawa wengi wao bado wanakuwa na ule umri ambao kisheria tunauita umri mdogo, na hii ni hatari sana. Kwani, licha ya umri wao mdogo, bado ni wanafunzi na wanapaswa kushughulikia masomo yao na sio kuangukia mikononi mwa mabazazi, au tuwaite wagonjwa kama ndugu yetu huyu.
Kwa kuwa mimi sio mtaalamu wa saikolojia, na kama nilivyosema katika bandiko langu na wengine kumshauri, nahisi anapaswa kuwaona wataalamu wanaohusika haraka. Kumwambia tu awaone hao anaowatamani kama ndugu au watoto wake haiwezi kumsaidia kwani moyoni anajua kuwa hao hana uhusiano nao, na kama gonjwa lake limekubuhu anaweza hata kuwatamani ndugu au watoto wake. Anahitaji msaada wa kitaalamu.