Natafuta vijana wa kufanya kazi za shamba.

Natafuta vijana wa kufanya kazi za shamba.

Trekta ni mkombozi kwa sehemu yenye matatizo ya nguvu kazi.

Umenichekesha kweli,

Trekta litalinda nyani/nguruwe? Je baada ya mavuno trector litalinda mavuno? Kuna saa za trector na saa za nguvu za mtu kaka.
 
Asante kwa mchango wako wa mawazo mkuu, gharama ya wastani kulima ekari moja kwa tractor ni 40,000/= . Shamba jipya ni ngumu kutumia tractor, option kusafisha kwanza kwa mikono ambapo bei ndo hiyo inakuwa 60,000/= kwa ekari moja. Pengine kwako hiyo ni pesa ndogo sana ila ni muhimu kutambua kuwa unapofanya biashara faida inategemea sana gharama za uzalishaji, na hiyo 60,000/= nayo imepatikana kwa kazi ngumu na kujibana vilevile. Mimi nilidhani ni vizuri kugawana hiki kidogo na watanzania wenzetu kwa kupeana ajira hizi katika kilimo, kuna taarifa kuwa katika baadhi ya sehemu wakenya wanakuja wanafanya hizi kazi mashambani. Samahani kama umekwazika mkuu!!

Mkuu mimi nilikuwa nalima tumbaku Urambo. Msimu Ukianza tunachanga na wezangu tunawafuata warundi. Hiyo ni hela nyingi sana Kwao ukijumlisha na chakula. Kwa kilimo hiyo hela ni reasonable kabisa. Ila toka ulilipopita operation Kimbunga nguvu kazi imepungua saana huku. Ulizia hata wasukuma unaweza wapata na wanapiga kazi saana.
 
embu niambieni production per eka ikoje,kwa kilindi na tanga
 
tpmazembe, namimi nalima huko handeni Komkonga. Nakabiliwa na tatizo la nguvukazi pia, kama unavyojua ilivyo vigumu kuwapata wenyeji na ukizingatia na hali ya mvua inavyonyesha sasa inakuwa ngumu kuwashawishi wakubali kuingia shambani. Labda tushirikiane tu kutafuta watu wa mikoani kama ulivyoamua tayari, ila nadhani namna nzuri ya kuwalipa ni kwa kipimo cha kazi. Mfano mimi pale nimekuwa nalipa 60,000/= kwa kila ekari moja inayofyekwa na kulimwa (Bado ni pori sehemu kubwa). Cha kufanya ni kuwatengenezea kambi hukohuko shambani, gharama za chakula ni sehemu ya malipo ya kazi yao. Kilimo kikiisha wanarudi kwao kupumzika hadi utakapowahitaji tena. Challenge kubwa ni namna ya kuwapata, tuwasiliane kwa pm tushirikiane kuwapata kwa wingi!
Nahitaji namba yako mkuu
 
Back
Top Bottom