Kuhusu wire, kuna namna 2 za wiring sasa hivi; ile ya kizamani kwamba ule waya ambao kwa ndani ume contain nyaya 3, neutral, live na earth halafu kuna hi wiring ya kisasa ambayo nyaya zinauzwa moja moja, neutral pekee yake, live na earth as well; now ikitokea ume opt hi ya wire mmoja mmoja ni gharama sana kulinganisha na hiyo ya kizamani, hi ya kizamani ni nzuri in terms of cost na hi ya kisasa ni nzuri in terms of security in case there is an emergence ya wire mmoja wapo kuungua (wire hua haungui, ile insulator/gamba au lile li mpira likipoteza nguvu) unautoa tu wire huo ulioungua na kuubadirisha; sasa kama bajeti yako ni ndogo tumia hizi nyaya za kizamzni, wanauza kwa roler ambalo lina mita kati ya 80 hadi 100, wire wa Tanzania ni mzuri tu, kuhusu switch zote hadi main switch pamoja na circuit breaker nunua tronics au heaves. Switch za pass/tv nk zipo za aina 3 sasa hivi, zile za kizamani ambazo kama pass au charge ya simu ina pin mbili inatakiwa utafute kitu cha kubonyeza kwa juu ili hiyo chaja iingie, halafu kuna switch ambazo inaingia yenyewe bila shida hata kama ina pin 2 pia kuna switch ambazo zina accomodate USB cable kwa ajili ya kuchajia simu bila hata kuhitaji vichwa, yaani kama upo kwenye basi tu. NImetumia lugha rahisi ili uelewe vizuri, kazi ni kwako sasa.