Natamani sana FIFA izifungie taasisi tatu ambazo ni Simba, Yanga na TFF kwa kuendeleza siasa katika mpira wa miguu

Natamani sana FIFA izifungie taasisi tatu ambazo ni Simba, Yanga na TFF kwa kuendeleza siasa katika mpira wa miguu

Smt016

JF-Expert Member
Joined
Jan 11, 2016
Posts
3,012
Reaction score
4,300
Kilichotokea kipo kwenye mipango na wote wahusika wameshirikiana katika kutengeneza hili tukio, Simba na Yanga zinatumika na serikali katika kupumbaza watu, katika kupenyeza ajenda zao za kisiasa na katika kuwafanya watu wasahau kuhoji mambo ya msingi kama kuna matukio nyeti.

Kwanini nasema kimepangwa;

1) Simba na Yanga wamecheza mechi nyingi sana derby lakini hakuwahi kutokea huu utaratibu wa kufanya mazoezi ya mwisho kwenye uwanja wa Mkapa. Yanga anafanya mazoezi yake mwanzo mwisho kwenye kambi yake maalumu huku na wao Simba hufanya mazoezi yake katika kambi yake maalumu kisha watakutana uwanjani katika mechi husika. Imekuaje leo mambo yabadilike ghafla kwa Yanga na Simba kufanya mazoezi ya mwisho kwenye uwanja utakaotumika katika mechi?

2) Kulikuwa na uwezekano mkubwa kwa jana kufanyika maridhiano kwa timu ya Simba kupewa ruhusa ya kuingia uwanjani kufanya mazoezi yao ya mwisho kwavile meneja wa uwanja alikuwepo hivyo ilikuwa ni swala la maridhiano kwa kuruhusu waingie ndani, hao wazee walioshukiwa ni waganga wangehamriwa wabakie nje kwasababu sio sehemu ya wahusika.

3) TFF wameonesha kuhairisha mechi sababu kuu ni uzembe wa watu kushindwa kutoa taarifa kwa meneja wa uwanja, maofisa wa mechi na timu mwenyewe kuwa watautumia uwanja kwa siku ya Ijumaa.

Hapa taasisi zote tatu zimeshiriki kuwachezea mashabiki na wapenzi wa mpira uhuni, Simba hawakuwa na sababu ya kuzuiwa kufanya mazoezi, baada ya Simba kuzuiwa haikiwa sababu ya wao kugomea mechi na TFF na bodi ya ligi nao walipaswa kuonesha nguvu zao kwa kusimamia kanuni na sheria kwa sababu zinazoweza kupelekea mechi kuhairishwa.

TFF na bodi ya ligi wamedhihirisha wazi zipo kwaajili ya manufaa ya Simba na Yanga na sio chombo kinachoweza kusimamia haki kwa timu zote na ndio maana tumeshuhudia Azam na timu zingine zikicheza mechi back to back mfululizo ila wao Simba na Yanga ni malaika wanapewa wiki nzima zijiandae na mechi.

Timu zingine zinachezeshwa mechi mchana wa jua kali kabisa ila Simba na Yanga timu ya mtaji wa serikali watayayuka kwenye jua kali wao wanachezeshwa jioni au usiku.

Hili tukio ingekuwa ni timu tofauti na Simba na Yanga tungeona vifungu vya sheria vikifanya kazi. Sio ajabu kuona hizi timu mbili zikibeba mabango, ziki print tisheti kwa ujumbe wa wana siasa wa chama kilicho madarakani ni kwavile ni mtaji wa serikali.

Simba, Yanga na TFF unaofanyia uhuni mpira wetu kwa mambo yenu ya kisiasa
 
Imani za ushirikina ni ujinga unaodumaza maendeleo ya mpira Tanzania. Kwani wakiingia na wavaa kaniki itawapa ushindi? Tunalishana ujinga tu.

Simba na Yanga ni vilabu vyenye nguvu ya pesa. Adhabu ya faini haiwatishi ndiyo sababu wanarudia makosa. Ziwekwe adhabu za kupokonywa pointi.
 
Imani za ushirikina ni ujinga unaodumaza maendeleo ya mpira Tanzania. Kwani wakiingia na wavaa kaniki itawapa ushindi? Tunalishana ujinga tu.

Simba na Yanga ni vilabu vyenye nguvu ya pesa. Adhabu ya faini haiwatishi ndiyo sababu wanarudia makosa. Ziwekwe adhabu za kupokonywa pointi.
Simba na Yanga ni tatizo kwa soka letu ila TFF na bodi ya ligi ndio uozo kabisa ni kama vile wapo kwaajili ya maslahi ya hivyo vilabu viwili
 
Viongozi wa Bodi ya Ligi wakiongozwa na Stev Mngeto na Almasi Kasongo waachie nafasi zao kwa kufanya maamuzi kinyume na kanuni zinavyosema hawakufuata kanuni zinasemaje maana yake wanaendeshwa kisiasa na kishabiki wapishe viti vile wakae watu wanaofuata kanuni zinasemaje
 
Kitu maichojua wengi hii game kuahirishwa inabaraka za Simba,yanga,tff na serikali kiujumla..isingewezekana game kuchezwa jana
Watu wamesafiri kutoka Mataifa mbalimbali kuja kuangalia gemu halafu viongozi wa Bodi ya Ligi kirahisi tu eti wanasema gemu hakuna bila kuangalia kanuni zinasemaje wapishe nafasi zao zile hawazitendei haki, walichotakiwa kufanya Bodi ya Ligi Almasi Kasongo na Steve Mngeto na wenzao wengine ni kupiga kimya na kusubiri timu ambayo haitofika uwanjani kinyume na kanuni zinavyosema mpaka saa 3 au 4 usiku ya Jana wakija na tamko ya kuipiga rungu timu ambayo haikufika uwanjani Jana basi hio ndio ilitakiwa kufanyika hivyo na sio vinginevyo wao wanaleta siasa na ushabiki kwenye mpira wakati wanatakiwa kubakia neutral waachie viti vile
 
Kilichotokea kipo kwenye mipango na wote wahusika wameshirikiana katika kutengeneza hili tukio, Simba na Yanga zinatumika na serikali katika kupumbaza watu, katika kupenyeza ajenda zao za kisiasa na katika kuwafanya watu wasahau kuhoji mambo ya msingi kama kuna matukio nyeti.

Kwanini nasema kimepangwa;

1) Simba na Yanga wamecheza mechi nyingi sana derby lakini hakuwahi kutokea huu utaratibu wa kufanya mazoezi ya mwisho kwenye uwanja wa Mkapa. Yanga anafanya mazoezi yake mwanzo mwisho kwenye kambi yake maalumu huku na wao Simba hufanya mazoezi yake katika kambi yake maalumu kisha watakutana uwanjani katika mechi husika. Imekuaje leo mambo yabadilike ghafla kwa Yanga na Simba kufanya mazoezi ya mwisho kwenye uwanja utakaotumika katika mechi?

2) Kulikuwa na uwezekano mkubwa kwa jana kufanyika maridhiano kwa timu ya Simba kupewa ruhusa ya kuingia uwanjani kufanya mazoezi yao ya mwisho kwavile meneja wa uwanja alikuwepo hivyo ilikuwa ni swala la maridhiano kwa kuruhusu waingie ndani, hao wazee walioshukiwa ni waganga wangehamriwa wabakie nje kwasababu sio sehemu ya wahusika.

3) TFF wameonesha kuhairisha mechi sababu kuu ni uzembe wa watu kushindwa kutoa taarifa kwa meneja wa uwanja, maofisa wa mechi na timu mwenyewe kuwa watautumia uwanja kwa siku ya Ijumaa.

Hapa taasisi zote tatu zimeshiriki kuwachezea mashabiki na wapenzi wa mpira uhuni, Simba hawakuwa na sababu ya kuzuiwa kufanya mazoezi, baada ya Simba kuzuiwa haikiwa sababu ya wao kugomea mechi na TFF na bodi ya ligi nao walipaswa kuonesha nguvu zao kwa kusimamia kanuni na sheria kwa sababu zinazoweza kupelekea mechi kuhairishwa.

TFF na bodi ya ligi wamedhihirisha wazi zipo kwaajili ya manufaa ya Simba na Yanga na sio chombo kinachoweza kusimamia haki kwa timu zote na ndio maana tumeshuhudia Azam na timu zingine zikicheza mechi back to back mfululizo ila wao Simba na Yanga ni malaika wanapewa wiki nzima zijiandae na mechi.

Timu zingine zinachezeshwa mechi mchana wa jua kali kabisa ila Simba na Yanga timu ya mtaji wa serikali watayayuka kwenye jua kali wao wanachezeshwa jioni au usiku.

Hili tukio ingekuwa ni timu tofauti na Simba na Yanga tungeona vifungu vya sheria vikifanya kazi. Sio ajabu kuona hizi timu mbili zikibeba mabango, ziki print tisheti kwa ujumbe wa wana siasa wa chama kilicho madarakani ni kwavile ni mtaji wa serikali.

Simba, Yanga na TFF unaofanyia uhuni mpira wetu kwa mambo yenu ya kisiasa
Sahihi kabsa
 
Watu wamesafiri kutoka Mataifa mbalimbali kuja kuangalia gemu halafu viongozi wa Bodi ya Ligi kirahisi tu eti wanasema gemu hakuna bila kuangalia kanuni zinasemaje wapishe nafasi zao zile hawazitendei haki, walichotakiwa kufanya Bodi ya Ligi Almasi Kasongo na Steve Mngeto na wenzao wengine ni kupiga kimya na kusubiri timu ambayo haitofika uwanjani kinyume na kanuni zinavyosema mpaka saa 3 au 4 usiku ya Jana wakija na tamko ya kuipiga rungu timu ambayo haikufika uwanjani Jana basi hio ndio ilitakiwa kufanyika hivyo na sio vinginevyo wao wanaleta siasa na ushabiki kwenye mpira wakati wanatakiwa kubakia neutral waachie viti vile
Mbona huelewi ndugu yangu,..game isingeweza kughairishwa bila sababu wakasema game haipo..game ya Jana kughairishwa Ina baraka za team zote mbili,bodi ya ligi na serikali kale ni ka mchezo tu ili mechi ionekane imeshindwa kufanyika.
Siku game itakaporudiwa utajua kwanini ilighairishwa..
Ule wa Jana ni mchezo wa kuigiza tu
 
baraka za team zote mbili,
Yanga wamesema hio tarehe ya gemu nyingine hawatocheza sasa hizo baraka za timu ya Yanga nani aliekwambia Yanga imekubariana na maamuzi ya Almasi Kasongo na Steve Mngeto?
 
Yanga wamesema hio tarehe ya gemu nyingine hawatocheza sasa hizo baraka za timu ya Yanga nani aliekwambia Yanga imekubariana na maamuzi ya Almasi Kasongo na Steve Mngeto?
Doh bas kama hujanielewa na hapo hutanielewa tena ..hiyo ni script ndugu yangu may be una kichwa kizito ..
Ukiambiwa Simba na yanga ni team za kisiasa hiyo ndo maana yake..
Hiyo game itapangiwa tarehe na itachezwa vizuri tu ..
Fungua kichwa chako Toka kwenye ushabiki ndo utanielewa nachosema..
Kwani game ya 2021 yanga walisemaje baada ya kuondoka s hawatacheza game nyngne,game haikuchezwa..
Simba na yanga ni zaid ya uzijuavyo..
 
Yanga wamesema hio tarehe ya gemu nyingine hawatocheza sasa hizo baraka za timu ya Yanga nani aliekwambia Yanga imekubariana na maamuzi ya Almasi Kasongo na Steve Mngeto?
Mkuu toka nje kidogo waza vitu kwa upana. Yanga ni mwenyeji wa huo mchezo, unadhani wataonesha kirahisi tu kuwa wameridhia na maamuzi wakati wamewaingiza watu na taasisi nyingi katika hasara? Hayo ni maigizo tu ili kuwafariji mashabiki na kuwahadaa kama vile hakuna kilichopangwa ila kila kitu kipo kwa mipango. Kuhairishwa kwa huu mchezo umetokana na mambo tu ya kisiasa.
 
Mkuu tokea nje kidogo waza vitu kwa upana. Yanga ni mwenyeji wa huo mchezo, unadhani wataonesha kirahisi tu kuwa wameridhia na maamuzi wakati wamewaingiza watu na taasisi nyingi katika hasara? Hayo ni maigizo tu ili kuwafariji mashabiki na kuwahadaa kama vile hakuna kilichopangwa ila kila kitu kipo kwa mipango. Kuhairishwa kwa huu mchezo umetokana na mambo tu ya kisiasa.
Kabisa mkuu..
 
Doh bas kama hujanielewa na hapo hutanielewa tena ..hiyo ni script ndugu yangu may be una kichwa kizito ..
Ukiambiwa Simba na yanga ni team za kisiasa hiyo ndo maana yake..
Hiyo game itapangiwa tarehe na itachezwa vizuri tu ..
Fungua kichwa chako Toka kwenye ushabiki ndo utanielewa nachosema..
Kwani game ya 2021 yanga walisemaje baada ya kuondoka s hawatacheza game nyngne,game haikuchezwa..
Simba na yanga ni zaid ya uzijuavyo..
Bodi ya Ligi imewatia watu hasara kwa maamuzi yao ya kiduanzi, alieogoma kucheza apigwe rungu lake yanga apewe point 3 na magoli 3 na yule aliegoma apigwe rungu
 
Bodi ya Ligi imewatia watu hasara kwa maamuzi yao ya kiduanzi, alieogoma kucheza apigwe rungu lake yanga apewe point 3 na magoli 3 na yule aliegoma apigwe rungu
Sorry for you..una kichwa kizito sana.
 
Kilichotokea kipo kwenye mipango na wote wahusika wameshirikiana katika kutengeneza hili tukio, Simba na Yanga zinatumika na serikali katika kupumbaza watu, katika kupenyeza ajenda zao za kisiasa na katika kuwafanya watu wasahau kuhoji mambo ya msingi kama kuna matukio nyeti.

Kwanini nasema kimepangwa;

1) Simba na Yanga wamecheza mechi nyingi sana derby lakini hakuwahi kutokea huu utaratibu wa kufanya mazoezi ya mwisho kwenye uwanja wa Mkapa. Yanga anafanya mazoezi yake mwanzo mwisho kwenye kambi yake maalumu huku na wao Simba hufanya mazoezi yake katika kambi yake maalumu kisha watakutana uwanjani katika mechi husika. Imekuaje leo mambo yabadilike ghafla kwa Yanga na Simba kufanya mazoezi ya mwisho kwenye uwanja utakaotumika katika mechi?

2) Kulikuwa na uwezekano mkubwa kwa jana kufanyika maridhiano kwa timu ya Simba kupewa ruhusa ya kuingia uwanjani kufanya mazoezi yao ya mwisho kwavile meneja wa uwanja alikuwepo hivyo ilikuwa ni swala la maridhiano kwa kuruhusu waingie ndani, hao wazee walioshukiwa ni waganga wangehamriwa wabakie nje kwasababu sio sehemu ya wahusika.

3) TFF wameonesha kuhairisha mechi sababu kuu ni uzembe wa watu kushindwa kutoa taarifa kwa meneja wa uwanja, maofisa wa mechi na timu mwenyewe kuwa watautumia uwanja kwa siku ya Ijumaa.

Hapa taasisi zote tatu zimeshiriki kuwachezea mashabiki na wapenzi wa mpira uhuni, Simba hawakuwa na sababu ya kuzuiwa kufanya mazoezi, baada ya Simba kuzuiwa haikiwa sababu ya wao kugomea mechi na TFF na bodi ya ligi nao walipaswa kuonesha nguvu zao kwa kusimamia kanuni na sheria kwa sababu zinazoweza kupelekea mechi kuhairishwa.

TFF na bodi ya ligi wamedhihirisha wazi zipo kwaajili ya manufaa ya Simba na Yanga na sio chombo kinachoweza kusimamia haki kwa timu zote na ndio maana tumeshuhudia Azam na timu zingine zikicheza mechi back to back mfululizo ila wao Simba na Yanga ni malaika wanapewa wiki nzima zijiandae na mechi.

Timu zingine zinachezeshwa mechi mchana wa jua kali kabisa ila Simba na Yanga timu ya mtaji wa serikali watayayuka kwenye jua kali wao wanachezeshwa jioni au usiku.

Hili tukio ingekuwa ni timu tofauti na Simba na Yanga tungeona vifungu vya sheria vikifanya kazi. Sio ajabu kuona hizi timu mbili zikibeba mabango, ziki print tisheti kwa ujumbe wa wana siasa wa chama kilicho madarakani ni kwavile ni mtaji wa serikali.

Simba, Yanga na TFF unaofanyia uhuni mpira wetu kwa mambo yenu ya kisiasa
Yanga kosa lake lipi?? Meneja wa uwanja ni mwajiriwa wa Yanga?? Simba kazuiliwa na yanga kuingia uwanjani??

Sheria za mpira zinasemaje?? Unadai haki kabla au baada ya mechi?? Ukinijibu hayo maswali nitakuwa na wewe kujenga hoja ya mada yako
 
Mkuu toka nje kidogo waza vitu kwa upana. Yanga ni mwenyeji wa huo mchezo, unadhani wataonesha kirahisi tu kuwa wameridhia na maamuzi wakati wamewaingiza watu na taasisi nyingi katika hasara? Hayo ni maigizo tu ili kuwafariji mashabiki na kuwahadaa kama vile hakuna kilichopangwa ila kila kitu kipo kwa mipango. Kuhairishwa kwa huu mchezo umetokana na mambo tu ya kisiasa.
Hao viongozi wa Bodi ya Ligi ndio wamefanya maamuzi ya kijinga
 
Back
Top Bottom