Nataka nijue faida za kuwa mjumbe wa NEC

Nataka nijue faida za kuwa mjumbe wa NEC

Fidel80

JF-Expert Member
Joined
May 3, 2008
Posts
21,947
Reaction score
4,470
Wakuu tumeshuhudia watu wakipigana vikumbo kugombea nafasi kadhaa ndani ya CCM na wengine kuhonga vitumbua ili tu wapate kuchaguliwa wajumbe wa mkutano mkuu au NEC mimi nataka nijue kuwa mjumbe wa NEC CCM kuna faida/maslahi gani mpaka ifike hatua watu wanatishana na bastola? Je kuna marupu rupu na posho ma/kubwa kwenye uwakilishi wa ujumbe wa NEC? Ni nini haswa faida kuwa mjumbe wa NEC mpaka mtu anadiriki kutumia mamilioni ya shillingi ili awe tu mjumbe je anapata faida gani? Akina zomba, Ritz, Rejao, Kibunango na wengineo naombeni nifahamu faida zake.
 
Faida moja wapo ya kuwa mjumbe wa Magamba-NEC ni kula Posho, kupewa ukuu wa mkoa au wilaya.
 
Kuwa ndani ya NEC ni tiketi tosha ya kukutana na wakubwa,
kuukwaa ukurugenzi katika taasisi za serikali, kufanya biashara
yoyote unayoitamani, kukwepa kodi nk...
 
Faida moja wapo ya kuwa mjumbe wa Magamba-NEC ni kula Posho, kupewa ukuu wa mkoa au wilaya.
Haiwezi kuwa hiyokwa sababu wanaopigana vikumbo hivyo wengine ni mafisadi wakubwa wana hela nyingi na hawana shida na viposho uchwara wala hivyo vyeo vya DC au RC.
Ipo sababu nyingine kubwa ya uficho ambayo tuitafute tuijue maana watu wazima na vyeo pamoja na fedha walizonazo kama wana tumia Bastola kutaka kutoana roho si jambo la mchezo.
Subirini Malima akirudi Mkuranga naye akawatolee ile SMG yake ndio mtakapowajua Al shabab (CCM) ni chama cha aina gani na nini umuhimu wa kuwa mjumbe wa NEC
 
Ngoja tusubiri majibu toka kwa mh kigwangalla
 
Last edited by a moderator:
Faida zingine ni kwamba unakuwa juu ya Sheria, Unaweza Endesha gari bila hata kuwa bima na usifanywe chochote, Utafanya kila Aina ya Ufisadi ikiwemo kuuza Wanyama Nje ya Nchi
 
NEC ni chombo kikubwa sana ktk chama. Ni rahisi kupata rushwa na ahadi kemkem wakati wa mchakato wa kutafuta mgombea urais.
 
Unakuwa unauza sura kisha dili zako chafu zinafichwa we unatengeneza mapene.
 
u become among the 5% of this country who share 75% of the national resources.
NOTE:One day God will punish u all for this.
 
Njia moja kubwa ya kuficha ufisadi wako ni kuwa mjumbe wa NEC ya ccm, huoni mafisadi wote wanapigana vukumbo kuingia kwenye kundi hilo; kuanzia Kimbisa, Chenge,Lowassa, Membe, Sitta, Karamagi mpaka Lukuvi wote wanataka kuingia humo!!
 
Mjumbe wa nec manake ni mujumbe wa kikao cha juu kabisa cha maamuzi cha chama kazi yake kubwa ni kutoa dira na mwelekeo wa chama iwe ccm au tlp au chadema.tusipindishe ukweli na maana za vitu
 
Mana ya nec kama ingekuwa kampuni ni board of directors.nec ya ccm ndio inayoandaa ilani ya uchaguzi ya chama
 
Faida zingine ni kwamba unakuwa juu ya Sheria, Unaweza Endesha gari bila hata kuwa bima na usifanywe chochote, Utafanya kila Aina ya Ufisadi ikiwemo kuuza Wanyama Nje ya Nchi

ningekuwa na akili ya kipuuzi kama ya kwako ningeamua kwenda mirembe
 
Kuwa ndani ya NEC ni tiketi tosha ya kukutana na wakubwa,
kuukwaa ukurugenzi katika taasisi za serikali, kufanya biashara
yoyote unayoitamani, kukwepa kodi nk...

kigezo cha kwanza huwa ni uzalendo,uaminifu na uchapakazi.hayo uliyoandika wewe ni uzushi mtupu
 
kigezo cha kwanza huwa ni uzalendo,uaminifu na uchapakazi.hayo uliyoandika wewe ni uzushi mtupu
Ndio uzalendo kama wa chenge kuficha vijisenti vya rada nje, lowasa na richimond, hata kuuza wanyama pori hai nje na kuingia mikataba ya kimangungo tena kwa ari, nguvu na kasi zaidi. bila ya sifa hizo ujumbe wa nec utaishia kuusikia tu.
 
kigezo cha kwanza huwa ni uzalendo,uaminifu na uchapakazi.hayo uliyoandika wewe ni uzushi mtupu
Vigezo hivyo vilitumika enzi za Nyerere nec ya sasa wanaangalia uwezo wa pesa wa mtu nitajie mkulima/mfanyakazi gani ni kapuku ndani ya nec.
 
Back
Top Bottom