Nasumbuliwa na kucha za vidole gumba miguuni.

Nasumbuliwa na kucha za vidole gumba miguuni.

1981

Member
Joined
Feb 2, 2017
Posts
38
Reaction score
21
Habari wana JF.

Naombeni ushauri ninatatizo la kucha za vidole gumba toka mwaka 2015 October.

Nimeshazunguka hospital nyingi hapa Dar es salaam na hata kufanyiwa upasuaji mdogo lakini tatizo limebaki pale pale.

Nilishsenda Hospital nikapima vipimo vyote ikiwemo na sukari lakini nikaonekana kutokua na tatizo lolote.

Napata tabu sana ndugu zangu naombeni ushauri nionane na Doctor yupi bingwa wa tatizo hili na yupo hospital gani.
 
Kuna tatizo la ingrowing nail, hili linatoka na ukataji mmbaya wa makucha na kucha linapoota linapoteza mwelekeo na kuingia ndani ya nyama. Tatizo la pili inawezekana ni fungus.
 
Here with the attached photo.
 

Attachments

  • IMG_20170402_203803.jpg
    IMG_20170402_203803.jpg
    91.9 KB · Views: 285
Here with the attached photo.
Hii mbona ni kama in-growing nail? Nilipata hili tatizo 1995 na sikufahamu tiba mpaka 1998 dr aliponi refer kwa chiropodist ambae alinifanyia upasuaji na kunionya niwe ninakata kucha na nail cutter tu.
 
Kaka huwa nazikata maana zinaota kwa ndani hivyo napata maumivu makali sana.

Nikizikata maumivu hupungua.[/QUOTE
Nenda Muhimbili sijajua chiropodist Tanzania anapatikana wapi.
 
tafuta Vicks VapoRub
uwe unapaka kila siku ndani ya siku kumi,ila badilisha viatu na soksi zote za zamani utupe maana kama ni fangasi hizo soksi zishabeba vijidudu so nunua viatu vipya na soksi mpya
Nashukuru kwa ushauri mpendwa.
 
Habari wana JF.

Naombeni ushauri ninatatizo la kucha za vidole gumba toka mwaka 2015 October.

Nimeshazunguka hospital nyingi hapa Dar es salaam na hata kufanyiwa upasuaji mdogo lakini tatizo limebaki pale pale.

Nilishsenda Hospital nikapima vipimo vyote ikiwemo na sukari lakini nikaonekana kutokua na tatizo lolote.

Napata tabu sana ndugu zangu naombeni ushauri nionane na Doctor yupi bingwa wa tatizo hili na yupo hospital gani.
Tatizo hilo ni kweli ukizikata ndani zinachongoka na shida zaidi ukivaa viatu vya kufunika, na tyr inaonekana kuna infection. Mara nyingi huondolewa kwa upasuaji mdogo, ili ziote upya tena!
 
Pole Sana. Nilipata hilo tatizo miaka zaidi ya 15 ilopita. Nilienda hospital na walinifanyia upasuaji mdogo kwa kung'oa kucha zote za vidole gumba vya mguu. Mara chache huwa inanitokea kucha za mikononi lakini huwa nazikata mapema.
 
Tafuta consultation na PODIATRIST / CHIROPODIST, hawa ni foot and ankle specialist, jaribu muhimbili, aga khan au regency, pole sana mkuu
 
Mimi nilipata shida hiyo pia ila niling'oa zote na zikaanza upya! Tatizo halijajirudia mwaka wa 4 sasa! Nashauri ufanye hivyo pia!
 
Mkishauri habari ya kung'oa kucha mnanikumbusha Dr Ulimboka kama alikuwa na tatizo hili alipata tiba bila ganzi

Sent from my TECNO P5 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom