Nataka kuagiza gari hii, itanigharimu vipi?

Nataka kuagiza gari hii, itanigharimu vipi?

Mzee hy 980 ni fob au cif price? kama ni fob price jumlisha na freight dola 800 +Jaai inspection usd 300 + insurance usd 50. total usd 2080. hy ni bei ya kuleta hl gari mpaka bandarini. then baada ya hapo tayarisha karibia ml 2.5 kwa ajili ya ushuru na charge nyingn pa1 na registration. km unalitaka ninaweza kukusaidia kuimport.
 
Mzee hy 980 ni fob au cif price? kama ni fob price jumlisha na freight dola 800 +Jaai inspection usd 300 + insurance usd 50. total usd 2080. hy ni bei ya kuleta hl gari mpaka bandarini. then baada ya hapo tayarisha karibia ml 2.5 kwa ajili ya ushuru na charge nyingn pa1 na registration. km unalitaka ninaweza kukusaidia kuimport.

Loh, kumbe other charges ni almost thrice the buying price? Tutaweza kuagiza magari kwa mtaji huu?
 
Fisadi J,

Kwa haraka haraka hii kitu inaweza kukucost kitu kama US$2200 (CIF)...Kutoka hapo, TRA watakula kama US$ 1595 so jumla itakuwa US$ 3,750*1350 =TSHS 5,123,250

Hapo itakuwa bado gharama za agent, registration na TRA, Road licence, insurance na gharama za bandarini which can cost you up to Tshs 500,000! So total kitu mpaka kipo barabarani will cost you estimated cost of Tshs 5,623,250!

BWT: Nimemwona Dullymo kajaa tele hapa ni mzoefu zaidi kny hizi issues so anaweza kukupa ushauri zaidi pia unaweza check na captain Kitomai!
 
Kaka Dullymo (au yeyote mwenye uelewewa huu) hebu fafanua hapo pa ushuru na other charges, manake ndipo panapotutisha wengi, si unajua hear say za mitaani. Toa mifano hata mitatu kwa FOB price say USD 1200, 1500 na 2000, na ukiweza tupatie na mifano kwenye CIF price.

Heshima mbele wazee.
 
1. Minimum hii gari ita-cost US$ 2,300 CIF Dar (FOB=980, JAII=250, Freight=1000, Insurance = 50)
2. Exchange rate ya TZS 1,300 ni sawa na madafu TZS 2,990,000
3. Ongeza Import charge 25%, VAT ya 18%, port charges etc (make it 50% 0f the CIF value) inakuja [TZS 2,990,000 times 1.5 = TZS 4,485,000]
4. Kwa kuwa ni over 10 years old kuna charge ya 25% scrap tax
5. Then from (4) above, TZS 2,990,000 times 1.75 = TZS 5,232,500
6. Estimated clearing costs, registration costs etc kama minimum TZS 800,000
7. The total cost minimun is TZS 6,000,000 (unakiendesha mtaani)
 
Do!
Asanteni sana mzee dully na wengineo.

Sasa namnahii kweli tutaweza kuepuka kugombania daladala?

Mimi nikajua kwa kuchagua ka gari cha bei nafuu basi nikizichanga na kufika 3,000,000 hivi pengine ningeaanza ku-enjoy kwenda kazini.

Lakini invyoonekana itabidi nianze kunyanyua vyuma tu. Hiyo hela nitumie kula vyakula vizuri vya kujenga mwili.

Au mnashaurije wazee?
 
1. Minimum hii gari ita-cost US$ 2,300 CIF Dar (FOB=980, JAII=250, Freight=1000, Insurance = 50)
2. Exchange rate ya TZS 1,300 ni sawa na madafu TZS 2,990,000
3. Ongeza Import charge 25%, VAT ya 18%, port charges etc (make it 50% 0f the CIF value) inakuja [TZS 2,990,000 times 1.5 = TZS 4,485,000]
4. Kwa kuwa ni over 10 years old kuna charge ya 25% scrap tax
5. Then from (4) above, TZS 2,990,000 times 1.75 = TZS 5,232,500
6. Estimated clearing costs, registration costs etc kama minimum TZS 800,000
7. The total cost minimun is TZS 6,000,000 (unakiendesha mtaani)

Marekebisho kidogo......ushuru wa uchakavu (scrap tax) ni 20% sio 25% mkubwa! kwingine kote tupo pamoja!
 
Do!
Asanteni sana mzee dully na wengineo.

Sasa namnahii kweli tutaweza kuepuka kugombania daladala?

Mimi nikajua kwa kuchagua ka gari cha bei nafuu basi nikizichanga na kufika 3,000,000 hivi pengine ningeaanza ku-enjoy kwenda kazini.

Lakini invyoonekana itabidi nianze kunyanyua vyuma tu. Hiyo hela nitumie kula vyakula vizuri vya kujenga mwili.

Au mnashaurije wazee?

Sio mbaya,ila pia bongo wapo wanaohitaji kubadilisha ladha ya magari. Unaweza ukapata za mtaani hapa hapa bongo badala ya kuagiza toka nje. Kuna watu kibao humu mtaani wanauza gari zao,onesha nia watakupa gari kwa hela hiyo au ongeza kidogo tu utapata gari bro.
 
Marekebisho kidogo......ushuru wa uchakavu (scrap tax) ni 20% sio 25% mkubwa! kwingine kote tupo pamoja!

Amesahau Excise Duty ya 5% ya CIF+VAT+Import+Scap Tax. In total tax anayotakiwa kulipa ni 85.85% ya CIF. Halafu weka Wharfage ya 1.6% + VAT = 1.89% ya CIF, na Processing Fee (IDF) 1.2% ya CIF + $10. Bado gharama za agent, normally Shs 150,000 to Shs 180,000 plus registration fees.
 
Amesahau Excise Duty ya 5% ya CIF+VAT+Import+Scap Tax. In total tax anayotakiwa kulipa ni 85.85% ya CIF. Halafu weka Wharfage ya 1.6% + VAT = 1.89% ya CIF, na Processing Fee (IDF) 1.2% ya CIF + $10. Bado gharama za agent, normally Shs 150,000 to Shs 180,000 plus registration fees.

Cheif,

Hiyo gari ni CC 650.....Excise duty inaapply kwa magari yenye CC higher than 1,000 mkuu....so kwa haka ka gari no ushuru wa bidhaa hapo!
 
Sio mbaya,ila pia bongo wapo wanaohitaji kubadilisha ladha ya magari. Unaweza ukapata za mtaani hapa hapa bongo badala ya kuagiza toka nje. Kuna watu kibao humu mtaani wanauza gari zao,onesha nia watakupa gari kwa hela hiyo au ongeza kidogo tu utapata gari bro.

Bei za gari zinazouzwa humu si unazionaga mzee? Yaani mtu anataja mil 12 kama vile ni chenji ya shopping ... lol ... sasa si tukitaja vihela vyetu si tutachekwa?

Kwa maeelzo niliyoyasuma huku, ukiona mtu anauza gari chini ya 5M basi ina matatizo. Ndio maana nkasema ngoja nijaribu kuagiza hata cha zamaniiiii cha bei ya chini kabisa. Nako pia naona si kwangu ... huu umasikini ndio ushatuganda wengine ....

Kwa data nilizozisoma hapa ni kwamba ili gari inigharimu 3,000,000 tu inabidi CIF iwe si zaidi ya $1,370. Je, wataalamu wa kukokotoa mnaweza kunihakikishia hili ili niwe ninasaka katika range hiyo tu?

Je, na hiki hapa chini hakinitoi?
http://www.tradecarview.com/used_car/japan car/subaru/legacy+touring+wagon/450751/
1996 Subaru Legacy Touring Wagon
Year / Month 1996/08
Odometer 180,000 km
Displacement 2,000 cc
Steering Right
Transmission Automatic
Fuel Gasoline/Petrol

Kina ma-scratch scratch sema ndio bora kuliko kugombania bana.
 
Kwa kuwa hela zako bado za mawazo tafuta mtaani utapata ya bei hiyo.
 
Bei za gari zinazouzwa humu si unazionaga mzee? Yaani mtu anataja mil 12 kama vile ni chenji ya shopping ... lol ... sasa si tukitaja vihela vyetu si tutachekwa?

Kwa maeelzo niliyoyasuma huku, ukiona mtu anauza gari chini ya 5M basi ina matatizo. Ndio maana nkasema ngoja nijaribu kuagiza hata cha zamaniiiii cha bei ya chini kabisa. Nako pia naona si kwangu ... huu umasikini ndio ushatuganda wengine ....

Kwa data nilizozisoma hapa ni kwamba ili gari inigharimu 3,000,000 tu inabidi CIF iwe si zaidi ya $1,370. Je, wataalamu wa kukokotoa mnaweza kunihakikishia hili ili niwe ninasaka katika range hiyo tu?

Mkuu gari yenye CIF US$ 1,370...mpaka unaiendesha itakugharimu kitu kama TZS 4,000,000....Hapo tayari upo barabarani mkuu!
 
Mkuu nakushauri ununue pikipiki tu ya Bajaj hutakaa kwenye foleni wewe ni kupenya tu na ni gharama nafuu kuiendesha kuliko gari. Kuna watu wana magari wanaendesha week end tu.
 
Mkuu nakushauri ununue pikipiki tu ya Bajaj hutakaa kwenye foleni wewe ni kupenya tu na ni gharama nafuu kuiendesha kuliko gari. Kuna watu wana magari wanaendesha week end tu.

Homeboi unajua bei ya bajaj now?.........for your information.....is not less than 4mil!
 
Mkuu gari yenye CIF US$ 1,370...mpaka unaiendesha itakugharimu kitu kama TZS 4,000,000....Hapo tayari upo barabarani mkuu!

Asante mkuu.

Hivi gharama za baada ya kulitoa bandarini zikoje? yaani registration, leseni, insurance, na vitu vingine tusivyovijua? Vina calculatiwa vipi?
 
Back
Top Bottom