Mimi nataka vitz ya bei rahisi sana used lakin iwe inafanya kazi kwa 4.2Mukiitaji ya mkononi usisite kunitafuta.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mimi nataka vitz ya bei rahisi sana used lakin iwe inafanya kazi kwa 4.2Mukiitaji ya mkononi usisite kunitafuta.
Hii hali ipo ila ujuzi hutafutwa jifunze mambo madogo madogo kupitia internet utapata ujuzi tuu kidogo kidogoWadau,
Naomba mwenye kujua kuhusu gari imara na inayotumia mafuta kidogo especially used from Japan, pia ni vitu gani vya msingi napaswa kujua kabla sijamiliki gari?
Ahsanteni
Ahsante sana Mkuu kwa ushauri mzuriHii hali ipo ila ujuzi hutafutwa jifunze mambo madogo madogo kupitia internet utapata ujuzi tuu kidogo kidogo
1.oil change interval
Naviginevyo ...hakuna aliezaliwa anajua isipokuwa elimu ya kula tu ndio tunazaliwa nayo.
Unapofikiria kununua gari ni sawa tu na unapofikiria kujenga nyumba kwa mfano. Lazima uangalie mambo ya msingi kama vile: ukubwa wa familia yako (hii inaweza husu gari na nyumba) maana yake ni kuwa kama una familia kubwa utahitaji gari lenye nafasi kubwa ya watu kuketi, aina ya maisha unayoishi (life style) (hii inaweza husu gari na nyumba) maana yake ni kuwa kama mimi hupendelea kusafiri kwenda kijijini kila mwisho wa mwaka lazima niwe na gari lenye kibeba mizigo (carrier) ili nibebe mkaa au ndizi na nyanya nikiwa njiani n.k. Safari utakazofanya (hii inahusu gari) maana yake kama unaenda njia zenye lami zaidi (on road) au kwenye njia mbaya (off road), umbo la mwili wako (inahusu gari) hii ina maana kama wewe ni 'kibonge' au mrefu wa futi sita hutaweza kutosha kwenye Vitz au Passo. Hivyo huwezi kununua gari hizo hata kama ulaji wa mafuta ni mdogo mno.Wadau,
Naomba mwenye kujua kuhusu gari imara na inayotumia mafuta kidogo especially used from Japan, pia ni vitu gani vya msingi napaswa kujua kabla sijamiliki gari?
Ahsanteni
Ubarikiwe ndg kwa ushauri mzuri sanaUnapofikiria kununua gari ni sawa tu na unapofikiria kujenga nyumba kwa mfano. Lazima uangalie mambo ya msingi kama vile: ukubwa wa familia yako (hii inaweza husu gari na nyumba) maana yake ni kuwa kama una familia kubwa utahitaji gari lenye nafasi kubwa ya watu kuketi, aina ya maisha unayoishi (life style) (hii inaweza husu gari na nyumba) maana yake ni kuwa kama mimi hupendelea kusafiri kwenda kijijini kila mwisho wa mwaka lazima niwe na gari lenye kibeba mizigo (carrier) ili nibebe mkaa au ndizi na nyanya nikiwa njiani n.k. Safari utakazofanya (hii inahusu gari) maana yake kama unaenda njia zenye lami zaidi (on road) au kwenye njia mbaya (off road), umbo la mwili wako (inahusu gari) hii ina maana kama wewe ni 'kibonge' au mrefu wa futi sita hutaweza kutosha kwenye Vitz au Passo. Hivyo huwezi kununua gari hizo hata kama ulaji wa mafuta ni mdogo mno.
Baada ya kutathmini haya ndio inakuja hatua ya gharama sasa kama vile ulaji mafuta, matunzo ya mara kwa mara (service), aina ya bima kama ni kubwa au ndogo n.k. Na mwisho kabisa bei ya kununulia gari lenyewe sasa.
Kwa kuwa inaonekana huna uzoefu wa aina za magari, suala la 'status' tuliache kwanza. Jitathmini kwa vigezo hivyo vichache vya hapo juu kwanza kisha utapata picha ya nini kitakufaa na ndipo utaweza kuingia sokoni kuangalia bidhaa zilizopo na usisite kuuliza kwa wale wenye uzoefu wa kuyatumia (practical experience) magari pindi ukikutana na changamoto katika kufanya maamuzi ya kununua sasa. Nasema uombe msaada kwa watumiaji wazoefu na sio tu madereva wa kukata kona kwa sababu hapa mjini kuna watu wanaendesha gari lenye Four Wheel Drive (4WD) lakini hawajawahi na hawajui kutumia hiyo kitu. Na kuna mwenye gari lenye winchi ya umeme (Electric Winch) kwenye ngao ya mbele kwa ajili ya kusaidia gari kujivuta lenyewe ili kujinasua kwenye kukwama lakini hajui hata jinsi ya kuitumia. Naamini utafanikiwa kupata gari litakalokufaa.
Kwa hiyo bajeti - tafuta gari za ingine size 1.3L, mfano IST etl, Kwa kigezo cha ulaji wa mafuta kidogo
Kwa hiyo bajeti - haitoshi kuagiza gari toka Japan (CIF + KODI), bali utanunua hapa hapa nchini.
Ni vyema ukaanza na hii thread utapata mwanga zaidi:
Dah jamaa fala wewe.. kwa hiyo site mirror, hazard, indicator etc hazimuhusu[emoji1] [emoji1]Unataka ushauri gani? Wewe kalia siti angalia mbele tu... Kanyaga mafuta na break basi,,, hakuna jingine...
Ahsante kwa ushauri mkuu....Je hiyo ya kuagiza direct inakwenda mpaka mil ngap ?
Ghalama inajulikana iwapo tu utasema:
- ni aina gani ya gari unahitaji?
- Iwe ya mwaka gani?
- iwe na cc ngapi?
Kumbuka kwa sasa kodi ya magari kidogo imeongezeka tofauti na mwaka jana.
Tuchukulie kwa mfano Toyota IST inatakiwa uandae sio chini ya 12m, Ambapo makadirio ya kodi ni kama 5m. : Used Motor Vehicle Valuation System - Used Motor Vehicle Valuation System
View attachment 687519
Kweli kabisamungu akubariki nami nilikuwa sijui umenipa mwanga naomba wachangiaji wa jamii f kama huna la kumsaidia mtu aliuliza bora unyamaze na usomee maoni ya wachangiaji wenye maadili mema sio kujibu ivyo hatakusaidia wewe ulieandika utumbo
mpaka unaiweka mkononi ilichukua bei gani?Mazda Demio unapata, Mimi nimenunua, nilishauriwa pale ofisi za Befoward posta, ni gari nzuri na ni ngumu sijajuta hats kidogo. Engine size in 1340 cc. Nimesafiri nayo kwenda mikoani.
Suzuki Jimny ni gari nzuri. Injini yake ni ndogo (cc chini ya 1500) na zina 4 Wheel na ziko juu (good ground clearance). Pia zina chassis fupi (short wheel base) na hivyo kupelekea kuwa na nafasi ndogo sana ndani. Mapungufu ya gari hizi ni kuruka ruka sana (bumpy) kwa kuwa na chassis fupi na ni rahisi mno kuanguka hasa kwenye kona kali kwa kuwa zimeinuka na ni compact. Kuna idara moja ya serikali ilizinunua hizi gari kwa kila wilaya nchi nzima. Vijana wakaajiriwa na kupatiwa magari hayo. Wengi wa vijana walikuwa na leseni mpya bila uzoefu wa kuhimili magari hasa kwa safari ndefu. Wengi walizidondosha!mi nakushauri tafuta suzuki jimny autajuta ni nzuri kwan inaendana na mazingira yote ya nnchi yetu na kwa hii bei yako unaweza kupata integemeana na soko la hiyo siku huko japan