Natafuta Mbuzi bora wa Nyama Madume aina ya Savanna na Boar hapa Tanzania

Mkuu habari za leo, unaendeleaje na shughuli za ufugaji?
Kwa sasa una breed gani shambani kwako na je uko mkoa gani? Ningependa kujifunza zaidi kuhusu ufugaji. hasa wa mbuzi
 
Amina na iwe baraka kwetu sote na mazizi yetu tubarikiwe tufikie malengo yetu na uzazi uendelee ktk mifugo yetu. Kama upo Dar kabla hujaagiza hao Mbuzi karibu kwangu uwaone vyema ili uwezi kuagiza kitu stahiki ktk ufugaji wako.
Mkuu, nimepitia comment zako kwenye huu Uzi ni wazi wewe ni mwema Sana na mwenye roho 'ya kila mtu apate'.

Umenifanya nitamani kufuga Mbuzi, natamani nije nikutembelee nije nijifunze kwa vitendo.
 
Angalizo,

Endapo utaenda kununua mbuzi basi jaribu kujua pia mazingira ukuaji wake. Na mazingira unayotegemea kuwafuga..

Mfano, mbuzi ambaye muda mwingi yupo ndani ukamnunua na kwenda kumfuga kwa kuchungwa porini, hudhoofika haraka na hufa.

Lakini pia, mbuzi wengine wameshazoea raha. Wanakula na kunywa kwa wakati. Ukinunua na kwenda kumtenga hupata sana stress.

Isiolo ni mbegu bora sana. Wana masikio makubwa, nikisema makubwa ni makubwa kweli. Wavumilivu.

Ila kuwa makini sana na kichaa cha mbuzi. Unaweza kumnunua mzima, unafikisha kwako shambani akili zinamruka. Kula hali, ni kupiga kelele tu. Anadhoofika bin taaban, kichaa hakiponi..

Chinja, kula nyama. Haina athari kiafya. Umekosa mbegu, umepata kitoweo. Bora hasara nusu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…