Nataka kuongeza bidhaa dukani

Nataka kuongeza bidhaa dukani

BradFord93

JF-Expert Member
Joined
Oct 11, 2017
Posts
917
Reaction score
2,217
N duka ambalo kwakweli nimeliinua tangu lilipokuwa chini mpk sasa hali inaridhsha

Sasa nnataka kuongeza bidhaa ambazo kwakweli sijawahi kuuza....bidhaa hizo ni Maziwa ya Tanga fresh na mtindi.....pia na mikate

Shida ninapata kwenye upatikanaji wa hizo bidhaa....nasikia wanapitisha kwa magari

Je ni utaratibu gani unatakiwa kufanyika ili mimi kuzipata bidhaa hizo??

Na je zinahitaji utunzaji wa aina gan ili zikae zikiwa in good condition katika uuuzaji??


Mawazo yanahitajika
 
Nitakusaidia tu kidogo kuhusu uhifadhi wa bidhaa hizo maana ni tofauti

Mikate inategemea maana shelf life huwa kuanzia siku 6 mpaka 10 inategemea na mapishi yake
Na maziwa kama ni fresh yanaweza kukaa kwenye fridge kuanzia siku 5 mpaka 7
Unapopata msambazaji wako hakikisha inakuwa na muda wa kutosha kwa matumizi

Usipokee maziwa au mikate iliyobakiza siku chache sana kama huna uhakika wa kuuza yote

Kuhusu supplier sijui kwa kweli ila unaweza ukaauliza wanaouza wanaweza kukusaidia kama wana ukarimu
 
Back
Top Bottom