Natafuta kazi nimesomea fani ya umeme

Natafuta kazi nimesomea fani ya umeme

Samahani kwa kuingilia uzi wa bwana Mkubwa ila kama utawiwa kunisaidia pia namm ntashukuru mimi pia natafuta ajira walau nipate chochote Nina diploma ya umeme nimemaliza muda kidgo.
umemaliza diploma mwaka gani,

una experience na umeme wa viwandani (machines/control systems)?
 
Mkuu; Nimeandika In short na km ukisoma vzr hayo uliyoyauliza yapo kasoro uzoefu: okay
Nimemaliza Mbeya University of Science and Technology course ni bachelor degree of Electrical and electronics Engineering mwaka 2019;
Ninauzoefu wa field TANESCO na viwandani na Wiring za majumbani pia nafaham; Pia baada ya kumaliza nimefanya kazi kwa kujitolea kwenye kiwanda Cha MW rice Miller hapa Morogoro kwa muda wa miez 4,,,,nimeacha hapo kutokana na ugumu wa mazingira ya kazi walikuwa hawanilipi hata Mia,,,,kwasasa nipo mtaani Sina kazi yyt natafuta,,
Kwa sisi Professional Technicians (Wajumbe) huwa hatupaiti kwa jina baya eneo tulilopitia. Hata kama hawajakulipa, usingewataja kwa jina. Maana kukaa kwao kwa miezi minne imekuongezea kitu cha kuandika kwenye CV. Jifunze hili, that's unprofessional.

Pia pole kwa changamoto za kutafuta kazi. Endelea kufuatilia Jukwaa hili kwa michongo mingi hutokea hapa. Nilipata kazi miaka 7 iliyopita kupitia Jukwaa hili.

Mjumbe Daraja Makofia.
 
Kwa sisi Professional Technicians (Wajumbe) huwa hatupaiti kwa jina baya eneo tulilopitia. Hata kama hawajakulipa, usingewataja kwa jina. Maana kukaa kwao kwa miezi minne imekuongezea kitu cha kuandika kwenye CV. Jifunze hili, that's unprofessional.

Pia pole kwa changamoto za kutafuta kazi. Endelea kufuatilia Jukwaa hili kwa michongo mingi hutokea hapa. Nilipata kazi miaka 7 iliyopita kupitia Jukwaa hili.

Mjumbe Daraja Makofia.
Shukran kwa kunifahamisha kitu kipya sikuwa najua b4...Pia naweka masahihisho hapo kutokana na uelewa uliojitokeza kwa watu ambao sikutarajia "Ni hivi tangu mwanzo naomba kufanya hapo walisema ruksa lkn hawatonilipa kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wao,,,Mimi nilikubali kwa lengo la kupata uzoefu pamoja na kutafuta connection kwahy nilifanya kadri ya uwezo wangu nikaishia Hy miezi minne ingawa nilikuwa nataman kuendelea km wangenilipa hata angalau 7K na kuendea per day ningefanya kwa mda mrefu tuu... Lakini haikuweza kuwa hivo.
Na nimetaja hapa nikiwa na lengo la kuweka sababu ya kuacha maana ningeweza kuulizwa kwann uliacha Pia sikuwa nafaham km kutaja eneo husika ni tatizo: Naomba Samahan.
Pamoja "MJUMBE"
 
Kwa sisi Professional Technicians (Wajumbe) huwa hatupaiti kwa jina baya eneo tulilopitia. Hata kama hawajakulipa, usingewataja kwa jina. Maana kukaa kwao kwa miezi minne imekuongezea kitu cha kuandika kwenye CV. Jifunze hili, that's unprofessional.

Pia pole kwa changamoto za kutafuta kazi. Endelea kufuatilia Jukwaa hili kwa michongo mingi hutokea hapa. Nilipata kazi miaka 7 iliyopita kupitia Jukwaa hili.

Mjumbe Daraja Makofia.
Pamoja MJUMBE kweli hili jukwaa ni Msaada sanaa kwetu sote
 
Samahani kwa kuingilia uzi wa bwana Mkubwa ila kama utawiwa kunisaidia pia namm ntashukuru mimi pia natafuta ajira walau nipate chochote Nina diploma ya umeme nimemaliza muda kidgo.
Electrical technician anahitajika Mamlaka ya maji Korogwe - Tanga, ngoja nicheki tangazo lao kama bado muda wake haujaisha halafu nikutumie.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jaribu pia kucheck Kama Kuna mradi wowote ule ndani au nje ya halmashauri uliyopo.

Na uwe mtu wa kujichanganya/kujiattach na kua tayari kujitolea upatapo fursa ya kushiriki mradi/kazi yoyote inayoendana na professional yako.

NB: kua na ujasiri wa kuonana na hao mameneja wa miradi na kubadilishana nao mawazo kwa lengo la kupata nafasi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kujitolea Ni ubwege, no free

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sijafanikiwa kupata tangazo kwa haraka, nimeomba mtu wa karibu anitafutie then anitumie.
Ili tusichelewe naomba nikutumie namba PM ili uwasiliane na huyo mtu moja kwa moja kwakuwa mm nakuwa bize sana.
Naamini utafanikiwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Bless sana bro hata ikitokea pia sijafanikisha lkn I can see your spirit kwa kujaribu. Endelea na moyo huo huo mkuu Mungu akubariki.
 
Back
Top Bottom