Natafuta Nafasi ya Kujifunza na Kufanya Mazoezi ya Kazi katika Fani ya Business IT

Natafuta Nafasi ya Kujifunza na Kufanya Mazoezi ya Kazi katika Fani ya Business IT

kingphisher

Member
Joined
Nov 30, 2024
Posts
45
Reaction score
79
Husika na mada tajwa hapo juu. Mimi ni mhitimu mwenye shahada ya Business Information Technology. Natafuta nafasi yoyote ambapo naweza kujifunza kazi kutokana na taaluma yangu. Ingawa nimejifunza mambo mengi nikiwa chuoni, natamani kupata sehemu ya kufanya mazoezi ya kazi, hasa katika upande wa networking. Aidha, niko tayari kujifunza na kushiriki katika majukumu mengine yanayohusiana na IT, isipokuwa programming.

Kwa kuwa nina utaalamu wa Business IT, pia ninaweza kufanya au kujifunza zaidi kuhusu masuala ya data science na data analysis kwa kutumia zana kama Power BI na Tableau. Hivyo basi, ninaomba msaada kutoka kwa yeyote mwenye uwezo wa kunisaidia katika hili.

Networking inahitaji mazoezi ya mara kwa mara, na nikikaa bila kufanya mazoezi, kuna uwezekano wa kusahau. Naomba usaidizi wenu wakuu. NAWASILISHA.

mawasiliano:
phone: (normal call, text and whatsapp) 0620224372.
location: nipo Dar es salaam.
 
Back
Top Bottom