Nataka kujua ni jinsi gani ya kutengeneza pilipili kama zile wanazotumia wauza chipsi

Jamani nataka kujua ni jinsi gan ya kutengeneza pilipili kama zile wanazotumia wauza chipsi wa Dar es Salaam na zinakaa kwa muda gani, nimeuliza sana ila sijapata jibu naamini leo nitapata majibu humu JF.

Karibuni kwa maujuzi.
Chukua embe mbichi kabisaa zile kali kiasi utakazo.

Kisha tafuta pili pili nyingi.

Kisha weka pamoja embe na pilipili,embe zimenye(toa maganda na kokwa)kisha ndo uweke kwenye sufuria na pilipili.

Tia maji humo kwa sufuria,kisha acha ichemkee weee,ichemkee mpaka iww rojo rojo,kisha iblend kabisa umemaliza
 
Pilipili ipi inafaa!? Pilipili mbuzi au zile kali na unakadiliaje hizo inputs, ratio yake? Ili zitoe kitu kizuri, let say nahitaji lita moja ya pilipili,nafanyaje!
 
Ninavyofanya mimi:
Chukua pilipili kali(toa vichwa/vijiti) zioshe
Tafuta mbilimbi au embe ichi--lichonge na ulikatakata
Chumvi vijiko viwili vikubwa
Vinegar--kikombe kimoja.
Tangawizi--iliomenywa
Vitunguu saumu
Maji ya limao/ndimu
Hakikisha pilipili ni nyingi kuliko viungo.
Weka kwenye blender na usage(ukichemsha itadumu kwa muda mrefu zaidi--mwaka mmoja+,usipochemsha roughly miezi mitatu).
Ukitaka idumu--chemsha chupa(chupa ya jam au yenye kifuniko cha chuma ni bora zaidi) ya kuhifadhia na maji moto ili kuitakasa.
Kisha ukishamimina,geuza chupa juu chini kwa muda ya lisaa limoja ili hewa extra itoke.
Process hii unaweza kutumia pia kwenye kusindika nyanya zikishuka bei
Kila la kheri!
 

Mkuu pilipili yako hii huwa ni rangi gani ukishaitengeneza?
 
ndimu nzima au
 
Kw kuongezea ukitaka isiharibe haraka usitumie maji mengi weka ndimu ya maji nyingi au malimao mengi ukikosa tumia hata vinegar hapo itakaa Sana tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…