Nataka kununua gari, ipi itafaa kati ya Kluger, Qashqai, Dualis ama Harrier Old Model

Nataka kununua gari, ipi itafaa kati ya Kluger, Qashqai, Dualis ama Harrier Old Model

Mtoa mada tatizo lako umependa magari zaidi ya matano sidhani kama utapata ushauri wa kueleweka ni Bora ungetuwekea at least mawili hapo tungekupa sifa za gari husika.
 
Mtoa mada TATIZO lako umependa magari zaidi ya matano sidhani kama utapata ushauri wa kueleweka ni Bora ungetuwekea at least mawili hapo tungekupa sifa za gari husika

Kati hao mkuu lipi unanishauri best kwako mbona watu wametoa ushauri mkuu we ni shauri kati ya hayo ndio nayapenda
 
IMG_1913.jpg

Dualis
 
Nataka gari ambayo ni rahisi kutengeneza pia vifaa vyake visiwe vya gharama kubwa.

Pia nataka gari ambayo matumizi ya mafuta yawe ya wastani per km pia gari inayo stahimili barabara mbaya za vijijini yaani gari yenye 4WD...

Gari hapo ni Nissan qshaqai tu mengine hamna kitu
 
Kluger na Harrier za mwanzo ni basically gari moja. Tofauti ni mwonekano tu na Harrier ina option ya engine ya 2.1l. So kama unachagua hapo wala usiumize kichwa. Angalia unalopenda mwonekano.

Kwa upande wa Nissans, kama ndio gari lako la kwanza, acha kwanza. Ila kama ni mzoefu unaweza kujaribu. Maana mambo ya kuagiza spare yatakuboa. Na kama mdau mmpja alivyokwambia, Dualis na Qashqai ya chini ya 2014 ni gari moja, majina tu ndio tofauti.

Kwa AWD ya Forester (2008 kuendelea) kwa offroad, hakuna anayetia mguu kati ya hao jamaa wengine. Japo Dualis hayuko mbali saana.
 
Kluger na Harrier za mwanzo ni basically gari moja. Tofauti ni mwonekano tu na Harrier ina option ya engine ya 2.1l. So kama unachagua hapo wala usiumize kichwa. Angalia unalopenda mwonekano...

Sawa mzee kwahiyo unashauri harrier na klugger
 
Back
Top Bottom