Nasikia harufu ya damu Man United vs Real Madrid

Nasikia harufu ya damu Man United vs Real Madrid

Tutawanyoa bila maji hao Madrid, ndo mwanzo wa kushuka kiwango...mtashangaa!! kesho tunaweza kuwaacha wakapeta ila kwenye kombe wasahau.
 
Hawa Real Madrid wasije kuniomba nifanye mazungumzo yeyote na De Gea ili nimshawishi nimeona ni wajinga sana

Usinisahau kwenye Baraza Jipya.
 
Ujio Wa Mourinho angalau umefanya timu yetu kuwa na kiasi Fulani cha ujeuri sokoni kama inavyopasa kuwa. Mi naombea hii vita kati ya Real na Man U iendelee tu ili tuone nani atakayetokwa na damu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukisikia fake news, ndio zimetawala kwenye hii mada.

MUNICH AIR DISASTER.

Madrid ilijitolea kuisaidia Man United kwa sababu rais wa Madrid wakati huo(Santiago Bernabeu) na kocha wa Man United(Matt Busby) walikuwa na mahusiano mazuri na waliheshimiana. Baada ya ajali, Real Madrid ambao waliibuka washindi ya European Cup(Champions League kwa sasa) walijitolea kuwapa Man United kikombe(wakakataa), pamoja na Di Stefano kwa mkopo wa msimu mmoja tu, ambapo United wangelipa sehemu ya mshahara wake. FA wakazuia dili ya Di Stefano ili kuwapa nafasi wachezaji wa nyumbani. Hiyo ya wachezaji watano ni ya vijiweni. How Real Madrid helped to rebuild Manchester United after Munich air


KUHUSU BECKHAM NA WENZIE WALOKUJA MADRID.

Beckham aliamua kuja Real Madrid baada ya kugundua kuwa Man United walikuwa kwenye mazungumzo ya kumuuza Barcelona baada ya 'ugomvi' wake na Fergie. Hakufanya mazungumzo na Barca. Beckham reveals how Man Utd almost sold him to Barcelona | Goal.com

Cristiano Ronaldo pia alilazimisha kuuzwa Madrid, na sio kwamba Machester United ilimuuza kwa roho safi. Ramon Calderon aliyekuwa rais wa Madrid wakati huo alitamani sana kumsajili Cristiano na akatumia njia ambazo Fergie hakupendezwa nazo. Ilibidi Fergie amuombe Cristiano abaki Man United kwa msimu mmoja zaidi, na akamuahidi kumuachia aende Madrid msimu unaofuata, na alitimiza ahadi yake. Sir Alex Ferguson book: David Beckham had to leave Man Utd

Kesi ya G Heinze inabidi uelewe club haiwezi kumuuza mchezaji kwa club nyingine bila ridhaa ya mchezaji husika. Lazima mchezaji akubaliane na club inayotaka kumnunua, ndio dili ifanikiwe. Club haimlazimishi mchezaji pa kumuuza.

KUHUSU MORATA.

Real Madrid ni club kubwa duniani na inaendeshwa kiweledi. Toka mwanzo Madrid waliweka wazi kuwa wanatamani kila mchezaji abaki, kwa sababu tayari tuna timu bora. Morata ndiye aliyetaka kuondoka, hivyo Madrid wakalazimika kutaja thamani ya Morata ili atakayefika dau amchukue. Man United walijaribu ku-negotiate, lakini hawakufikia muafaka na wakaondoka, simple as that.

‘It is a right of Madrid to ask for their players the amount they want. We will not be the ones who put a price on a Real Madrid player. I cannot criticise Real Madrid and I can not criticise my club.

‘(We made) offers we thought were fair and yet no agreement was reached.’ -
Mourinho.

Manchester United news: Jose Mourinho breaks silence on Alvaro Morata transfer pursuit | Metro News

Hizi habari kuwa Madrid wameweka kinyongo kwa sababu ya De Gea ni utanzania mtupu. Madrid walishajaribu kuwasajili Alaba na Ribery kwa misimu kadhaa bila mafanikio, na bado wanawauzia Bayern Robben, Alonso, na James bila mtima nyongo.


REAL MADRID NI CLUB YA KIU-UNGWANA ZAIDI.

Msimu huu Real Madrid imesajili wachezaji wawili kutoka Atletico Madrid(Theo Hernandez) na Real Betis(Dani Ceballos). Wachezaji wote wawili walikuwa na vifungu katika mikataba yao vya kuwaruhusu kuhamia clubs nyingine, endapo kama kiasi cha hela kilichotajwa kingelipwa(release clauses). Maana yake ni kuwa, Real Madrid baada ya kuelewana na wachezaji husika, ingeweza kwenda moja moja FA na kulipa hizo hela bila kuongea chochote na clubs husika. Kuonyesha uungwana na ukomavu, Madrid iliamua kuelewana na hizi clubs na kuishia kulipa gharama zaidi ili tu kulinda mahusiano baina yao.



MAHUSIANO BAINA YA REAL MADRID NA MAN UNITED.

Hakuna tatizo lolote kati ya hizi club mbili. Wanafanya mazoezi na kuishi jirani, na wanatembeleana muda wa kupumzika, Hizi porojo na 'visasi' viko kwa mashabiki tu.
 
Ujio Wa Mourinho angalau umefanya timu yetu kuwa na kiasi Fulani cha ujeuri sokoni kama inavyopasa kuwa. Mi naombea hii vita kati ya Real na Man U iendelee tu ili tuone nani atakayetokwa na damu.

Sent using Jamii Forums mobile app

Man UTD hana jeuri ya kushindana na real madrid sokoni. Namaanisha, madrid na man utd wote wawe serious juu ya kuhitaji kumsajili mchezaji fulani sokoni, ni real madrid ndo ataibuka kinara.

Na nikwambie tuu, real madrid ni ndoto ya kila mchezaji kuichezea.
 
Man UTD hana jeuri ya kushindana na real madrid sokoni. Namaanisha, madrid na man utd wote wawe serious juu ya kuhitaji kumsajili mchezaji fulani sokoni, ni real madrid ndo ataibuka kinara.

Na nikwambie tuu, real madrid ni ndoto ya kila mchezaji kuichezea.
Unaishi kwa kukariri wewe. Ninachofahamu kwa sasa wapo serious wanatafuta golikipa, na de gea bado ni main target kwao, wamchukue sasa. Madrid ya Leo sio ile ya juzi. Hii ya Leo na yenyewe inapata frustration sokoni. Masuala ya dream siku hizi hayapo,weka mkwanza mzuri mezani na uwe umefuzu UCL.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unaishi kwa kukariri wewe. Ninachofahamu kwa sasa wapo serious wanatafuta golikipa, na de gea bado ni main target kwao, wamchukue sasa. Madrid ya Leo sio ile ya juzi. Hii ya Leo na yenyewe inapata frustration sokoni. Masuala ya dream siku hizi hayapo,weka mkwanza mzuri mezani na uwe umefuzu UCL.

Sent using Jamii Forums mobile app

Madrid haijamtaka de gea, madrid ikimtaka de gea, si man u wala de gea mwenye jeuri ya kukataa. Hizo habar unazosema ni habari za magazeti ya udaku ya uingereza.
 
Back
Top Bottom