Nataka niwekeze gari zangu mbili kwenye kampuni ya uhakika zifanye biashara, ushauri tafadhali

Nataka niwekeze gari zangu mbili kwenye kampuni ya uhakika zifanye biashara, ushauri tafadhali

G Sam

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2013
Posts
11,795
Reaction score
36,704
Wakuu salaam,

Kama mada inavyosema nina gari zangu mbili zipo tu hazina shughuli. Moja ni Ti Carina na nyingine ni Spacio new model, sitaki kuwapa madereva wa mtaani maana sitaki usumbufu. Nataka nizisajili kwenye kampuni ya uhakika ili ziniingizie fedha ya uhakika bila gari zenyewe kupata dhoruba za hapa na pale za hawa madereva wetu.

Mwenye kujua sehemu ya uhakika naomba tusaidiane tafadhali na wazo litakalonifaa kisha nikali apply na kuona matokeo yake napenda kusema kwa dhati kuwa nitatoa fadhila kwa aliyetoa wazo hilo.

Naomba tusaidiane kwa wale wenye mawazo tafadhali.
 
Kumbe ukali wako wote kwa amgufuri ni kwasababu ya Vyuma kukaza. karibu kwenye ujasiliamali kamili

Wakuu salaam,

Kama mada inavyosema nina gari zangu mbili zipo tu hazina shughuli. Moja ni Ti Carina na nyingine ni Spacio new model, sitaki kuwapa madereva wa mtaani maana sitaki usumbufu. Nataka nizisajili kwenye kampuni ya uhakika ili ziniingizie fedha ya uhakika bila gari zenyewe kupata dhoruba za hapa na pale za hawa madereva wetu.

Mwenye kujua sehemu ya uhakika naomba tusaidiane tafadhali na wazo litakalonifaa kisha nikali apply na kuona matokeo yake napenda kusema kwa dhati kuwa nitatoa fadhila kwa aliyetoa wazo hilo.

Naomba tusaidiane kwa wale wenye mawazo tafadhali.
 
Hizo gari zako zote kama zimeshapita miaka kumi ni skreppa *(despite wewe kuziita new model gari za miaka ya 2001). Na hakuna kampuni inayohangaika na skreppa...🙄
 
Hizo gari zako zote kama zimeshapita miaka kumi ni skreppa *(despite wewe kuziita new model gari za miaka ya 2001). Na hakuna kampuni inayohangaika na skreppa...🙄
Mkuu gari zangu ziko makini na siwezi kuagiza gari 2001...Una lingine?
 
Kumbe ukali wako wote kwa amgufuri ni kwasababu ya Vyuma kukaza. karibu kwenye ujasiliamali kamili
Nimeagiza nyingine za awamu ya tatu sasa naona haya yapo tu. Huwa bahati mbaya siwezagi kuuza kitu nachomiliki! Nikikichoka sana nampa mshkaji wangu
 
Kumbe ukali wako wote kwa amgufuri ni kwasababu ya Vyuma kukaza. karibu kwenye ujasiliamali kamili
Ukali wangu kwa Magu uko palepale kutokana na sera zake mbovu za kiuchumi. Tupeane ushauri mkuu!
 
Mkuu, tatizo la uber unawekewa a limited space kwenye kichukua. Hii inahatari maana unaweza siku ikaisha hujaona kitu!
Yaani limit kivipi?
Idadi ya trip au?
 
wakodishe chadema, mwisho wa siku wadai bil.7 kama alivyofanya mfalme mboye
 
Back
Top Bottom