Komeo Lachuma
JF-Expert Member
- Oct 31, 2014
- 7,926
- 17,030
Kiukweli kama week mbili sasa sikuwa na amani kabisa wala furaha. Huyu dada nampenda sana na ni mwaka sasa. Nimeamua nimuoe. Of course nlimkuta ana mtu so nikatumia nguvu nyingi kumpata.
Sasa last week nlienda kufanya sapraiz kwake. Bahati mbaya nikamkuta na mwanaume wake wa zamani wananyonyana mate sebuleni. Nlishtuka sana nikawaomba radhi nikatoka kurudi home.
Baadaye nlimtafuta kwa simu akawa hapokei. Baada ya siku mbili ndo akapokea. Alinifokea sana kuwa nlimdhalilisha nitaendaje kwake bila kumtaarifu. Na hizo tabia za kishamba hapendi. Aliniambia wanaume huwa hawafanyi hivyo.
Kweli nlijisikia vibaya sana. Maana yeye alidhani nlienda kumfumania makusudi kumbe wala hata sikuwa na hiyo nia. Basi tu ilitokea bahati mbaya. Kiukweli kipindi chote napotaka kwenda huwa namwambia siku moja kabla siku ile ufala tu uliniingia. Nilijutia kosa langu kwa kweli.
Nimembembeleza sana mwishowe ameamua kunisamehe na kuruhusu tuendelee na uhusiano. Jaman nashauri msipende kusapraizi mtu si nzuri kwenye mahusiano.
Sasa tumerudiana na nimeshika adabu yangu. Huyu dada nachompendea pia ana msimamo sana so tumekutana watu wa misimamo. Mwakani nataka nimuwowe.
Sasa last week nlienda kufanya sapraiz kwake. Bahati mbaya nikamkuta na mwanaume wake wa zamani wananyonyana mate sebuleni. Nlishtuka sana nikawaomba radhi nikatoka kurudi home.
Baadaye nlimtafuta kwa simu akawa hapokei. Baada ya siku mbili ndo akapokea. Alinifokea sana kuwa nlimdhalilisha nitaendaje kwake bila kumtaarifu. Na hizo tabia za kishamba hapendi. Aliniambia wanaume huwa hawafanyi hivyo.
Kweli nlijisikia vibaya sana. Maana yeye alidhani nlienda kumfumania makusudi kumbe wala hata sikuwa na hiyo nia. Basi tu ilitokea bahati mbaya. Kiukweli kipindi chote napotaka kwenda huwa namwambia siku moja kabla siku ile ufala tu uliniingia. Nilijutia kosa langu kwa kweli.
Nimembembeleza sana mwishowe ameamua kunisamehe na kuruhusu tuendelee na uhusiano. Jaman nashauri msipende kusapraizi mtu si nzuri kwenye mahusiano.
Sasa tumerudiana na nimeshika adabu yangu. Huyu dada nachompendea pia ana msimamo sana so tumekutana watu wa misimamo. Mwakani nataka nimuwowe.