Nina miaka sita toka niajiriwe kwenye kampuni flani,
Mshahara wangu ni tsh 800000 kwa mwezi ambao ukikatwa na makato pamoja na marejesho ya mkopo napokea tsh 421000 kwa mwezi
Familia yangu ni ya watu watatu yani mama,baba,na mtoto mmoja
Nimebahatika kununua Noah mbili ambazo nazifanyia biashara kila moja inanipatia tsh 40000 kwa siku ni sawa na 80000 kwa noah zote mbili
Kwa mwezi ni sawa na 2400000,kiasi ambacho ni Mara tatu ya basic ya mshahara wangu
Nina leseni ya udereva na wakati mwingine naendesha mwenyewe,
Sasa nataka niache kazi ya kuajiriwa ili nijikite zaidi kwenye biashara maana naona inalipa zaidi
Naombeni ushauri