Natafuta Mke halisi wa kuoa ALIYEOKOKA


hivi minaamini kuwa mwenye uwezo pekee wa kutuokoa ni Yesu Kristu kutoka utumwa wa dhambi , wee mtoa mada kwani aliyekwambia umeokolewa ni nani ,?Yesu pekee ndiye aliyemsamehe yule mwanamama aliye iosha miguu ya Yesu kwa machozi yake na akaipaka mafuta kwa nywele zake asa nyie mnaojidai oohh mii nimeokoka unajifananisha uwezo wako na Yesu ?, kweli nyakati hizi kuna manaabii wa uwongo wengi watakuja hata kwenye biblia imeandikwa ole wenu sasa kina KIDOMA ,
 
duu mkubwa unaonekana hujaokoka kabisa yaaan
Ila sio mbaya dada yangu ni mlokole lakini kaathirika na vigezo vyote anavyo vp nimwambie au unataka mlokole labda unazani atakuwa bikra
 
Baada ya kuandika hizo sifa zote na kumaliza, bado unahisi umeokoka??
Nilidhani yule mwokovu ni yule anaemtegemea Mwokozi wake na kushukuru kwa kila jambo!
Bali ungalimo unaishi kwa SHERIA ..............!

cha motoooooo
wewe umeokokaa??
If so ntaomba tuwekane sawa kufuatia hoja zako

tatizo nililoona linatokana na mtazamo wako na/au mtazamo wa wengi kama wewe!

Najibu hivi bado ninaamin nimeokoka maana tafsiri ya kuokoka ni rahisi tu ya kuwa ni kumkiri Yesu kwa kinywa chako na kumwamini moyon mwako. hiyo ni rahisi laki ngumu ni kudumu katika wokovu, hiyo ni process yenye kupanda na kushuka huku safari ikiwa inaendelea.

Pili bado ninamtegemea MUNGU. Iko wazi kwamba ukimuomba Mungu hakika anajibu, but anajibu kwa style gani na lini?
anaweza kujibu saa hiyohiyo, baada ya siku kadhaa wiki, mwezi mwaka au hata miaka KIKUBWA ANAJIBU KWA WAKATI WAKE NA UTASHI WAKE!!
Lakini Je? anajibu kwa style gani, kwa ndoto, maono, ishara, neno, unabii, kutuma wajumbe.
Na je unaweza kuthibitishaje kama jibu hili limetoka kwa Mungu wala si shetani au mawazo na mtazamo wako?
hilo nalo nin somo linalochanganya wengi

Hivyo, njia nayoitumia ni mojawapo ambayo Mungu huitumia pia

naomba unitakie baraka la una mchnga na hoja bado karibu!!
 

Kwa hiyo unakubaliana na Kapongo kwamba hapa duniani kusema umeokoka ni kujidanganya?kama we mlokole mwenyewe umekiri hapo nilipoweka msisitozo?Ndugu kumkiri Kristu tu kwa kinywa halafu usimuhishie haikupi chochote katika Roho Imani bila matendo imekufa.Ikiwa bado nina uhai nawezaji kupiga vita vilivyo viovu na kuvikwa taji nikiwa hai?!
 

kwa maneno haya wewe unaweza kweli kujiita mlokole kakangu?na kama huuu ndo ulokole bora nibakie kuwa Mkristu wa kawaida nisubiri kutoa dinari yangu.hivi si hatukujui kidogo tu umemsengenya mtu hapa unajua madhara ya ulimi wewe?umewahi kuwakuta fraglecto delicto hadi kusema huyo kigogo anamchukua huyo mama?Ukweli huwa nasemaga walokole ni wanafiki ni mfano ni huu,.Kila la kheri kaka mlokole.
 

aksante sana bwana kiplagati kwa mausia yako
inaonyesha huwaamini wasomaji wa jf kabisa na kama anaweza kuwepo mwenye hekima na aliyeokoka kama wewe

hata hivyo nauchukua ushauri wako kwa tahadhari kubwa na naahid kuupokea moyoni kwa utendaji
 
mmh sasa wewmaonekana utakuja kuwa mwijilist machachari unayetumia vifungu vya biblia kuhararisha yale unayoyataka
maana unavyojicganganya mwenyewe hata nimeshindwa nikujibu au ni comment kwa lipi

hata hivyo siku moja neema ya Mungu itakushukia utaja yafaham mambo yote hayo kwa usahihi

hata mm nilikuwa mbishi na mpingaji kama ww lakini ni katika kubisha kwa lengo la kutaka kujua ndipo nilikutana na huyu Yesu!
 
wandugu
niliahidi toka moyoni mwangu kwamba nimngejibu kila mchangiaji lakini naona naanzakuchemsha

hata hivyo nitajitahidi kufanya vile kwa kila mtu atakaye nigusa

hatahivyo, kunamichango mingine ambayo majibu yake sahihi ni kukaa kimya
 
Sasa kwa huo ulokole wako hautaishia kwenye uchungaji nami si itanibidi niache kazi niwe mama mchungaji tumtumikie Mungu wetu na tulishe kondoo wake.. Inakuwaje hapo? Mungu amekuonyesha mke wako atapatikana JF???.. Haleluyaaaaa....!
 
Sasa kwa huo ulokole wako hautaishia kwenye uchungaji nami si itanibidi niache kazi niwe mama mchungaji tumtumikie Mungu wetu na tulishe kondoo wake.. Inakuwaje hapo? Mungu amekuonyesha mke wako atapatikana JF???.. Haleluyaaaaa....!

Mmmmh umeshakuwa mtabiri au nabii? maana umekwisha ijua mipango ya Mungu hata kabla haijatokea na usivyopenda kumtumikia Mungu au labda kwa kuogopa kwako? mmmh!

SIJAFUNULIWA KUWA mke yupo JF bali ninatafuta kama unavyoweza kutafuta sehemu nyingine yoyote ila sharti Wokovu; upo mdada?

but be serious m nipo serious na issue hiyo, sawa?
 
duu mkubwa unaonekana hujaokoka kabisa yaaan
Ila sio mbaya dada yangu ni mlokole lakini kaathirika na vigezo vyote anavyo vp nimwambie au unataka mlokole labda unazani atakuwa bikra

Nashukuru maana umejiuliza maswali, umejihoji na mwisho wa yote umejijibu mwenyewe

kila kheri kwako!
 

Aaah sio kama sipendi kumtumikia Mungu, ila maisha haya na mama uchungaji mmh... Mume aache kazi alishe kondoo, mke aache kazi amsaidie mume kulisha kondoo.. Tutaishi kwa sadaka za waumini au inakuwaje? LOL... Nakutakia kila la heri...
 
Mkuu Kidoma,
I wish you all the best, utapata tu!
Watu wangapi wamepata wachumba humu JF na criteria zao zilikuwa more ridiculous kuliko huyu bwana.
Naamini kuna walokole huku na hata kama watakuwa hawana criteria nyingine wajaribu tu huwezi jua...
 

Mimi ni shahidi wa YEHOVA.
Ninachoona ni kuwa umeweka vigezo kwa macho ya kibaadamu sana, na kusahau kuwa MKE MWEMA utoka kwa BWANA.
Yesu hakuja kwa watenda mema, bali kwa wakosaji ili waokolewe nae, hivyo unaweza kupata MKE ambae si Mlokole kama unavyolazimisha, ila kupitia kwako jina la BWANA litainuliwa. Kwani NDOA kwangu mimi ni kama IBADA.
Urembo, Elimu, na vingine si sababu ya kuwa yu mke mwema, kama walivyosema wachangiaji wengine na kumbuka maneno ya muuimbaji wa nyimbo za injili, aliimba Mke mwema hutoka kwa BWANA.
Msisitizo wangu huyo Mke mwema utapewa na Bwana ili mapenzi yake yatimie, nakutia moyo usugue goti lako chini ukimlilia BWANA akupatie Mke mwema, si kwa mapenzi yako ila mapenzi yake, BWANA, yatimizwe.
 
SIFA ZA MKE MWEMA


Kitabu cha mithali 31 kuanzia msitari wa 10 hadi 31 kimeelezea sifa mbalimbali za mke mwema, tuangalie kwa uchache sifa hizo kwa kuzichambua katika maeneo tofauti. 1. Imani Mithali 31:26, 29, 30 Mke mwema anayashika na kuyafanyia kazi maneno ya Mungu na ni mtu ambaye anamtumikia Mungu kwa moyo wake wote na akili yake yote. Anatafuta makusudi ya Mungu katika maisha yake na kuyafuata. Zaburi 119;15 2. Ndoa Mithali 31:11-12, 23, 28 Mke mwema humuheshimu mume wake na anahakikisha anamtendea mambo mema siku zote za maisha yake. Ni wa kuaminika na msaidizi kwa mume wake. Efeso 5:22-24, 1Petro 3 3. Malezi Mithali 31: 26, 28 Mke mwema anawafundisha watoto wake njia za Mungu na pia anawatunza kwa upendo. Huwafundisha kwa hekima na kuwaelekeza njia iwapasayo kuiendea. Mithali 22:6 4. Huduma Mithali 31:12-15, 17, 20 Mke mwema anamhudumia mume wake na familia yake yote kwa ukarimu na upendo. Anahakikisha wanapata chakula kilicho bora na chenye afya. Ni mtu mwenye huruma na ukarimu. 5. Mali Mithali 31:14, 16, 18 Mke mwema anatafuta kwanza ushauri wa mumewe kabla ya kutumia fedha na pia anafanya manunuzi kwa hekima. Ni muangalifu kununua bidhaa zenye ubora kulingana na mahitaji ya familia yake.Efeso 5:23 6. Nyumba Mithali 31:15, 20-22, 27 Mke mwema ni mtu anayeifanya nyumba iwe mahali pa kuishi. Anatengeneza mazingira ya kuvutia kwa familia yake na wageni wote na anawahudumia watu wake wote kwa ukarimu. 1pet 4:9, Ebrania 13:2


Na hii nimechukua kutoka kwa Ndugu Kiplagati26 mchangiaji hapo juu.
 
Bwana Yesu asifiwe. Wasiliana nami kwa e-mail hii.makojuli@yahoo.com

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…