Nataka kufungua duka la mchele, naomba ushauri

Nataka kufungua duka la mchele, naomba ushauri

Mafanikio mema. Ukisumbuliwa kwa namna yeyote ile report mamlaka husika. Wakikuzungusha wasiliana nasi kupitia Meza ya Rais | The President Table tutafikisha moja kwa moja kwa Rais
 
Biashara hiyo ni pasua kichwa niko now kweny biashara na nina mtaji wa m10 na bado unaniangaisha faida siion mpka leo.. mimi kama mimi sikushaurii kufungua store nibora ufungue duka la rejareja maana hapo huwo mchele kama ndo unaanza biashra kwa kuangalia unajua unaenda uuza bei gani unaweza jikadiria unaenda kuuza elfu moja miasita una fika sokoniii ukakataa bei hiyoo unataka 1400 uuze hapo ndo kasheshe inapoanza afu pia imagine huko unakochukua mzigo nimbaliii sana mzgo utatumia siku nying njian utakuwa unauza hakuna kila siku kama utapata wateja wa kuchukua wote kwa pamoja
 
Tani mbili sio mzigo wa kufungua kitu kinaitwa "store ya mchele" tena hapo unataka uutoe Katavi. Hiyo ni kianzio cha kufungua duka la mchele, sio store kibongobongo.

Ukisema store kwa lugha ya mtaani ni kwamba unauza jumla, sasa jumla gani ya tani mbili. Direct cost za mchele huwa ziko juu sana. Faida ya mchele huwa haizidi 200TSH kwa kilo hapo ni maximum, ukipata 50TSH/kg kawaida ukipata 100TSH/kg uko vizuri.

Chukua wastani wa 100TSH/kg zidisha na tani 2 hapo faida ya wastani baada ya kila kitu ni 200,000.
Hiyo ni profit baada ya kutoa ushuru wa kusafirisha, gharama za kusafirisha, kupakia na kushusha, kupaka mafuta, kuuchekecha kwenye mashine (grading), kulipia viroba na packaging, kusafirisha kutoka ambapo gari litaushusha mpaka store yako (probably utaungana na wenzio wanaoshusha soko la Tandika).

Anyway nisiandike sana. Hiyo ni biashara kichaa kwa mpango ulionao na uwezo wako. Najua watakuja motivation speakers wa JF waseme nina wivu na negativity ila nasisitiza kwa kubold na kupigia mstari. Hiyo ni biashara kichaa.

Badala yake bora uanzishe duka (sio store) la nafaka mbalimbali za rejareja. Naona una mtaji mdogo mkuu
Fuata huuu ushauru📌
 
Back
Top Bottom