Unajua mficha uchi hazai.
Wewe weka shida yako wazi.Unaweza kukuta mtu akakupa Buree bila hata kukudai.
Humu wote usituone hivi tuna madeni telee,lla tumo tu humu tunajifariji.Na ndio maana unaweza kukuta member anaingia humu yeye ni matusi mwanzo mwisho,yaani anahamisha tension za nyumbani analeta humu inakuwa sehem ya burudani.Na ndio maana Jf hakuna anaenuna labda awe wa Mkoani.
Watu wanamatatizo ya kifamilia humu wakikuambia utaona bora uzikwe,ila humu Jf ni sehem ya faraja,unaweza kukuta mtu anachangia mada ya mamilioni lakini anamadeni akiona sim inaita roho inadunda.
Huyu alieleta sim sijui nani,maana zamani anaekudai lazima aje,na ukimsikia mbio,ila siku hizi kazi kweli.Ugonjwa wa moyo umeongezeka kwa sim za tunaodawia.
Nakushauri weka wazi,Pesa sio utatuzi wa matataizo yako,unaweza kupewa ushauri ukawa ni bora kulikopesa,au ukakupa muongozo wa namna ya kulitatua.Unakuta wengi tunafikiria kwamba pesa ndio inatatua kila kitu,na ukiwa na dhana hii basi huto piga hatua,itakuwa wewe ni mchumia matatizo na unakwepa changamoto,na anaekwepa changamoto za kimaisha basi siku zote ni mtu wa huzuni.
Ni sawa na kuomba mkopo Bank bila ushauri wa kina,ukizipata hujui hata umefafanya nini,badala ya kutatua tatizo ndio unaongeza.