Natamani Misiba ya Wahaya iwe mingi kwani inatusaidia sana Kuimarisha Afya zetu kwa Vyakula na Kuoka Bajeti zetu za Kimaisha

Natamani Misiba ya Wahaya iwe mingi kwani inatusaidia sana Kuimarisha Afya zetu kwa Vyakula na Kuoka Bajeti zetu za Kimaisha

Sawa mtani, ila mnabid na nyie mfe kwa wingi ili na sisi tujenge afya pia

Sent using Jamii Forums mobile app

Mkuu na ' Mtani ' vipi hujasikia labda ' Msiba ' wowote wa Mhaya mwingine mwenye Hela na Utajiri hapa Dar es Salaam ili niunganishe baadae nikitoka Karimjee nielekee huko? Vifo vyenu vinaokoa sana ' Bajeti ' zetu za Maisha hapa mjini hasa ukizingatia hali ya Kimaisha sasa ni ngumu sana kama siyo mno.
 
Naunga mkono hoja. Mi nataka wapare wadedi kwa wingi ili tubadilishe menu kwa kufakamia makande kwa wingi huku tukijifunza kubana matumizi kwa kugonga ugali kwa picha ya samaki perege.

Cc Mshana Jr , NAKWEDE
Heee. Kumbe mchawi namba moja humu jf ni mpare??


,[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahah jamaa kajichanganya kwenye anga mbaya amekutana na gazeti la matusi.

Sent from my Redmi Note 5 using Tapatalk

Nitaomba katika hilo hilo Gazeti unionyeshe hayo ' Matusi ' ili nami niyajue ila ninachojua tu ni kwamba neno Mjinga lipo mara 12 katika Kitabu Kitakatifu cha Biblia na neno Pumbavu / Mpumbavu lipo mara 24 katika Kitabu hicho hicho Kitakatifu cha Biblia hivyo kama maneno hayo mawili ambayo Mimi hupenda mno na sana kuyatumia ya Mjinga ( Ngumbaru ) na Mpumbavu ( Popoma ) ni ' Matusi ' basi nadhani hayo ' Matusi ' nitakuwa nimejifunza kwa Baba Muumba / Maulana / Mola / Mwenyezi Mungu mwenyewe.
 
Unaponiambia nije na Ng'ombe wa Kuchinja Msibani wakati unajua fika kuwa Mimi nakuja ' Kushibia ' katika hiyo Misiba yenu ' Wahaya ' unamaanisha nini labda?
Namaanisha hakuna vya bure hapa, tutawapa wengine chakula ila mtu akigundulika ni mkurya anakaa na njaa yake.

[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wahaya tafadhalini endeleeni Kufa ili wana Mkoa wa Mara ( Musoma ) tuje Kula, Kunywa na Kusaza Majumbani mwenu. Na naomba Mungu sana Wahaya wakishamaliza Kufa wote sasa zamu iwe kwa Waha kisha Wanyiramba, Wanyaturu, Warangi na Wakara ili tuweze ' Kushiba ' huko Misibani mwenu.

Jamani bado naendelea kuwapa Pole zangu nyingi sana Watanzania wote, wana Familia wa CMG, wana Tasnia ya Habari nchini, Familia yake nzima Baba na Mama pamoja na wale Wapendwa wake wote ambao wameguswa kwa namna moja au nyingine na Msiba huu mzito wa Ndugu yetu ' Genius ' wa Entertainment, Creative Industry na Media Marehemu Ruge Mutahaba.

Tupo pamoja katika Msiba ( siyo Cyprian ) mzito kabisa na pigo kwa nchini na Sisi Watani zenu wana Mkoa wa Mara ( Musoma ) tumeumia na kusikitika mno kwani ni kupitia huyu huyu Marehemu Ruge ndiyo aliweza ' Kuwahimiza ' Wahaya wote hasa Wanawake wawe wanapenda na kujipendekeza sana kwa Wanaume wa Mkoa wa Mara ( Musoma ) na kutulazimisha tuwaoe huku wakisema kuwa Wanaume wa Kagera ( Bukoba ) hawajui Kupenda, hawapigi na hawajeruhi pia.

Nawasilisha.


Eti uende kula kwa Muhaya ushibe, kuna kabila hapa Tanzania ambao ni wachoyo wa asili ya chakula zaidiya Wahaya? Muhaya kwake chakula ni Mungu, jamaa ni wachoyo kishenzi. usitegemee kwenda kwa Muhaya akakukaribisha chakula hata siku moja.
 
Pumbavu ni wana Ukoo wako wote pamoja nawe. Wahaya ni Watani zetu wakubwa mno na hakuna Watu ninaowapenda kama Watani zangu Wahaya, Waha, Wanyiramba, Wanyaturu, Wakara na Warangi. Na isitoshe nimeleta hapa huu ' Uzi ' ukiwa ni Jukwaa la Utani. Halafu ni nani aliyekuambia kuwa katika Msiba Watu hawaruhusiwi Kutaniana? Hivi Wewe ' Takataka ' unajua dhana nzima ya ' Utani ' kuwepo katika Jamii ya Watanzania? au unadhani Mimi GENTAMYCINE sijaumia na siumii Kufariki Kwake Ruge Mutahaba?

Nakumbuka miaka ya 90 huko wakati wa Msiba wa Kaka yake Mwalimu Nyerere ( R.I.P ) pale Butiama ( waliokuwepo watanirekebisha ) Watani zetu hawa hawa Wahaya wakati Jeneza liko mbele walikuwa Wahaya fulani wawili wakawa wanalikalia huku wakilifanyia ' dhihaka ' za kila aina na wakisema kuwa Wazanaki na Mwalimu Nyerere tumemtoa ' Kafara ' Marehemu kisha wakasema Marehemu haendi Kuzikwa hadi kupatikane Pesa fulani na nakumbuka Hayati Mwalimu ilibidi pale pale awaite Wazee wa Kimila pamoja na hata Mzee Butiku ili Hela ya Watani ipatikane na wapewe na hilo lilifanyika haraka sana na wakapewa hizo Pesa na kuruhusu Marehemu akazikwe Mwitongo.

Ili uone kuwa Utani una Faida kubwa kuliko uwazavyo Mpumbavu Wewe ile Hela ambayo Watani zetu Wahaya waliiomba Sisi tulidhani labda wanataka tu kwenda ' Kuitumbua ' lakini huwezi amini Watani zetu hawa Wahaya ile Hela pamoja na zao ( walizochangishana ) wao kwa wao walienda Kununua Ng'ombe na Mahitaji mengine ya pale Msibani ndipo Sisi wengine ambao bado tulikuwa wadogo tukaujua umuhimu wa Utani hasa kwa Makabila ya Tanzania zaidi ya 120.

Siku zingine acha kuwa Mpumbavu tafadhali na hawa Watani zangu Wapendwa Wahaya, Waha, Wanyiramba, Wanyaturu, Wakara na Warangi nitaendelea ' Kuwatania ' hadi Siku ile na Mimi naingia Kaburini Kulazwa na bado nasisitiza hakuna Watu ninaowapenda na kuwaheshimu kama Watani zangu hao na ndiyo maana hata wakinisema ( wakinichana ) huwa nakuwa mpole kwani ni Wajomba na Shangazi zetu.

Pumbavu.
Mkuu watanie uwafariji achana hao wa kizazi cha Doti komuu..
 
Hapana....kanda ya mbali nanyi...

Sent using Jamii Forums mobile app

Umeshaona wana Mkoa wa Mara ( Musoma ) tunakufa Kizembe Kizembe kama Wahaya, Waha, Wanyiramba, Wanyaturu, Warangi na Wakara? Na kwa taarifa yako tu hakuna Watu ambao Mwenyezi Mungu amewapenda na amewachagua kuishi muda mrefu ( miaka mingi ) kama wa kutoka Mkoani Kwetu Mara ( Musoma ) Mkoa ' uliobarikiwa ' kwa kila Kitu. Kwanza mnatakiwa mtuheshimu sana kwani bila Sisi wana Mkoa wa Mara ( Musoma ) kupitia Hayati Mwalimu Nyerere nchi hii isingekuwa Huru hivi na kama haitoshi hata huu ' Usalama ' Wenu hapa Tanzania bila Wana Mkoa wa Mara ( Musoma ) kuusimamia hadi hivi leo mngekuwa mmeshapigwa na Uganda, Malawi, Kenya na hata Rwanda. Mnatakiwa mtushukuru mno na sana tu.
 
Genta..... Bwana umenikumbusha mbali kwa utani wako, ila ni vema maana babu yako aihamia huko toka Bukoba miaka mingi iliyopita, wewe ni mjukuu wa Wahaya

Sent using Jamii Forums mobile app

Niambie ' Mtani ' wangu. Pole na poleni pia kwa Msiba huu mzito na tuko pamoja. Japo naendeleza hapa ' Utani ' Wetu ila nisiwaficheni nina ' Huzuni ' kubwa na kila nikiliona ' Jeneza ' la Marehemu Ruge hapa katika Runinga najiona ' ninalia ' na kinachoniliza zaidi ni kwamba sina hata 5% ya ' Thamani ' aliyokuwa nayo Marehemu Ruge kwa Jamii yetu na ameondoka bado nadhani Jamii ikiwa inamuhitaji tena pengine kuliko hata Yeye ambavyo alikuwa akidhani au akijidhania. Ama hakika ni ' pengo ' kubwa na ' pigo ' kubwa katika Tasnia nzima na Watanzania wengi wenye ' mwamko ' wa Kimaendeleo, Ubunifu na Fursa.

Poleni nyote!
 
Namaanisha hakuna vya bure hapa, tutawapa wengine chakula ila mtu akigundulika ni mkurya anakaa na njaa yake.

[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]

Sent using Jamii Forums mobile app

Kuna Msiba mmoja Wahaya mlituhenyesha mno hivyo na Sisi safari hii ni zamu yetu. Ila kwa hizi Siku Tatu Nne Familia ya Mzee Mutahaba pale Mikocheni ' imenishibisha ' sana na Kuokoa ' Bajeti ' yangu hapa Mjini. Akhsanteni mno Watani zangu Wahaya na ndiyo maana bado nasisitiza Kwenu kuwa endeleeni ' Kufa ' kama siyo ' Kufariki ' ili tuendelee Kula na Kunywa bure bure.
 
Eti uende kula kwa Muhaya ushibe, kuna kabila hapa Tanzania ambao ni wachoyo wa asili ya chakula zaidiya Wahaya? Muhaya kwake chakula ni Mungu, jamaa ni wachoyo kishenzi. usitegemee kwenda kwa Muhaya akakukaribisha chakula hata siku moja.

Una ' Utani ' nao wa ' Kiasili ' kama Mimi au unawatafuta tu ' Ubaya ' Mkuu? Shauri yako na hapa JamiiForums wapo wengi tu hivyo ' utawakoma ' na anza Kujiandaa ' Kisaikolojia ' kwani najua hawatakuacha hivi hivi.
 
Mkuu watanie uwafariji achana hao wa kizazi cha Doti komuu..

Na ndicho nakifanya Mkuu na huwezi amini naandika hapa lakini nipo katika Huzuni kubwa na Majonzi makubwa. Jembe la Uhakika limeondoka na sijui kama litatokea Jembe jingine kama Marehemu Ruge Mutahaba a.k.a Jasiri Muongoza Njia.
 
Back
Top Bottom