Pia hujawaambia utakaanao kwa muda gani ili u-confirm ndoa. Maana ni rahisi sana ku pretend ili mwanamke aendane na wewe katika kipindi cha matazamio ila baada ya hapo ndio utajua ni yeye uliyemchagua au umechaguliwa na mtu.Nimewahi kuweka tangazo humu miaka minne iliyopitaa la kutafuta mke ila kabla ya kufanya maamuzi nilipata mtu ambae tulikuwa na mahusiano zamani kidogo.
Malengo yalikua ndoa Ila tabia zake zilinishinda, busara na heshima vilikua vidogo sana kwake.
Nikapata mwingine tukadate kama mwaka hivi ila nae hatukuweza kuoana.
Jf ni sehemu ya great thinkers hivyo nina amini nitapata mwenye busara na heshima humu.
Sifa zangu;
*Umri nayemhitaji Usiwe zaidi ya miaka 35
- Nina elimu ya shahada ya kwanza
- Ninaishi Daressalaam, japo nasafiri mara kwa mara Dodoma( hivyo ni Dar na Dom).
- Nina Nyumba mbili Dom na Dar na magari mawili( Canter na Kluger).
- Dini yangu ni Mkristo japo sibagui Muislamu( nipo tayari kuishi na dini yoyote). Heshima mbele, nasisitiza hili.
- Ninafanya shughuli za kilimo sana, ni mkulima mkubwa Dom.
* Single Mother's ni ruksa, Ila awe mkweli sababu ya kuwa single mother. Nikigundua aliongopa basi niwe mkweli tu hatutaendelea tena.
- Awe tayari kusafiri Dar na Dom kwa mwezi angalau mara 2, hivyo kwa asiyependa safari au mvivu wa safari itakua ngumu kuwa nae.
- Sibagui elimu Ila asiwe ameishia darasa la 7, minimum kabisa awe Form 4
Naweka wazi tena, awe tayari pia kushiriki shughuli zangu za kilimo na kuna muda inaweza kumpasa kukaa huko hata wiki 3 mfululizo kwa maana kuna kipindi nakua nimesafiri nje ya Dom na Dar. Ila Kama ni mfanyakazi basi hakuna shida, ila Kama hana kazi basi hiki kipengele kitamhusu.
Natanguliza shukrani.....
Nakutakia kila lakheri upate mke mwema ila nikukumbushe tu kwamba mke mwema hatoki jf "mke mwema hutoka kwa Mungu" haina maana jf hayupo ila unapaswa kumshirikisha Mungu kwa karibu mno katika mchakato huu.