Nashukuru ninachokipata na ninachopewa

Nashukuru ninachokipata na ninachopewa

Habari wakuu.

Katika huu mchezo wa Maisha Kuna mambo mengi sana Sisi wanaume tunapitia.

Sometimes unaenda kutafuta unarudi na kitu kidogo mfukoni kufika home watoto wanakukimbilia Kwa shangwe Sana. Basi Nguvu ya nafsi inakwambia hawa watoto ndio faraja yako. Unaingia ndani ya nyumba mke naye anatabasamu kuona mume wake umerudi Salama.

Maisha Yana furaha ukiwa karibu na familia yako. Hakikisha hufanyi makosa Yale aliyofanya baba yako.
Mwanaume mwenzangu mpende mkeo na watoto wako mana Hao ndio hujua baba yupo ndani amelala na mama.

Kugombana kupo lakini hakuna jipya chini ya jua Zaidi tunaishi ili tufe.

Salute kwenu brothers ambao mnanipa support pale ninapokwama kiuchumi.
Baba yangu hajafanya makosa
 
Umenikumbusha nilivyokua mdogo, tunafurahia baba akirudi nyumbani na kumkimbilia kumuwaoooo, ilikua best part of our day, I hope kwake naye tulimpa faraja kama watoto.

Familia ni kila kitu 🤍
Bila Shaka na Wewe una watoto
 
Uzi mzuri lakini kitendo cha kumsema vibaya baba hapo ndo amekosea kabisa.
Unajua maana ya makosa ya wazazi (MADINGI)
kukimbia uzao wake
Kuitelekeza familia Yake hili ndio kosa ambalo ninazungumia Mimi.
Na zile kutia mimbo hovyo mabinti halafu huduma mbovu.

Inapendeza sana watoto wengi wawe baba mmoja na mama mmoja.
 
Unajua maana ya makosa ya wazazi (MADINGI)
kukimbia uzao wake
Kuitelekeza familia Yake hili ndio kosa ambalo ninazungumia Mimi.
Na zile kutia mimbo hovyo mabinti halafu huduma mbovu.

Inapendeza sana watoto wengi wawe baba mmoja na mama mmoja.
Kumbe wewe umelelewa na mzazi mmoja? Sikujua mkuu, sorry, basi usingejumlisha wazazi wote.
 
maisha hayana kanuni au mfumo, hivyo vitu vidogo kwa wengine ni vikubwa mno.

nikiwa mwenyewe nipo nipo, ila niki enda nyumbani. Mzuka haswa.
Mara hili au lile.

Money comes and go, but family is everything.
 
Nimekutana na huu uzi umenikumbusha,jana asubuhi ya saa 07:23 AM pale Magomeni Kagera maarufu Oil Com (wanaotumia hii barabara ya Morogoro wanapajua) nilipata sononeko kubwa sana la nafsi nilipomuona mwanaume mwenzangu,baba wa familia na muhangaikaji mwenzangu(umri above 40+) akiiingia Toyota Rav4 kwa mbele na pikipiki yake,yule brother alikuwa amevaa Kaunda Suit ya brown na bag mgongoni yaani yupo tu smart wala siyo bodaboda bodaboda wanajulikana.

Yaani within a second jamaa alikuwa hafai,alikuwa hajavaa helmet kichwa chote damu puani mdomoni masikioni yaani hajiwezi,anabebwa pale yaani dah!kilichonifanya nikamuhurumia sana ni mazingira niliyotoka home,wakati natoka mbio mbio (mimi huwa navaa kofia) nilisahau kuvaa so nikampita mwanangu wa kike aged six alikuwa anakinga maji bombani aingie msalani kuwahi shule,nimetembea kama hatua saba mbele kakaniita ”Baba unaenda kazini?” kabla sijajibu kakaniambia “umesahau kofia” kisha mbio ndani kwa mama yake kakaniletea nikapokea nikavaa kisha kakasema ”bye baba” nikamjibu aaya nikampiga kakofi mgongoni mie mbio.

Nilipoona hili tukio nilivaa viatu vya jamaa kwa hii situation aliyokutana nayo,ameaga vizuri wanae nyumbani kwa furaha akili asubuhi imechangamka mipango yote halafu dah,anakutana na mzinga anaishia hospital au kwingine aisee niliwawaza mkewe na wanae wakisikia kilichompata mpendwa wao ilibaki kidogo nilie,ila ndiyo maisha tumeandikiwa in short vipo vitu tunaishi navyo vinaumiza sana but ndiyo reality lazima vitukute kama kwa kutaka au kutotaka muhimu tuendelee kuombeana heri mke na mume migogoro ya ndani iishe pale mmoja wenu anainua mguu kwenda kutafuta mtakie mema hata likimtokea baya liwe na afadhali.

NB:Aisee mkuu uliyepata ajali jana eneo tajwa hapo juu kama upo humu ikitokea Mungu amekujaalia ukakaa sawa ukikutana na hii post usiache kusema neno kuhusu maendeleo yako,pole sana.
 
Uzi mzuri lakini kitendo cha kumsema vibaya baba hapo ndo amekosea kabisa.
hajamsa baba ila amesema ukweli kabsa wazee wetu mao
wamezngua kwa namna moja au nyingne na ss tujaribu kutokurudia makosa hajakosea
 
Nimekutana na huu uzi umenikumbusha,jana asubuhi ya saa 07:23 AM pale Magomeni Kagera maarufu Oil Com (wanaotumia hii barabara ya Morogoro wanapajua) nilipata sononeko kubwa sana la nafsi nilipomuona mwanaume mwenzangu,baba wa familia na muhangaikaji mwenzangu(umri above 40) akiiingia Toyota Rav4 kwa mbele na pikipiki yake,yule brother alikuwa amevaa Kaunda Suit ya brown na bag mgongoni yaani yupo tu smart.

Yaani within a second jamaa alikuwa hafai,alikuwa hajavaa helmet kichwa chote damu puani mdomoni masikioni yaani hajiwezi,anabebwa pale yaani dah!kilichonifanya nikamuhurumia sana ni mazingira niliyotoka home,wakati natoka mbio mbio (mimi huwa navaa kofia) nilisahau kuvaa so nikampita mwanangu wa kike aged six alikuwa anakinga maji bombani aingie msalani kuwahi shule,nimetembea kama hatua saba mbele kakaniita ”Baba unaenda kazini?” kabla sijajibu kakaniambia “umesahau kofia” kisha mbio ndani kwa mama yake kakaniletea nikapokea nikavaa kisha kakasema ”bye baba” nikamjibu aaya nikampiga kakofi mgongoni mie mbio.

Nilipoona hili tukio nilivaa viatu vya jamaa kwa hii situation aliyokutana nayo,ameaga vizuri wanae nyumbani kwa furaha akili asubuhi imechangamka mipango yote halafu dah,anakutana na mzinga anaishia hospital au kwingine aisee niliwawaza mkewe na wanae wakisikia kilichompata mpendwa wao ilibaki kidogo nilie,ila ndiyo maisha tumeandikiwa in short vipo vitu tunaishi navyo vinaumiza sana but ndiyo reality lazima vitukute kama kwa kutaka au kutotaka muhimu tuendelee kuombeana heri mke na mume migogoro ya ndani iishe pale mmoja wenu anainua mguu kwenda kutafuta mtakie mema hata likimtokea baya liwe na afadhali.

NB:Aisee mkuu uliyepata ajali jana eneo tajwa hapo juu kama upo humu ikitokea Mungu amekujaalia ukakaa sawa ukikutana na hii post usiache kusema neno kuhusu maendeleo yako,pole sana.
Fate mkuu. Sisi tupambane tu hatuijui fate yetu, ila mwamba hapo kuwasema wababa waliotuzaa vibaya nashindwa kuelewa kama anajua aliyokuwa anapitia baba yake......
 
Habari wakuu.

Katika huu mchezo wa Maisha Kuna mambo mengi sana Sisi wanaume tunapitia.

Sometimes unaenda kutafuta unarudi na kitu kidogo mfukoni kufika home watoto wanakukimbilia Kwa shangwe Sana. Basi Nguvu ya nafsi inakwambia hawa watoto ndio faraja yako. Unaingia ndani ya nyumba mke naye anatabasamu kuona mume wake umerudi Salama.

Maisha Yana furaha ukiwa karibu na familia yako. Hakikisha hufanyi makosa Yale aliyofanya baba yako.
Mwanaume mwenzangu mpende mkeo na watoto wako mana Hao ndio hujua baba yupo ndani amelala na mama.

Kugombana kupo lakini hakuna jipya chini ya jua Zaidi tunaishi ili tufe.

Salute kwenu brothers ambao mnanipa support pale ninapokwama kiuchumi.
Hakika walisema Kushukuru ni Kuomba tena halafu wazee na maandeko wakaongezea kwamba Usiposhukuru kwa kile kidogo ulichopewa hata ukipewa kikubwa hutoshukuru.
 
nipe jero ntakudai 4500

IMG_20250201_232338.png
 
Fate mkuu. Sisi tupambane tu hatuijui fate yetu, ila mwamba hapo kuwasema wababa waliotuzaa vibaya nashindwa kuelewa kama anajua aliyokuwa anapitia baba yake......
Bila Shaka umeelewa nilichomaanisha.
 
Back
Top Bottom