Nataka kufunga ndoa bila sherehe

Kuna jamaa yangu kafunga juzi tulienda kanisani watu kama 10 mpaka padri alishangaa maana hapakua na shangwe lolote lkn padri alisema amependa iyo staili na kwenye mahubiri yake alisema ndoa ni watu wawili na wazamini wao mengine ni mbwembwe lkn kibaya yule jamaa yangu alichangisha watu
 
Kama ukiweza unganisha honeymoon moja kwa moja ukitoka church..
 
Mkuu,
Tena unazo baraka tele. Maandiko hayasemi afanyae sherehe apata mke na kibali kwa Mungu/ Bwana.

Bali apataye mke apata kibali kwa Bwana.


Sherehe ni porojo tu za wanadamu.


Kila la Heri uwe na ndoa yenye furaha, amani na baraka.
 
Kisheria ndoa lazima iwe na sherehe.Ingawa sheria ya ndoa haijasema sherehe iwe vipi.Kwa hiyo fanyeni sherehe hata ya watu kumi tu haina tatizo.


Hakuna sheria ya ivo Tanzania na hatutawahi kuitunga. Sheria ya ndoa inatambua ndoa kufungwa ukiwa na mashaidi na mfungishaji ambapo wawili mtakula kiapo bila au kwa kuvaa Pete pia.

Ila ayo ya sherehe yanatajwa kama mazingira ya kufungia ndoa. Yaweza kuwa ofisini, sehemu ya wazi, ukumbini nk nk

Tueleze ni kifungu gani cha sheria ya ndoa kinachoweka ulazima wa sherehe?


Nampongeza mleta mada kwa kuwa anaonesha sasa watu waneanza kujitambua. Ndoa yako kwa nn upoteze mali kuwafurahisha watu?
 
Naona madharau kabisa, tena zinadumu kuliko za sherehe kwenye boat na kumbi mbalimbali.
Ila ya kwangu lazima niwachezeshe kwaito kama navozicheza mimi now


Haaaa haaaa o là là, Ma Cheri ce ne pas bonne 'idée!!
 
Wana, JF, ndoa ni mume na mke kuwa pamoja sherehe ni mbwembwe uchwara.

Pana, Bibi zetu zamani wanasema walikuwa wanatoroshwa (nimeisikia hili neno kutoroshwa sana kanda ya ziwa) na ndoa zao zilidumu, na zikawa na furaha na amani.

Mleta Uzi, wewe funga ndoa cha muhimu ishi kwa amani, upendo na furaha na mkeo. Utaona baraka sana maishani mwenu.


Pia, nimetoa "likes kwa comments almost zote" kuonesha kuwa NDOA siyo sherehe Bali ni makubliano ya mtu mume na mtu mke kukubaliana kuishi pamoja kama mke na mume.

Mimi siyo shekhe, Mchungaji au padri, ila viongozi wote hao hawasemi habari za sherehe bali wanasema (mume na mke ndiyo ndoa).

Kila la Heri kwa wote wanaotaka kuwa na wenzi wa maisha (mtu mwanamume na mtu mwanamke) kwa ndoa ya aina hii ya bila sherehe.

Japo, anayependa sherehe na jamii yake inataka kufanya sherehe poa tu ila sherehe isiwe kikwazo cha vijana (wa kiume na kike) kuoana.

[HASHTAG]#emmyta[/HASHTAG]
 
Hakuna tatizo....tena hapo utakuwa umeepusha matatizo kibao!

Mimi nategemea kufanya hivyo, sherehe sizipendi pia kusumbua watu siwezi...hivyo hata nikisema nichangishe pengine sitaweza kukusanya hata mia, hata kama ni sherehe nitafanya ndogo tu ambayo naweza kuimudu mwenyewe tena nitaweka hema home tu inatosha...
 
Ahsante sana kwa mawazo na ushauri mzuri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…