Nataka kufanya biashara ya kuuza viatu vya mtumba

Nataka kufanya biashara ya kuuza viatu vya mtumba

PAPAA JIWE

JF-Expert Member
Joined
May 12, 2014
Posts
863
Reaction score
149
Habari wadau?

Naomba kupata ushauri na uzoefu kutoka kwenu.

Ningependa kujua jinsi ya kuanzisha BIASHARA ya viatu vya mtumba (vya kike na vya kiume), mahala napoweza kupata viatu hivyo (kwa bei ya jumla), gharama ya kununulia na kuuzia, na faida pia.

Pia ningependa kujua vibali navyotakiwa kuwa navyo ili niendeshe biashara hii kwa Uhalali.

Mwisho kama kuna mbinu za kibiashara mnijuze.

Nawashukuru kwa muda wenu na natarajia msaada toka kwenu.
 
Kanunue Viatu Weka.

Kalipie Leseni Manispaa. TRA Wakikusumbua Nunua Kitambulisho Cha Kibwengo Magu

Hakuna Jipya.
 
Kanunue Viatu Weka.

Kalipie Leseni Manispaa. TRA Wakikusumbua Nunua Kitambulisho Cha Kibwengo Magu

Hakuna Jipya.
Hivi kwa nini mnapenda kumtamka Rais wa nchi kwa lugha mbaya mbaya?

JAH Rastafari Morning Africa.Trust JAH respect nature
 
Nilikuwa Mwanza wiki iliyopita nimenunua viatu vya mtumba vya kuvalia suti bei rahisi sana. Wanasema wanatoa mitumba Uganda. Jaribu kuangalia wale machinga wanaopanga viatu Nyerer Road pale Mwanza wanaweza kukupa mwanga
 
Mkaruka shukrani sana mkuu kwa maelezo mazuri. Pakuvinunua ndiyo sijapata maelekezo. Kwani robota linauzwaje? Na ni wapi pa kuvinunulia.
 
Nilikuwa Mwanza wiki iliyopita nimenunua viatu vya mtumba vya kuvalia suti bei rahisi sana. Wanasema wanatoa mitumba Uganda. Jaribu kuangalia wale machinga wanaopanga viatu Nyerer Road pale Mwanza wanaweza kukupa mwanga

Bei gani Boss share na wanajukwaa wengine
Maana wanasema ukiona umeula sana jua umeliwa sana
Size yake haijaanza na 255/265/270?
Kama kina hizo Namba kwa chini jua umeumia pakubwa sana


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bei gani Boss share na wanajukwaa wengine
Maana wanasema ukiona umeula sana jua umeliwa sana
Size yake haijaanza na 255/265/270?
Kama kina hizo Namba kwa chini jua umeumia pakubwa sana


Sent using Jamii Forums mobile app
Mie wala saingalii hizo namba mie nachojali kuwa kiatu ni pure leather na kinanitosha na kunipendeza hata nchi kilipotengenezwa mie uwa sizingatii
 
Hata anayekuwa wa kwanza darasani hapati masomo yote 100, Yawezekana ukajua vitu vingi lakini usijue kila kitu.
Yawezekana ukaishi BONGO miaka 50 lakini usifike katika kila kitongoji.
Yawezekana umefanya biashara nyingi sana lakini si kweli kwamba zote umezimaliza.
Namuelewa sana mtu anayetumia akili yake, taaluma yake, na busara zake pia katika kuwavusha watu wengine na wala si kuwadharau na kuwakejeli.

NOTE: Hata genius na matajiri nao huhitaji msaada wa mawazo kutoka hata kwa watu wasio wasomi wakati fulani.
 
Nina uzoefu wa kazi zingine, Lakini katika uuzaji wa viatu mimi ni mshamba kwa maana bado mimi mgeni katika biashara hiyo.
Kuuliza na kuomba ushauri ni hatua nzuri katika kutimiza malengo uliyojiwekea.
Nilihitaji kujua mahali yanakoagizwa marobota ya viatu, Maana wengine husema nafuu iko Uganda, wengine Bandari Salama, Na wengine Zanzibar.
Biashara usiyo na uzoefu nayo ama haujawahi kuifanya sidhani kama ni vema kuianza kwa kuikurupukia.
Sijui kitu kwenye uuzaji na uagizaji wa marobota ya viatu, Lakini ukinikuta na mimi kwenye anga zangu za software utasema kweli jamaa ni mtata.

NOTE: Utafanya biashara nyingi sana lakini moja utaipenda kuliko zote. Na hata uzoefu wake utakuwa mkubwa sana kuliko uzoefu wa biashara nyingine ulizowahi kuzifanya ama bado unazifanya.
 
Back
Top Bottom