Nataka kuanza Kilimo cha Maharage

Nataka kuanza Kilimo cha Maharage

Pole na hongera sana japo changamoto ilikufelisha ila next time itakuwa bora zaidi kwako
Sio kila changamoto inakufelisha. Sijafikia malengo nilioyoyataka ila si kwamba maharage hayamo.
Hivi kufeli si ni sifuri kabisa?
Nadhani ntapata mbegu ya kama heka 5+ badala ya heka 10 kama milivyokuwa nimelenga.
Nafikiri nimefaulu kwa kiwango cha B natakiwa niende A+ sipo kwenye F.
 
Changamoto ya maharagwe Tanzania inachangiwa na matumizi ya mbegu zile zile sio zilizothibitishwa hivyo kupelekea mavuno kuwa machache.
Yaani wazalishaji mbegu ile Basic seed ni wachache kisha wanaomultiply ndio kabisa,ukitaka mbegu wakala wa mbegu (ASA) muda mwingi ameelemewa na wateja hivyo kutokidhi soko, TARI za Uyole na Maruku nao wanapambana ila nao vilevile.
Ushauri wangu mtu ukihitaji kulima kisasa jiandae mapema walau miezi kadhaa nyuma na labda kwa wenye Nia wawasiliane na vituo vya tafiti vya karibu au ASA,wale wa Arusha na Kilimanjaro wanaweza kwenda Catri,Tengeru na Lyamungo hapo watakuwa salama,Kanda ya Kati Mashariki ni ni Moro aidha Sua au ASA na wale wa Nyanda za juu kusini ni Uyole au ASA Njombe mwisho wale wa kanda ya ziwa ni Maruku mkoani kagera.
Maandalizi mema.
 
kuhusu palizi, je maharage yanapaliliwa ili kuongeza udongo kwenye shina au kwa ajili ya kuua magugu. kama kuweka udoñgo kwenye shina siyo muhimu kwenye ukuaji wa harage, je kuna dawa za kupuliza zinazoweza kutumika kwenye palizi na kuua magugu kwa uhakika (weed selector) . kama dawa zipo naomba kuzifahamu na waliowahi kutumia ufanisi wake ukoje.
 
1.Passion.
2.Knowledge
3.Capital pesa
4. Ardhi yenye rutuba
5.Mbegu.
6.Hali ya hewa inayokubali maharage, ni joto la kadri.
7.Mbegu zinazopendwa kwa ukanda wako, mbeya kipapi na njano, mwasipenjele., njombe njano kijani
8. Msimu wa kupanda ni wa mvua na kiangazi.
9. Msimu wa mvua ni disemba na march.Wengi hupanda march kukwepa mvua haribufu.
10.Msimu wa mvua ni muhimu kupiga madawa ya ukungu.
11.Msimu wa kiangazi hulimwa kwenye mabonde oevu au kando ya vyanzo vya maji ili kumwagilia.
12.Mbolea ni za samadi na kisasa.
14. Szmadi ni junia za debe kumi walau 5, ya kuku ni nzuri zaidi,ya ng'mbe ina otesha nyasi na wadudu wahatibifu, kama sio muisilamu ya nguruwe nayo hutumika na ina nguvu sana.
15.Ya dukani mfuko mmoja miksa dap na can. Vilevile itategemea na ardhi ya huko.
Ardhi nzuri mbolea hazitumiki kabisa(virgin land).
16.Mbegu kwa heka debe 1.5 mpaka 2 inategemea na ukubwa wa maharage.
17.Palizi: Inategemeana na msimu na unakolima, Njombe hawafanyi palizi iwapo utapanda march, Mbeya palizi ni lazima mara moja tu.
18.Inakidiriwa katika hali nzuri utavuna debe 32 kwa heka moja.
Sawa na junia 3 za debe 10.
Bei ya kuuza inategemea mahala ulipo be msimu wa kuuza.
Msimu mzuri wa kiangazi debe hufika mpaka 35000 na wa mavuno ni 23000 au 25elf .
Mwaka jana nimenunua mbegu debe 45000 kipapi ya mbeya.
Songea bei huwa mpaka sh 700 kwa kilo msimu wa kununua.
Changamoyobni nyingi ila kubwa kuwwaweka wati wskudimamie shamba.
Binafsi nimeingia hasara mwaka huu.nilitmia kanuni zote za kupanda ila msimamizi aliunguza maharage kwa sumu iliozidi.
Picha hizi hapa.View attachment 1782264View attachment 1782264



Walifanya uzembe hawakupalilia. Hivyo kuna magugu yaliothiri hapo.
Nililima kwa dhumuni la kupata mbegu kwa ajili ya kulima heka 10 mwakani , basubiri nione ntapata debe ngapi ila 32 ni ngumu japo yaliota vizuri sana na ardhi ina rutuba sana.Nilitumia laki 300000 kwa heka.
Best wish.
mkuu km unategemea kupata mazao ambayo hayana afya inakuwaje utumie tena km mbegu na uwe na matarajio ya kupata mazao mengi kutoka kwenye mbegu hafifu.
 
mkuu km unategemea kupata mazao ambayo hayana afya inakuwaje utumie tena km mbegu na uwe na matarajio ya kupata mazao mengi kutoka kwenye mbegu hafifu.
Wazo zuri, ila kuna mengine mazuri ntayachagua yale mabaya ntakula.
Sio lazima yawe mbegu yenyewe, naweza yauza kwa bei ileile ya soko na kununua mengine kwa hio bado yatatumika kama mbegu kwa replacement.
 
Hello Mr. Tangantika.

Habari za Uzima wako.

Nilikuwa napitia Nondo zako hapa za maharage na nimeshawishika kukuomba mrejesho Tafadhari.

Tangu wakati Ule Mpaka Leo 2024, yamkini utakuwa mwalimu Mzuri kwetu sisi tunaohitaji Kwenda field mwaka huu.

Karibu Tafadhari
 
mkuu km unategemea kupata mazao ambayo hayana afya inakuwaje utumie tena km mbegu na uwe na matarajio ya kupata mazao mengi kutoka kwenye mbegu hafifu.
Ukidumaa wewe ukawa mfupi ukizaa utazaa mtoto mdumavu. Mbegu ni vinasaba au physical apearance..
Mninu huwa ni nyingi unaweza pata mbegu ukabadilishana na mbegu nyingine ukauza ukanunua nyingine, ukachagua mlemle the best.
Kwenye kilimo kuna propaganda nyingi sana.
Makampuni yanayouza mbegu za hybrid hayawezi kukwambia kuwa ukirudia mbegu itafanya vizuri bali ununue nyingine ili wauze.
Ukweli ni kwamba ukiwa makini unaweza nunua mbegu mara 1 na ukaendelea kuitumia kwa mbinu mbali mbali.
 
Back
Top Bottom