Nasumbulia na tumbo naomba msaada

mchoyo

Member
Joined
Aug 13, 2013
Posts
48
Reaction score
8
Habari zenu wana JF,

Mimi tatizo langu ni hili nasumbuliwa sana na tumbo kushoto na kulia chini ya kitovu, then nina miaka mitatu ndani ya ndoa sijapata hata baby jamani.

Nilicheki utra sound nikaambiwa sina matatizo kwenye kizazi au mfumo wa uzaz mzima nipo okey. Sasa Sijajua kipi kinasababisha nisibebe ujauzito natamani sana mtoto jaman nisaidieni hata wanaojua tiba mbadala help me please.

Nakosa raha sometime sipati siku zangu miezi hata mitano
 
umeshaenda Mico dispensary? pale kuna dr anaitwa Mnyau pia ni dr kule lugalo, nilikuwa na tatizo kama lako baada ya vipimo kusema sina tatizo ila yeye akanifanyia operation kuna vitu vilitolewa na baada ya miezi nane nilibeba mimba na sasa nilipata mapacha, hivyo jitahidi ukamuone naimani atakusaidia. pole Mungu atakusaidia utakuwa mama muda si mrefu
 
asante sana kwa kunitia moyo mico ipo sehemu gani hapa dar?
 
toccara njoo umfahamishe mwenzako ilipo hospitali
 
Last edited by a moderator:
toccara njoo umfahamishe mwenzako ilipo hospitali

niko online my dear, mimi alinitibu lugalo ila sasa anapatikana sana hapo mico iko sinza palestina na tegeta ingawa mico zipo nyingi ila hizo mbili ndiyo anapatikana sana
 
Msipende kwenda kutumia makemical tuu jamani tumiae vyakula mbadala angalau hayo madawa ndoo baade yanakuja kuzua matatizo mengi katika miili yetu
 
ok asante nitamcheki cnza my dia then ntakujulisha itakavyokuwa.
 
Pole sana kutokana na maelezo yako una matatizo ya mambo ya kiswahili (Sayansi ya Giza) nitafute kwa wakati wako na pia unaweza kunitumia Email baruwa ya pepe email yangu hii hapa fewgoodman@hotmail.com

Pole dada, Ngoja nikuitie MziziMkavu, utafiti hawezi mambo haya
Habari yako bibie Prince?
 
Last edited by a moderator:
Tatizo lako linatatulika dada, tafadhali mwone daktari bingwa wa kina mama alie karibu na uliko, kama ni mjini wako wengi ila kuna wengne mhh! uliza wengine upate mwenye ueledi vizuri
 
asante sana kwa kunitia moyo mico ipo sehemu gani hapa dar?

wahi hospitalini bwana, huyo Mnyau ni doctor bingwa wa magonjwa ya wanawake, baada ya kupimwa na kuonekana sina ugonjwa ingawa nilikuwa naumwa upande wa kushoto siwezi kulala wala kukaa yaani yale maumivu hayaelezeki, yeye akanipasua na vitu vilivyotoka humu tumboni kama unaimani ndogo utatembea kwa kila mganga kujua nani kakuwekea hayo madude, ila mimi alinipa darasa nikamwelewa na nikarudi tuu kujiuguza na aliniambia utashika mimba na kweli kwa uwezo wa Mungu nikashika. jitahidi uwahi
 
asante dada angu kwa ushauri wako yani ukiliona tumbo langu utasema nina mimba ya miez minne kubwa then gumu ukilishika najickia vibaya sana jaman
 
pole sana mumie nakushsauri kama uko dar muone Dr Ngarina hapo MNH ama [Prof. Kaisi] UKIENDA WODI ya akina mama mama hapo MNH ukiwaulizia hawa utapewa mawasiliano yao. hata Dr Kapona naye ni mzuri sana hebu watafute hawa mumie..........
 
Ninacho kushauri nenda na mmeo mkamuone daktari unaweza kuta tatizo liko na mmeo halafu ww unangaika kupata mtoto kumbe mmeo hana nguvu za kutosha. Na tatizo la sisi wanaume tunatabia ya kujiamini kuwa tunaweza kumbe hamna kitu.
 
pole sana mumie nakushsauri kama uko dar muone Dr Ngarina hapo MNH ama [Prof. Kaisi] UKIENDA WODI ya akina mama mama hapo MNH ukiwaulizia hawa utapewa mawasiliano yao. hata Dr Kapona naye ni mzuri sana hebu watafute hawa mumie..........


Naaaam! Bila kumsahau lane
 
Last edited by a moderator:
ok asante kwa ushaur wenu ntaufanyia kazi nashukuru sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…