Muache tu huyo labda ni wale Wa 'tuma kwa namba hii'
Kaka mawazo yangu ni kuwa
Biashara yoyote inatokana na experience hata kwenye kazi za kuajiri nikitu kinacho angaliwa
Biashara pia ina changamoto nyingi, sio lazima uweke 5M yote katika business moja na ndo maana tunasema au kushauri watu wafanye diversification of capital( yaani usiweke mayai yote katika kapu moja tawanya mayai au mtaji wako)
Mfano biashara ikienda mlama inamaana capital yako ya 5M iko mahala pabaya.
Usifanye biashara kisa Juma anafanya na anapata faida
Haujui nyuma ya pazia anachokifanya, biashara zinamambo mengi ukiacha kitu kama Location kinacho pelekea biashara kufanikiwa, kuna Customer care, know how ya business , experience ya biashara unayotaka fungua unayo, Muda wa usimamizi unao?, Gharama za uendeshaji unazijua yaani Operating Cost usije ukawa umeangalia tu kwa macho ukajiridhisha inabidi ufanye reserch mpk ya gharama na wateja kujua kwa wastani wanakuwepo wangapi katika location yako, biashara nyingine watu wanaloga na kufanya makafala so nakuomba ufanye biashara unayoipenda toka moyoni usifanye kwakua unahitaji kufanya ili mkono uende kinywani au ili usogeze maisha.
Sijajua uko Mkoa gani ila kama unataka biashara inayotoka kwa haraka naweza sema ni biashara ya vitu vya electronic accessories kama Simu ( najua na kufahamu unaelewa watumiaji wa simu ni wengi), lakini pia kuna biashara nimeiona watu wanafanya ni ya Taa za Solar ambazo wanatumia watu wa magengeni mbadala wa vibatali na chemli yaani Taa izo zinachagiwa kwa Jua au Umeme jioni wanakuja kodi kwako kwakuwa hawawezi vuta umeme mpk pembezoni mwa barabara na kwa siku wanalipia elfu 1 tu ambapo wanatumia saa moja mpka saa 5 usiku wanarejesha so unaweza ona ukipata watu 20 umeingiza tsh 20,000 per day na nibiashara ya muda mrefu zaidi ila pia biashara nyingine niya Chakula ( watu wanafanya kazi ili wapate kula na kulala mahala pazuri, biashara ya Money transaction
Ila biashara zote izo zinafanywa na watu so ili uweze kutake over ni lazima uende extra na kuadd value katika biashara yako ndipo utakapo weza toboa usipende copy and paste biashara be Unique
Nihayotu ndugu yangu