Natamani watu kama Spika Tulia, Lissu, Shivji, Mwakyembe, Kabudi, Halima na Masereka waandae kongamano. Tuone jinsi Tulia atakavyowatoa jasho

deblabant

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2022
Posts
2,650
Reaction score
4,065
Dr. Tulia Ackson kishawaambia mkataba hauna vifungu vyenye kasoro. Lissu anasema vipo vyenye kasoro. Kabudi anasema hakuna vyenye kasoro. Shivji anasema Kuna vyenya kasoro. Masereka anasema Kuna vyenye kasoro. Feleshi anasema hakuna vyenya kasoro.

Hao wote ni wanasheria. Sasa sijui nani yuko sahihi. Ila ukizingatia Tulia ni Mwalimu wa lissu. Kabudi ni Mwalimu wa Shivji nk.

Naomba mtanange uandaliwe tuone jinsi Tulia atakavyowatoa mbio.

NB. Lissu ana GPA ya 3.6. Shivji ana GPA ya 3.8. Tulia ana GPA ya 4.5 na kabudi ana GPA y 4.9. huu mtanange tujue nani mbabe
 
Tulia ni mwanafunzi wa Issa ama hujui?
 
Tulia anayetembelea PhD ya maandishi bila uzoefu ndo awatoe jasho magwiji. Hajawahi kusimamia kesi za kimataifa ndo asimame na Lisu, Rugemeleza, n.k?
 
Huyu ndiyo awatoe mbio wakina Shivji![emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Kati ya hao uliowataja,tulia ndiye kalaza wa mwisho.
 
Sidhan kama unaweza kua think tank hata kweny kikao cha walevi!!
 
Kuwa mwanasheria ni jambo moja ...na kuwa mwanasheria wa biashara na mikataba ni Jambo lingine...

Shivji ni more of a political scientist than a corporate lawyer...

Ndo maana wenzetu Wana somea specific law degree kwenye industry husika...kuna mpaka Entertainment lawyers....
Sisi mtu kasomea Criminal justice....anaenda YouTube kujifanya Mtaalam wa " law in International investment"...mradi kaitwa mwanasheria basi anajua "kila kitu"..

Ndo maana upumbavu ni mwingi sana hata Kwa unaofikiri ndo wasomi
 
Mi mwenyewe naitamani sana hii battle. Niliona Tulia alivombana Halima Mdee njia nyembamba siku ile bungeni Halima akaanza kuweweseka nikasema dah huyu Tulia anapaswa kuandaliwa battle na watu design ya uliowataja
 
Naihurumia shingo yako, imebeba tofali!

Hebu tuambie, umeweza kujibu kwa vifungu vya sheria hoja ngapi alizotoa Prof. Shivji jana?

Ajabu, wewe layman, kwasababu tu unajua wapo wanasheria wanao specialise kwenye specific field, basi ndio unajiona una mandate ya kupinga nondo alizotoa Prof. Shivji jana, usijue wapo manguli competent in more than one field.

Hujui pia, mwanasheria anaweza akawa ame- specialise kwenye field moja, lakini pia akawa anazifahamu A,B,C's za field nyingine, na hiyo pekee itamtosha kuonesha njia.

Hujui kitu.
 
Kabudi ni mdogo kwa Shivji kiumri, hawezi kuwa Mwl wa Shivji. Shivji ameandika vitabu na machapisho ya kisheria zaidi ya 300. Afrika hakuna. Infact Shivji alitakiwa apewe DLitt.

Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app
 
Mleta mada hili swala la bandari sio swala la ligi ,eti katarama inakimbia kuliko ally's huo ni ujinga.
 
Upo sahihi...jamaa kapuyanga kidogo.
 
Hata kuelewa mtu alichoandika huwezi....wapi nimemtaja Shivji?..
Au Shivji yupo kichwani mwako??...
Jihurumie wewe kwa ujuaji wa kipumbavu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…