Nataka kwenda kula bata mkoani nikatalii mkoa gani? Kwetu dar

Arusha- Tarangire, Ngorongoro crater halafu unaweza kuhamia Serengeti N P ukitokea Ngorongoro hutajuta
Naongezea hapo Manyara...Olduvai Gorge anaingia Serengeti anatokezea geti la Fort Ikoma anaingia Nata ....Nyamswa ....Butiama kwa Baba wa Taifa (Makumbusho) kisha anaingia Musoma anashangaa shangaa siku moja anamalizia Mwanza. Kama ni mwezi huu wa August anakuwa amefanya na booking kabisa ya kukata utepe ya Dreamliner mpya anaruka zake back to Dar
 
Aisee safi umenikumbusha Butiama kwa Baba wa Taifa. Mwanza pazuri sana
 
Yani avatar yako imenichefua sana, so wew pia ni me? Kama ni me hakika utapata tabu sana, ila kama ni ke very sorry.
 
Mkoa wa starehe na tulivu ni Tanga. Anzia Magoroto camp pale halafu panda Lushoto gwanta view then malizia Manza Bay.
 
Budget yako shingapi sio unabuku mbili alafu nikushauri uende singita
 
Aiseee aaikudanganye mtu,karibu sana Iringa pia utafika mpaka Mbeya!. Utakuwa na utalii na mapumziko mazuri kabisa. Nitakuorodheshea vivutio zaid zaid ya 20 ukanda huu ambavyo havitangazwi lkn ukifika na kujionea kamwe hutojutia muda wako na pesa

Mkuu nyakati hizi ni kipindi cha baridi katika ukanda huo,kama jamaa hajazoea baridi atapata tabu sana.ila akisubilia mwezi wa tisa hadi wa kumi ukanda huo kuna faaa.
 
Njoo Arusha,nitakupokea mimi
 
Mkuu nyakati hizi ni kipindi cha baridi katika ukanda huo,kama jamaa hajazoea baridi atapata tabu sana.ila akisubilia mwezi wa tisa hadi wa kumi ukanda huo kuna faaa.
Barid limeisha kabisa mkuu!,tunajifunika shuka tu kwa sasa. Mi nipo huku na deal zangu ni iringa na Mbeya so namhakikishia through experience hakuna barid kwa sasa
 
Karibu msitu wa Mabwepanande utaenjoy hadi raha aisee tena kivutio bora zaidi ni pale makumbusho ya Dr Ulimboka
 
Mkoa wa starehe na tulivu ni Tanga. Anzia Magoroto camp pale halafu panda Lushoto gwanta view then malizia Manza Bay.
Hivi Manza Bay ipo wapi mkuu naona kwa watu wa Tanga ni sehemu maarufu kweli
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…