Matamanio yangu (kuwa fisadi)
Natamani, natamani, na mimi niwe fisadi
Natamani, natamani, na mimi niwe zaidi
Natamani, natamani, na mimi niwe kaidi
Fisadi ama kaidi, nitawaliza wandugu!
Kwa kuwaliza wabongo, nataka niwe fisadi
Nije wapiga madongo, yaliyo ya kigaidi!
Hata mkila udongo, majani au zaidi!
Fisadi au kaidi, nitawaliza wabongo!
Mwenzenu natamania, ninaongeza juhudi
Nitauza Tanzania, halafu niwe hasidi!
Dharau ya kuringia , tafanya kwa makusudi
Fisadi ama kaidi, nitawaliza wabongo!
Najua hilo ni dili, yaani kuwa fisadi
Hata mkini jadili, mwenzenu nitawanadi
Hesabu za kikatili, napiga niwe fisadi
Fisadi ama kaidi, nitawaliza Wabongo!
Na wala sina huruma, ni sifa yangu fisadi
Halafu tena nasema, nauza hata vya jadi
Nasema mtanikoma, msichezee kaidi!
Fisadi ama kaidi, nitawaliza Wabongo!
Na kila chenye thamani, mwenzenu nita kinadi
Sitoufanya utani, hata mpate shahidi
Fidia ya ki mjini, nitawatoza na kodi
Fisadi ama kaidi ,nitawaliza wabongo!
Mseme hili na lile, na wala sito jirudi
Mpige hata kelele, mfie kwenye migodi
Niuze hata vya kale, halafu mje vikodi
Fisadi ama kaidi, nitawaliza wabongo!
Kaditama ya tamati, kikomo changu fisadi!
Misitu pia na miti, kati ya nitavyonadi
Ni mwisho wa zangu beti, si mwisho wa ukaidi
Fisadi ama kaidi, nitawaliza wabongo!
"Fisadi Chipukizi"
Natamani, natamani, na mimi niwe fisadi
Natamani, natamani, na mimi niwe zaidi
Natamani, natamani, na mimi niwe kaidi
Fisadi ama kaidi, nitawaliza wandugu!
Kwa kuwaliza wabongo, nataka niwe fisadi
Nije wapiga madongo, yaliyo ya kigaidi!
Hata mkila udongo, majani au zaidi!
Fisadi au kaidi, nitawaliza wabongo!
Mwenzenu natamania, ninaongeza juhudi
Nitauza Tanzania, halafu niwe hasidi!
Dharau ya kuringia , tafanya kwa makusudi
Fisadi ama kaidi, nitawaliza wabongo!
Najua hilo ni dili, yaani kuwa fisadi
Hata mkini jadili, mwenzenu nitawanadi
Hesabu za kikatili, napiga niwe fisadi
Fisadi ama kaidi, nitawaliza Wabongo!
Na wala sina huruma, ni sifa yangu fisadi
Halafu tena nasema, nauza hata vya jadi
Nasema mtanikoma, msichezee kaidi!
Fisadi ama kaidi, nitawaliza Wabongo!
Na kila chenye thamani, mwenzenu nita kinadi
Sitoufanya utani, hata mpate shahidi
Fidia ya ki mjini, nitawatoza na kodi
Fisadi ama kaidi ,nitawaliza wabongo!
Mseme hili na lile, na wala sito jirudi
Mpige hata kelele, mfie kwenye migodi
Niuze hata vya kale, halafu mje vikodi
Fisadi ama kaidi, nitawaliza wabongo!
Kaditama ya tamati, kikomo changu fisadi!
Misitu pia na miti, kati ya nitavyonadi
Ni mwisho wa zangu beti, si mwisho wa ukaidi
Fisadi ama kaidi, nitawaliza wabongo!
"Fisadi Chipukizi"