Naskia BSS bila kura ingekuwa catastrophy!!

Naskia BSS bila kura ingekuwa catastrophy!!

Mshindi wao kwa mwaka huu kwa majaji alikuwa ni Kelvin Mbati!!!! Naona aibu ilkuwa kubwa kama wangethubutu kutompa Paschal Casian. Iwe fundisho kwao baada ya kumchaga Misoji mwaka jana bila ridhaa ya Watanzania. Mwaka jana yule dogo ambaye alikuwa ni composor ana alikuwa anacheza gitaa yaani yule mshindi wa pili ndiye alitakiwa awe mshindi

Hakika ile BSS ya mwaka jana ilinichefua na mwaka huu sikuiangalia tena. Niliamini huyo Misoji alibebwa.

Mwakani Mungu akitujalia nitaangalia.

Hongera Paschal
 
Burn

wewe una make sense kiasi fulani, maana nilikua najuliza credibility ya hao Star fish mobile .

Kupanga matokeo kwa kumandaa Cassian toka mwanzo kama mshindi ina wezekana, kwa maana ya kustet kura nyingi ziende kwa Cassian, kwa sababu ni rahisi ku mcontrol cassian kuliko Kevin.

lakini hata hivyo nime fuatilia sana hii BSS , hata walipo kua wana kwenda kupiga show live Mfano coco beach na kwingine, ungeshangaa jinsi Cassian alivyo kua ana shangiliwa kupita wote na ilionyesha kua cassian alikua ana fans wengi.

To sinani

Suala la Misoji naweza sema ushabiki ulikua unakaribiana na yule jamaa guitarist ,pale Misoji alishinda kihalali alikua na fans wengi , mimi mmoja wapo nili vote for Misoji

Suala la Miss TZ , mara nyingi mshindi tunakua tuna mjua kabisa na mara zote huwa ni huyo tunaye mtabiri ,kasoro hizi miss TZ mbili za mwisho yaani Ms Karrim na huyu Ms Gerald , hizo mbili Mshindi kajuweza tabiriwa, sasa kama majority wanajua mshindi lazima atakua fulani kutokana na vigezo tunavyo viona , sasa matokeo yatapangwaje?

Halafu mjue mashindani yanayo involve watu wa kawaida kuvote , mara nyingi huwa haya zingatii sana kipaji moja kwa moja, kwa sababu audience ina weza amua mchagua fulani kwa sababu zozote , labda uzuri wa sura, maringo au hata kuonea huruma.

Again, wengi mnao lalamika , mtakuta hamjafuatatilai toka mwanzo na mna kua mana fuatilai mwishoni kwa kua fulani kakukuna ila hamjaona majority wanataka nini. nawengine hata ku vote hammvote .

To Fidel80
Sio kweli unavyo sema , cassian tulisha jua atashinda kwani kura za nyuma zilizo oneyshwa kila siku zilikua anaongoza na siku ya show pia zilipo onyeshwa tulijua atashinda .Kevin kuna wakati alikua anapitwa hadi na yule jamaa wa Tanga kwa kura na Hadi Ritha kasema kabisa Jama wa Tanga amekuja juu ghafla maan walishangaa alivyo ibuka.

To Joyceline

Kweli kabisa , jamaa alikua na haki zote , kwanza suku ya kwanza anafanya audition ali udefend kabisa aina ya uimbaji anao imba kwa kujaribu kueleza ni unapendwa na watu waina gani , uzuri Ritha alimuelewa .
Kilicho tukoga zaidi ni jinsi anavyo badilika kila ziku , mimi nilikua fan wa Kevin ila mwisho nikabadili mawazo.

To BadoNipo

Yes kwa mtizamo wa Master J, kwamba Kebvin anauzika kwa Bongo flava na nadhanialipenda kufanya kazi nae na ingekua rahisi zaidi kwa Bongo flava , ila Kura zilikua za haki , sijui kama ulikuepo kwenye show, usipime huyu Cassian alipo panda jukwani , ilkua ni ajabu kwa mlipuko wa kelele za mashabik.

AY hakushangiliwa sana na hata Shaa hakushangiliwa kama wlaivyo shangiliwa washiriki wa BSS, hii labda kutokana na washabiki kuona hao jamaa wako juu . ila Shaa alitoa bonge la show kuliko AY.
 
Chaguo la madamu ni Kelvin...hata wakati kula zinaendelea kupigwa phase ya kwanza ilipo isha wakti wanatoa comment alisea salama katuma sms kumkubali Kelvin..toka uko aliko kuonyesha wapiga kula kuwa hivi tunafanya nini wakati hata majaji wote tunamkubali kelvin....Master J nae anasema kelvin yuko mbali anawashangaa watanzania...hivi kweli ule wimbo wa Marlow aliutendea haki kweli yule kijana?Hata kaam ni kulalili....kweli kweli?

Hapana kelvin hakuwa akifaaa hata kidogo yeye kukaa kwake nje basi angeimba nyimbo za kizungu...alishidwa hata na Jaksoni katika kuimba jackson alitendea haki wimbo wa R.kELLY.

Angalizo kwa BSS...Next time watafute watu makini wenye kujua mziki...adoubt kama tanzania wapo wa kuwa hired na Madam...ila kama tunaweza toka 25m basi tunaweza pata watu makini...Master J anajua..lakini alikaa na wasio Jua.Tuige mfano wa tusker project fame....hata kidogo kama hatuwezi vyote..kule hakuna ubishi...watu wanaimba....
 
Dhumuni la mashindano haya ni kuibua vipaji na kuwezesha kiuchumi, Cassian hatakama hatapanda chart tena ,ila teari ni a 25 million richer , ambazo akitulia ana weza fanyia la maana, Million 25 angepata wapi ? mkopo wa Bank wenye riba ya kufa mtu? BSS ime mfaidisha.

Tuangalie mashindani mengine kama mfano haya Tusker Project fame, washindi wale wawwili wako wapi umeshawaahi sikia tena?

Hata American Idol ,pia kuna walio shinda na wame hit record za mwanzo tuu baadae waka[potea na wengine walishinda na hawakua chaguo la ma judge, mfano Ruben na hata yule Fantasia.

Mahsindano haya yana kuibua kukupa nafasi uonekane , baada ya hapo ni juu yako mwenywe kujiendeleza pale mkataba ukiisha kwani utakua umenufaika kw amafunzo na kiuchumi pia .sawa kabia na hata mashindano America Next top Model, kuna watu walihoji je washidi inakuaje baadae!
 
Hapo umelonga maana Kevin aliimba ile nyimbo ya "Wind beneath my wing" siku i recognise kabisa mbaka nakaribua mwisho, maana ili sound horrible na ile poor diction ndio ilikua ime haribu kabisa.

Nilikua kwenye show, ukiwasikiliza Live tokana na kelele za mle ndani una weza dhani wanaimba vizuri, ila nilipo toka home niliacha na record ile show kwenye DVD, baadae kuja ku review ile DVD, nili stushwa na jinsi walivyo kua wana sound vibaya tena wote hata huyu Cassian na nikasema hii nyimbo ya Marlow kwakweli kaiimba vibaya sana huyu Kevin.
 
Mbali na hilo, ushindi wa Pascal umekosolewa ‘kiduchu' na wadau kwamba licha ya kuwa msanii huyo ana sauti nzuri, yenye nguvu na pumzi lakini alifanya makosa wakati wa fainali ambayo hayakukosolewa na majaji.

Ilielezwa na wadau kuwa, mshindi huyo wa mwaka huu, alikuwa na tatizo la kukatika pumzi mara kwa mara wakati anaimba lakini majaji hawakumkosoa, badala yake walimpongeza, hivyo kuondoa uhalisia wa uwepo wa majaji siku hiyo.

Katika hilo, Samson Kashlata wa Mbezi Beach, Dar alisema kuwa, inawezekana majaji walishindwa kukosoa baada ya kuona sehemu kubwa ya wahudhuriaji wa fainali walikuwa wanampongeza.

"Suala hapa ni kusema ukweli, nakubali kuwa, Pascal ni mzuri lakini siku hiyo alifanya makosa mengi ya kitaalamu jukwaani, pumzi ilikatika halafu majaji hawakukosoa, hii si sawa. Ushindi angepewa lakini angekosolewa kwanza kwa sababu leo (usiku wa kuamkia Jumatano) amefanya shoo mbaya.

"Ingependeza majaji wetu wamuige Jaji Ian wa Project Fame, yule jamaa ilikuwa hata mashabiki washangilie wote lakini ukikosea kitaalamu atakukosoa tu, tunataka na hapa iwe hivyo," alisema Samson.

Wadau pia, walimshauri mtaalamu wa ‘voko' za Kiingereza, Kelvin kujiandaa na mashindano ya Project Fame Season Four kwa maelezo kuwa uwezo wake unatosha kumfanya mshindi katika mashindano hayo.

"Kelvin ana uwezo mkubwa, hapa wapigakura wa Tanzania ni wale wenye mitazamo ya ki-Bongo Flava zaidi, naamini Kelvin ni bonge la mwanamuziki, kwahiyo naamini kule atafanya vizuri kwa sababu sauti yake inakubalika kimataifa," alisema Sadala K wa Sinza, Dar.

Kukamata nafasi ya nne kwa mshiriki kutoka Tanga, Jackson kumechukuliwa kama maajabu kwa kuwa historia inaonesha kwamba, tangu mashindano hayo yafikie hatua ya 20 Bora, alikuwa ni mmoja kati ya waliopokea misukosuko mingi ya kutoka.

Hata wakati 10 Bora inatangazwa, Jackson alionekana kuingia hatua hiyo kwa staili ya kupenya katika tundu la sindano kwa sababu mara kwa mara alitajwa kuwemo kwenye orodha ya waliokuwamo katika mstari wa kutoka.

Mshiriki huyo wa Tanga, pia alilamba msoto 10 Bora, baada ya kuingia na kujikuta akiwekwa kwenye mstari wa hatari, ingawa alipona na kubaki Saba Bora kabla ya kufanya ‘wandaz' na kutinga Tano Bora a.k.a fainali.

Katika kuingia Tano Bora, Jackson alifanyakazi ya ziada, akisaidiwa na wapigakura ili kumuondoa aliyekuwa mshiriki mwenye kipaji kikubwa, Catherine Ntepa.

Maajabu ya Jackson, pia yalijionesha siku ya fainali ambapo aliweza kukusanya kura nyingi kumzidi Kelvin ambaye aliokolewa na majumuisho ya kura za nyuma ambazo zilimuwezesha kubaki nafasi ya tatu.

Aidha, kwa ushindi wa nne mbele ya Beatrice, Jackson pia anatafsiriwa kuwa alifanya ‘wandaz' kwa kumtoa ‘knock out' dada huyo, aliyelitawala shindano hilo kwa muda mrefu wakati linaanza.

Ushindi wa Pascal, pia nao unatafsiriwa kama maajabu yaliyotokea, kwani wakati anaanza, baadhi ya majaji, hasa Joachim Kimaryo ‘Master Jay' walimuelezea kuwa habebeki katika soko la muziki kutokana na sauti yake ‘kubezi' katika nyimbo za kanisani.

Hata hivyo, ubishi wa Chifu Jaji wa BSS, Rita Paulsen ‘Madam' kuwa Pascal a.k.a Baba Rita ni mwanamuziki mzuri na anaweza kubadilika, ulizaa matunda kwani baada ya staa huyo wa Bongo kwa sasa, kuanza kuimba staili nyingine, alijichotea mashabiki wengi waliomfikisha alipo.

Kutokana na uwezo wake wa kubadilika na kuimba staili mbalimbali, Pascal alipewa a.k.a ya Mzee wa Mavoko, ikiwa ni zawadi ya majaji na mashabiki kukubali sauti yake nzuri na yenye nguvu anapoimba.

Mbali na hilo, Rita ambaye pia ni Mkurugenzi wa Benchmark Production inayoratibu BSS, amepongezwa kwa kubuni shindano hilo kwa kuwa sasa linatoa mwanga mpana wa mafanikio kwa vijana wenye vipaji.

Hata hivyo, Rita ameshauriwa kuwasimamia wanamuziki wake ipasavyo yaweze kufika mbali ili yasije kutokea yale ya akina Jummne Idd (mshindi BSS 2007), Misoji Nkwabi (BSS 2008), Rogers Lucas (BSS namba mbili 2008) na wengineo.

Rita, ameshauriwa pia kuendeleza vipaji vya washiriki wa mwaka huu, kama Peter, Beatrice, Catherine na wengineo kwa kuwa wao wakifanikiwa, ni kielelezo tosha cha mafanikio ya BSS na harakati zake.

Aidha, kubwa lililozungumzwa na wadau ni majaji kwamba wakati mwingine walikuwa wanaelemewa na mapenzi binafsi kwa baadhi ya washiriki na kushindwa kufanya uamuzi sahihi pale ilipohitajika.

Janet Byemerwa wa Makongo, Dar alisema: "Hatukatai mtu kumpenda yule anayekuvutia, lakini kama jaji hutakiwi kuonesha mapenzi wazi wazi. Kubwa ambalo nililiona tangu shindano hilo likiwa kwenye mchujo ni kauli za majaji, kuna watu ambao walipondwa na wanaweza lakini wapo waliosifiwa ingawa hawakuwa na uwezo.

"Tulipofika 10 Bora ndiyo ikawa tatizo kabisa, mshiriki mwenye uwezo mkubwa anapondwa kwa sauti kali tena ya juu, wakati yule ambaye wanampenda wao hata akiboronga wanamsifia tu, kwahiyo tunaomba mwakani mambo haya yasijirudie."

Gazeti hili linampongeza Madam Rita na timu yake nzima kwa kuwezesha BSS kufikia hatua iliyopo. Sisi Ijumaa tunaamini kuwa BSS ni mkombozi wa vijana, pia tunampongeza Pascal kwa ushindi wake. MHARIRI.

http://www.globalpublisherstz.com/2009/10/16/az_bss_2009.html
 
Hakuna kitu Kevin anabidi afanye trainning kwa sana sana, bado kabisa hana international quality yeyote , vocals zake labda kwa Bongo ndio kali , lakini huwezi sema ni ziko juu kihivyo .

Diction ndio mbaya , anabidi ajifunze kutamka vizuri maneno ya inglish ingawa yeye ndio alikua bora kuliko hata huyo Ms Mtepa .

Kuingia kweney Project fame ajaribu ila sidhani kama atafika mbali, wenzetu wa east ni wanauwezo mkubwa wa kuimba. Hemedi alifika fila tuu sababu ya looks ila live alikua ana sound horrible , kwanza nilishanga alifikaje , huyu Kevin sidhani look yake ina weza mfikisha mbali.

Angalia mshindi wa Project fame huyu Mrwanda , vocally hawezi shindana kabisa na yule Jamaa wa pili wa Kenya ila kilicho msaidia ni looks tuu.

Huyu Kevin hawezi hata mfikia huyu demu aliye tuwakilisha Project fame, Illumitana kwa vocal na hata diction , na still Illuminata kila siku alikua kwenye probation.
 
You are not sure, haikuwahi hata siku moja kuonyeshwa idadi ya kura kwa BSS ya mwaka jana, tell us something else.
 
Kuna kitu kimejitokeza kwenye ushindi wa huyu dogo ambacho watu wengi hawakukiona, kura ndio zimembeba na si uwezo. Tofauti na miaka mingine shindano hili mwaka huu lilipata umaarufu sana mikoani hasa mikoa iliyokuwa na wawakilishi. Ukilinganisha dar na mwanza kwa mfano ambapo mashindano ya bongo star search yanaangaliwa na watu wengi mwanza zaidi ya dar, hii inatokana na ukweli kwamba kwa dar watu wana option ya kuangalia american idol, so u think u can dance na takataka nyingine nyingi(mbishi aende DSTV aulize idadi ya wateja wa dar na mwanza) hivyo hawashoboki na BSS kihivyo hata wakiangalia. Kingine watu wa mikoani ni likely kupiga kura kuliko hapa dar, kwanza kwa kuwa mikoani watu wanajiona wapo karibu na mshiriki kuliko dar hivyo kumpigia kura mshiriki wa mkoa wao ni rahisi zaidi ya dar. pia kuna ka element ka dar against mikoani ambapo mikoa yote inaungana kuashindana na dar linapokuja suala la kushindana, kwao ni bora mshindi atoke mkoa mwingine wowote kulikoni dar.
Hivi vigezo vya kura vitatosha kumfanya mtu kama pascal awe star kweli?
 
Haya ni majungu, acheni hizo Ritha toka mwazo alisha jua Kevin sio mshindi. Kwa walio fuatilia watakua wanaua kabisa kuwa ila siku baada ya show waliku wanaoneysha idadi ya kura , hakuna siku hata moja Kevin akaonekana ana kura nyingi ,sasa iweje eti Kevin aandaliwe wakati matokeo ya Kura tulikua tuna yaona kila siku?

Halafu ile sio show ya Ritha kama yake pekee ,ile ina wadhamini wakubwa kama VOdacom na TBL , wote hao sio wajinga kumuachia Ritha ajiamulie anavyotaka sababu eti yeye ni exective producer.

Watu wengi ni wa kwanza kulalamika wakati ukiwauliza kama walivote utakuta hakuna hata mmoja aliye vote .

Kuhusu suala la Misoji Nkwabi kwamba alipewa, Kwanza kabisa Misoji ali perfrm bonge la nyimbo " I will always love u" na kuiimba vizuri sana kiasi cha watu wote kumkubali, na pia, kura zote zilikua zinaoneyshwa na mara zote Misoji alikua anaongoza,
Naomba muwe na uhakika na manacho sema.
nakubaliana nawe....haya ni majungu tu, mwanzaoni ni hawahawa waliokua wanaiponda, sasa wameumbuka baada ya onesho kung'ara , swala la upendeleo kama wangetaka wangedanganya tu......kwani nani alikua akimonitor kura za wananchi, ni wao wenyewe kamati ya BSS, WALIHISI KUNA WATU WANGEPIKA MANENO WAKAWAKATA KILIMILIMI.
ongera Ritha, hongera kamati nzima ya BSS, mmejitahidi. maana Mwanzoni Habari coparation walianzisha kampeni chafu dhidi yenu, lakini mmesimama nakufanikiwa.
Misoji anajua kuimba, hakukuwa na mfano, hata washiriki wenyewe waliridhia ushindi wake.
 
You are not sure, haikuwahi hata siku moja kuonyeshwa idadi ya kura kwa BSS ya mwaka jana, tell us something else.

wewe lazima unamatatizo ya kumbukumbu, kila mwaka huwa wanaonesha idadi na mwenendo wa kura za kila wiki.
 
acheni majungu jamani nakubaliana kabisa na mtoto wa kishua hoja zake ya kuwa wengi hampigi kura mmekalia kupika majungu mwanzo mwisho... kila mmoja wetu alijua anachukua cassian sasa mambo ya kevin kuandaliwa yametoka wapi??? kura zenyewe hazikuonyesha kuwa alikuwa na chnace hata ya kuwa wa pili jamani. mngesema peter msechu sawa ila sio kevin.... ushindi ulienda kwa haki na hakukuwa na upendeleo wowotw acheni majungu jamani hayajengi
 
Majaji walitumia siku ile kuhitimisha au ni mapenzi binafsi ya nyie watazamaji mkaja na matokeo yenu ukimbini kuwa Pascal ndo mshindi.
Nilishangaa supa staa AY alivyo panda jukwaani alitegemea atashangiliwa watu ziiiiiiiiiiii wanamwangalia tu dah kila akijaribu kukonga nyoyo za watu lakini wapi.
Kweli Fidel,unajua A.Y amezaliwa na bahati sana lakini mi najua huyu jamaa ni supa star with under ground qualities,kuna vitu vingi vya kisupa staa jamaa anamiss pamoja na kusafiri sana lakini swaga zake awapo on stage mi huwa bored!!!
 
acheni majungu jamani nakubaliana kabisa na mtoto wa kishua hoja zake ya kuwa wengi hampigi kura mmekalia kupika majungu mwanzo mwisho... kila mmoja wetu alijua anachukua cassian sasa mambo ya kevin kuandaliwa yametoka wapi??? kura zenyewe hazikuonyesha kuwa alikuwa na chnace hata ya kuwa wa pili jamani. mngesema peter msechu sawa ila sio kevin.... ushindi ulienda kwa haki na hakukuwa na upendeleo wowotw acheni majungu jamani hayajengi
Bamutu mie simo,nilichosikia ni kuwa kunamtu alitakiwa kupewa endapo zisingetiliwa maanani kura za mashabiki,kuhusu Kelvin mi sijui,ila kwanini wote wamzungumzie yeye,au ndio hapendwi na wote?
 
lisemwalo lipo ila mimi kwa upande wangu sikupiga kura, nilikuwa nasubiri watu wamchague mshindi halafu nilalamike kuwa amependelewa
 
Kuna kitu kimejitokeza kwenye ushindi wa huyu dogo ambacho watu wengi hawakukiona, kura ndio zimembeba na si uwezo. Tofauti na miaka mingine shindano hili mwaka huu lilipata umaarufu sana mikoani hasa mikoa iliyokuwa na wawakilishi. Ukilinganisha dar na mwanza kwa mfano ambapo mashindano ya bongo star search yanaangaliwa na watu wengi mwanza zaidi ya dar, hii inatokana na ukweli kwamba kwa dar watu wana option ya kuangalia american idol, so u think u can dance na takataka nyingine nyingi(mbishi aende DSTV aulize idadi ya wateja wa dar na mwanza) hivyo hawashoboki na BSS kihivyo hata wakiangalia. Kingine watu wa mikoani ni likely kupiga kura kuliko hapa dar, kwanza kwa kuwa mikoani watu wanajiona wapo karibu na mshiriki kuliko dar hivyo kumpigia kura mshiriki wa mkoa wao ni rahisi zaidi ya dar. pia kuna ka element ka dar against mikoani ambapo mikoa yote inaungana kuashindana na dar linapokuja suala la kushindana, kwao ni bora mshindi atoke mkoa mwingine wowote kulikoni dar.
Hivi vigezo vya kura vitatosha kumfanya mtu kama pascal awe star kweli?
Kwa mtu kama mimi,hata kama nipo Dar,huwezi niambia nimpigie kura mtu dhaifu na asiye na uwezo kama Mbati eti kisa tuu anatoka mkoa mmoja na mimi,wewe hata siku ya pambano la Kaseba na Cheka bila shaka ungeniambia nimshabikie Kaseba kisa tuu katokea Dar!!
 
Tetesi nilizozipata hivi karibuni ni kwamba baadhi ya majaji wa bongo star search wameujutia uamuzi wao wa kukubali kuwa kura za mashabiki ndio zitakuwa muamuzi wa mwisho,na si maamuzi ya majaji,ukweli ni kwamba kwenye kabinet ya majaji kulikuwa na baadhi yao waliopenda ile tuzo iende kwa mtu ambaye walikuwa wameshamuandaa,lakini endapo maamuzi ya majaji yangechukua nafasi naamini kabisa pale diamond pasingekalika,poleni sana majaji na sera zenu za ukandamizaji,naomba hizi sera za kura zidumishwe hadi kwenye ma miss.Mwisho nampongeza sana bwana Pascal Cassian kwa kuibuka mshindi wa haki!!!

Utaratibu huu wa kura ungekuwa unatumika hadi kwa mashindao ya Miss Tanzania, nina uhakika tungepata washiriki wazuri sana wa kutuwakilisha!
 
hata mimi nilipenda Kelvin Mbati ashinde sema watanzania wengi hawakuliona hilo.Cassian yeye aliamua kubadilika kutoka kuimba nyimbo za injili na kuhamia upande mwingine.Hivyo naamini ndio maana wengi wakamchagua ambavyo sio mbaya.Ninachotaka kusema hapa ni kile kinachosemwa kipaji.je ni kipi kama watanzania tulikuwa tunakitafuta?je ni kipaji cha kuimba au ni kitu gani?kama ni kipaji cha kuimba wote walionyesha kuwa nacho sema zaidi sana MSHINDI NAMBA MBILI PIA ALIKUWA NA UBUNIFU SANA.Sasa Kelvin yeye alijikita kwenye nyimbo za kiingereza na wale wanaopenda kitu kama hicho kama mimi nilitamani ashinde.Lakini watanzania wengi walipenda Cassian ashinde kwa kuwa aliimba nyimbo zaidi za kiswahili tena za kileoleo.basi tusonge mbele kwani kila mtu anao utashi wake.
 
Back
Top Bottom