Nateswa sana na jini mahaba

Nateswa sana na jini mahaba

Pole sana ndugu kwa huo mkasa unaokutesa. Hapa kitu ulichokosea kabisa ni kwenda kwa waganga. Amini huyo jini hatakuacha, na hutakuja kufanikiwa kumkimbia hata kwa kujiua.

Kikubwa; Fanya maombi sana, tubu zambi zako na ufunge ukifanya maombi. Watu tunapitia mengi. Pia huwa nasumbuliwa sana na ndoto za hovyo lakini sijawahi enda kwa mganga. Zaidi huwa napambana kukemea hadi nakuwa sawa.

Ipo siku ntasimulia mwanzo mwisho wa hizi ndoto nazoota mara kwa mara.
 
HII NDIO TIBA SAHIHI, 90% Ya wadau humu wana imani hizo za ajabu, na ni sababu ya mazingira ya jamii yetu, upungufu wa uwelewa ikiwemo elimu, maisha duni

Na Imani hizi zimeshamiri sana maeneo ya Pwani, na baadhi ya kusini

Kuendelea kuamini ugonjwa unakomaa, NI MAGONJWA YA AKILI NA UNAUSABABISHA MWENYEWE

Sorry mm sina taaluma yeyote, NI IMANI YANGU TU na kama ni vinginevyo Mwenyezi MUNGU ANISAMEHE
Ni kweli magonjwa ya akili yapo ila pia na haya yanayoelezwa humu pia yapo, sehemu zenye hizi imani na hayo mambo ndio yapo.
 
Jini mahaba, chuma ulete, limbwata, kurogwa ni matatizo ya watu masikini tu. THINK


BTW hizo ni image umezitengeneza mwenyewe kichwani MATATIZO/ CHALLENGES zipo kutufunza ni formula you cant grow if you dont face challenges usifikirie zimeletwa na mtu au kiumbe.
Unaweza ukawa sahihi kwa mtazamo wa maeneo ambayo hakuna sana imani za kishirikina na hivyo watu hawajishughulishi sana na ushirikina hivyo huwezi kusikia visa kama vya chuma ulete, issue kama ya kurogwa tatizo huwezi kutofautisha kurogwa na tatizo la kawaida kwa kuangalia kwa macho tu kwa sababu huo uchawi unaweza kuwa ni chanzo cha tatizo ambalo ni tatizo la kawaida ambalo laweza kusababishwa na sababu zengine za kawaida.
 
Kuna uwezekano mkubwa sana hauko "possessed" na "evil spirits" tafuta msaada wa kisaikolojia huku ukimwomba Mungu, vijana wengi wanapata shida za kiakili na kisaikolojia (mf. Personality disorders, depression, stress, schizoid behavior nknk) sasa kwa vile jamii yetu haina uelewa Wa mambo haya, watu wanakimbilia kuaminishana uchawi, majini, mapepo, kulogwa n.k. ukipata mtaalamu mzuri wa magonjwa ya akili au ya kisaikolojia, utashangaa na utarudi kutushukuru.
 
Ndio nadhan ni wa asili yetu aliwah mpata marehem babu yng...kukutana nae nawezaje na nifanyaje nimkatae assinisumbue kbsa
Msaada wa kwanza.

Uliza kwenye asili yenu, kuna ambaye hayo mambo yanayokusibu wewe yaliwahi mkuta? Waulize wazee, babu bibi kama wapo. Usipopata namna ya ku deal nayo huko,

Unaweza ku deal nayo wewe kama wewe, lakini inataka moyo na ubishi
Maana mimi sitakuelekeza kwa mganga! Ntakuelekeza ukutane nalo live uso kwa macho alafu ndo umwambie sasa unachotaka kumwambia, kama hiwezi achana navyo komaa we pambana na maisha kibishi, likiona hueleweki nalo halitaeleweka vile vile maana hujali..

Ni madhaifu pia ukiyapatia.
 
Nielekeze namna hiyo
Msaada wa kwanza.

Uliza kwenye asili yenu, kuna ambaye hayo mambo yanayokusibu wewe yaliwahi mkuta? Waulize wazee, babu bibi kama wapo. Usipopata namna ya ku deal nayo huko,

Unaweza ku deal nayo wewe kama wewe, lakini inataka moyo na ubishi
Maana mimi sitakuelekeza kwa mganga! Ntakuelekeza ukutane nalo live uso kwa macho alafu ndo umwambie sasa unachotaka kumwambia, kama hiwezi achana navyo komaa we pambana na maisha kibishi, likiona hueleweki nalo halitaeleweka vile vile maana hujali..

Ni madhaifu pia ukiyapatia.
 
Wapo wanaowah kuitambua hali na wapo wanaochelewa kuitambua hali
Unajua hii mada imekuja hapa si kwa bahati mbaya, tena ukute kuna wahanga wengi sna ila hawajui watapata suluhisho wapi, hebu km una majibu tupeni tupate kupona, hii ni vita tutumie silaha zoteee.
 
Amen Amen
Tambua kwamba mwili wako si nyumba ya mashetani na majini mwili wako ni hekalu la Mungu,usi deal na huyo jini wala shetani gani deal na mwili wako,safisha hekalu la Mungu,unajua unaweza lalamika kwanini Mende hawaishi ndani kwako na kila siku unaweka dawa? shida sio dawa

unazoweka zakuzuia mende,shida ni CHANZO kinachosababsha mende kuja ndani kwako Yawezekana jikoni ndani kwako kuna uchafu na masalia ya vyakula kila iitwapo LEO kamwe mende hawawezi isha nyumbani kwako,utatumia kila dawa ila Mende waturudi tu,KWANINI? kwasababu uchafu ndio misingi ya nyumba yako.

SASA BASI achana kudeal na majini au mashetani Tuanze na jambo 1 tu ambalo kufanya usafi wa hekalu la bwana (huo mwili wako) Acha kila kitu unachotumia kisichompendeza Mungu.

Jisafishe,Jitakase kuwa serious katika hili,Kwenye maombi yako usitamke "Mungu namkataa huyu jini" nk nk wewe wakati unaomba mwambie "Mungu safisha mwili wangu,hili ni hekalu lako" mahali pako pa kupumzikia, nisafishe BABA nitakase..

Omba toba,omba utakaso,omba roho mtakatifu aingie ndani yako (yani fanya kama humjui jini) wewe deal na mwili wako komaa eneo hilo,Ukishampokea roho mtakatifu akakushukia maana yake Utakua safi.

sasa baada ya kumpokea roho mtakatifu,Dunda na Mia zako tuone huyo jini mahaba ataingia nyumba ipi wakati mwenye nyumba yupo ndani anatawala,Ajaribu bahati yake aone kitachomkuta.

Brother unapambana vita ya kiroho sio ya kimwili,lazima ukubali kuacha kila takataka ya dunia ili alie juu (roho mtakatifu) aweze kukushukia akusaidie, vita sio vyetu vita ni vya alie juu.

Ndio mana nimekwambia hata kwenye maombi usimpe kiki kwa kumtaja "jini mahaba sijui" usimpe showtime kabisa komaa na maombi ya utakaso,jiweke safi Nakuhakikishia ukishakua safi Hayo mengine unayoyataka yatakua Automaticaly tu.

Hamnaga Mende nyumba safi,hamnaga Panya nyumba safi ukiona hao viumbe jua kuna shida mahali shda si wao shda ni "wewe" na hata ktk hili mimi nina ujasiri kukwambia shda sio "jini mahaba" shida ni wewe. Badilika chukua hatua.
 
Amen Amen
Kuna special case.
Inawezekana ukawa mtu mtulivu sana,na HUJAWAHI KUFANYA ZINAA(kama wewe ni bikra hakikisha unasali sana,hawa viumbe hupenda sana mtu msafi wa aina hiyo sababu ya kuwapa material fulani ya kichawi muhimu kwao).Lakini kukawa na jambo fulani umelifanya kuondoa ulinzi wa kiungu,labda hufanyi ibada,au una stress sana etc.Ghafla haya maviumbe yakaanza kukuandama.
Ujue hapo kinachotafutwa ni nguvu zako za uhai kupitia sperms(unavyolala na kuota unafanya navyo mapenzi actually ni njia ya kukufanya uwape material hiyo muhimu sana katika ulimwengu wao wa roho na uchawi.
Na kwa case hii inawezekana pia pakawa na mkono wa mtu,yaani wachawi na wanapendelea kuiba nguvu hizo toka kwa watu wasafi wasiofanya uasherati,ulevi etc

Principle ni ile ile tu.Tafuta pale ulipopungua mbele za Mungu,fix it,then fanya ibada endelevu.Yatakwisha.
Huwezi kutibu kitu endelevu kwa kutumia tiba ya mara moja.
Kama majini na wachawi hawachoki,wanakutaka kila siku,then you need to be a man of prayers daily all your life.
Pengine kuna swali unajiuliza,why me?The answer is very simple..BECAUSE IT'S YOU.
Sisi binadamu tulivyo tofauti sura zetu na muonekano basi mpaka kiroho ni hivyo hivyo.
Wapo wenye mvuto wa kiroho kuliko wengine na hawa kama wasipojitambua na kujua waishije,huishia kuwa na tabu sana hapa duniani.
Utakuta kijana mzuri,ana akili na kila sababu ya kuwa namna fulani,lakini hayuko hivyo.
So usije ukajifananisha na watu why wao wako na amani,wanafanya maovu na wanasonga mbele,lakini wewe ni vita tuu hadi uishi mfumo fulani wa maisha.
Ujue una namna yako katika ulimwengu wa roho kinachovutia wanaoendesha ulimwengu huo so unapaswa kujitambua.
 
Amen Ame
Katika kusaidiana kupata msaada wa Mungu,mimi nina jambo ninalolifahamu ambalo ningependa kukupa naamini linasaidia sana,ni very powerful weapon katika vita hizi.
Nalo ni moja tu...JINA LA MWENYEZI MUNGU.
Jaribu kila usalipo utamke Jina halisi la Mwenyezi Mungu kumuomba msaada.
Na uwe unarudiarudia sala hiyo(iwe fupi) mara kwa mara hata utembeapo,uwapo ofisini etc.
Sijui wewe ni dini gani,ila mimi nafahamu Jina la YAHWEH mkuu,Muumba mbingu na nchi.
Sisi wakristo tunapomaliza kusali huwa tunasema KWA JINA LA BABA,MWANA NA ROHO MTAKATIFU.
Sasa hapo mimi hutamka majina halisi,yaani YAHWEH,YAHSHUA na RUACH ELOHIM.
YAHWEH ni Jina kuu la Mwenyezi Mungu,maana yake MIMI NIKO(and bring everything into existence).Halafu YAHSHUA(YESU) maana yake ni YAHWEH NINAYEOKOA na RUACH ELOHIM maana yake ni Roho/pumzi/upepo wa Mungu wenye nguvu na uelekeo according to his purpose.
Sasa hebu tafsiri hili unakuwa unamuita Mungu anayeishi(aliyepo),ambaye amekufanya uwepo,na anaweza kukutendea neno unalomuomba akalifanya likatokea(likawepo),akuokoe kwa kutumia nguvu yake ya kiungu (roho) ije kutenda kile ulichoomba but according to his will.(Huu upepo/Roho ndio tool ambayo Mungu anaitumia kufanya analotaka liwepo likawepo its a certain divine power,force.)
Matamshi haya pekee tayari ni mkataba kati yako na Mungu na sala itakayofuatia lazima itende kazi katika maisha yako kwa namna ya kipekee sana.Nazungumza kitu nilichokiexperience in real life.
Angalizo tu,huwezi kufikia kumuita Mungu kwa kiwango hiki halafu usiwe serious na ulichoomba.Ni jambo lenye uwajibikaji ndani yake.Imeandikwa Kila alitajaye Jina la Mungu na auache uovu.Na pia imeandikwa "Usilitaje BURE jina la Mungu".
Kama umeamua kufikia hatua hii basi uwe na shida yenye uzito wa kufanya hivyo, uwe rohoni umeamua kwa dhati ndipo umuite Mungu kwa staili hii.Vyovyote iwavyo majibu utayapata.Kama uko serious utapata majibu na pia kama hauko serious utayapata majibu yatakayokufanya uwe serious!
Sometimes tukiwa tumeelemewa sana hatuwezi hata kujiamini kutunga sala ili umfikishie Muumba wako.
Kama uko katika hali hiyo,unaweza tu kuchukua biblia,tafuta kitabu cha Zaburi,Soma Zaburi sura ya 10;1-17 kwa ajili ya kupambana vita na roho yoyote chafu.Unaposoma Zaburi hii kila penye neno BWANA sema "El Meez" maana yake "Mungu mtetezi wa wanyonge" na moyoni mwako ukimwona hivyo.Ukimaliza mwambie El Meez nisaidie mimi fulani mwana wa..(tamka jina la kwanza la mama yako).
Atakuja Ruach Elohim kukusaidia kwa nia ya Yahweh akiwa kama El Meez msaada wako.
Zaburi hii ya "kivita" iendane na Zaburi za toba (Zaburi 6 na Zaburi 25).Unaweza usiku kusoma zaburi hizi za toba na asubuhi kabla ya kuanza shughuli zako unasoma ile ya mapambano.Ufanye hivyo mpaka pale utakapoona nafsini mwako kwamba umeomba vya kutosha kilichobaki ni Mungu mwenyewe kujibu,then switch to Zaburi sura ya 8.Ni ya kushukuru,kusifu na kuabudu na kutambua mamlaka ya kibinadamu ambayo Mungu amekupa juu ya nchi na hakuna wa kukuondolea mamlaka hiyo.
Unairudisha mamlaka yako na akili zako kwa Muumba wako na wewe mwenyewe,badala ya kuhofu na kuwaza viumbe wengine walioumbwa kama wewe tu,na hawana cha kukufanya ukisimama na Mungu wako.

God bless you,na ushinde,ukaishi kwa Jina lake.
 
Matatizo yeyeto ya mtu utatuliwa na mtu mwenyewe.Kwenda kwa mganga au mchungaji ni maamuzi ya pili.
Wewe umeriruhusu jini lifanye makao mwilini mwako na wewe ndiwe mwenye uwezo wa kulitoa kupitia imani.
 
Habari za muda huu ndugu zangu.

Mimi ni kijana Me 26 nimekulia maisha yenye furaha sana mpaka nilipofikia umri wa miaka 24 na kugundua mwili wangu haupo sawa. Yani nasumbuliwa na kiumbe aitwa jini mahaba apo awali nilikuwa nahisi furaha kupata ndoto ya jima na mwanamke ila hasara za huyu kiumbe nimeziona nilipoingia kwenye mahusiano na binti mcha mungu sana.

Ni miaka miwili sasa nateseka kwa aliewahi kupata tatizo langu ni rahisi kunielewa. Nimezungu kwa waganga wa jadi wengi sana wenye uweledi ila nimekuwa nikilitatua tatizo langu kwa kipindi kifupi na kurudi. Tokea nimemtambua uyu kiumbe na kuanza vita nae amezidi kuniandama na kufunga mpaka riziki zangu. Nimefukuzwa kazi, nakataliwa na watu, nadhulumiwa kwenye jasho langu nimekuwa mtu wa kulia sana na kuomba lakini wapi.

Sifahamu ametokea wapi au ametumwa na nani? Ngoja niwaelezee kidogo kuhusu uyu kiumbe na mateso yake kwangu...Uyu kiumbe sio kama mashwetani wa kawaida ukisema akiitwa atazungumza na kueleza dhamira yake. uyu kiumbe anapoona kuna makali ya kumuumiza mfano maombi au dua hutoka na kuondoka na baada ya dawa kuisha hurudi hiyo ndio sababu kubwa ya kushindikana kuondoka kwa huyu kiumbe.

Baada ya kufuatilia mlolongo wa maisha yangu ya nyuma baada ya kutambua nina kiumbe huyu ndani mwangu nimegundua, mwanamke hunipenda ila mimi sitompenda nitamtumia na mwishowe nitamuachia huzuni ya kumuacha, kosa kubwa ni mimi nikimpenda mwanamke zitafanyika hila zozote za kunifanya nishindwane na huyo mwanamke, mfano nitashindwa kumuingilia uyo mwanamke kila nikitaka kufanya hivyo uume hutoweza kufanya lolote ila nikienda kwa mwanamke mwingine naweza niliwahi kuambiwa ni kwamba anapata wivu ndio sababu ya kuniharibia "nimewapoteza bila sababu wengi sana niliokuwa nawapenda nimeumia sana" nipo na mwanamke mcha mungu amekuwa akiniombea na ni strong nadhan ndio moja ya sababu kumshindwa kiumbe huyu

Nimemuingiza katika vita sababu ya upendo wake anapambana sana na mimi katika vita hii, anapata mandoto usiku ya kumtisha anaona wanawake wanamjia na kumwambia umeamua kumfanya unavyotaka sio, baada ya kuwa natumia gharama nyingi kwa waganga kwa ajili ya tatizo langu aliamua kufunga riziki zangu nisipate hata 100 ili nisiweze kufanya jitihada zozote za kumuondoa. Nimeachishwa kazi bila sababu. Apa nilipo sina hata senti.

Vihoja vya mateso kwenye maisha yangu ni vingi sana hata kukumbuka nashindwa nimekuwa kwenye kifungo kikubwa sana nimeenda madhabau mengi na tofauti kanisani, kwa mashekh, kwa waganga ila sijapata auheni zaidi ya uyu kiumbe kuzidi kunipatia mateso. Hivi ninanyoandika nimechoka na kuishi kwa sasa ni mwanamke wangu ambae sina imani katika safari yangu kama nitafika nae.

Nateseka nateseka haswa. Siku uyu binadamu wa karibu yangu pekee atakapo kata tamaa na mimi basi na mimi sitokuwa na budi kuiacha dunia na kupata pumziko la milele, sioni faida ya kuishi apa nilipo nmeuza mali zangu nyingi nilizokuwa nazo ila napota ela bila kujua kufahamu. huu ni moja ya mfano mmoja kati ya mingi ya ajabu iliyonikumba niliwahii kuchukua simu ya mtu nimelekee mteja ili niipaate elf20 ya udalal ila nilienda kushikwa na kuambiwa nimeiiba ile simu na kuwekwa ndani ila baada ya siku2 iligundulika ile simu sio ya wizi imefananishwa nikaachiwa, niliwahi kuitwa interview nilizunguka saa nzima naupita mlango wa chumba cha inteview mpak mda ukaisha.

Katika ndoto usiku naambiwa nawaona wanawake wananiambia wewe si mbishi tutakuonyesha. Nimechoka nahitaji msaada kwa njia yoyote ile inatosha naitaka amani, kuna wakati nalia sana usiku nakuomba...Mwili wangu ni wa nyama vita yang ni ya kiroho Mungu wangu ameniacha. Kuna wakati nawaangalia watu fulani na kutamani kuwa wao na kujiona mimi ni mkosi...Maisha yangu ni ya kulia tuu barabarani, nyumbani, kanisani.

Ewe binadamu unaefahamu msaada wa tatizo langu naomba unisaidie kutoka kufungoni Kwa namna yoyote. Na mungu atakubariki sana.

Asante sana
Mkuu polle kwa maswaibu hayo..ni kweli majini mahaba ukishaingia agano nao..ni wagumu kutoka. Kumbuka kama kuna siku uliwahi ota unafunga ndoa ...kama ishakutokea..basi jua huyo atakusumbua milele hadi uvunje agano nao. Binafsi lilinisumbua sana hadi nilipokabidhi maisha yangu kwa Yesu ndipo nikaweza vunja maagano nae. Na kuvunja agano sio kazi..ni kuweka maisha yako kwa Kristo Yesu..kwa kukiri kuwa bwana na mwokozi wa maisha yako. Hatua itayofuata ni kuvunja maagano yote uliyoweka na huyo jini, waganga wa kienyeji..maana nao hawana tiba ya kweli..ni kuuingiza zaidi kwenye vifungo vya shetani. Ukivunja kwa jina la Yesu na kwa damu ya yesu shatani hana ujanja. Ila inabidi uwe unamaninisha sana..ukiweza funga siku 7 ukiomba kila siku. Mungu ni mwaminifu sana.

Na kwa kuwa mwenza wako kakubari kusimama na wewe, shikamana nae..mfanye maombi na mungu atakufungua. Au tafuta wachungaji wa kweli..maana sikuhizi waganga ndio wachungaji wengi mjini..usipokuwa makini..utazinguliwa tu..ukate tamaa.
 
Asante, ni kwel nilishawah ota kuhusu ndoa ila nishaanza maombi naamini nitapona kwa jina la yes, ilikuchukua mda gan mpka kupona kwako mtumishi kabisa
Mkuu polle kwa maswaibu hayo..ni kweli majini mahaba ukishaingia agano nao..ni wagumu kutoka. Kumbuka kama kuna siku uliwahi ota unafunga ndoa ...kama ishakutokea..basi jua huyo atakusumbua milele hadi uvunje agano nao. Binafsi lilinisumbua sana hadi nilipokabidhi maisha yangu kwa Yesu ndipo nikaweza vunja maagano nae. Na kuvunja agano sio kazi..ni kuweka maisha yako kwa Kristo Yesu..kwa kukiri kuwa bwana na mwokozi wa maisha yako. Hatua itayofuata ni kuvunja maagano yote uliyoweka na huyo jini, waganga wa kienyeji..maana nao hawana tiba ya kweli..ni kuuingiza zaidi kwenye vifungo vya shetani. Ukivunja kwa jina la Yesu na kwa damu ya yesu shatani hana ujanja. Ila inabidi uwe unamaninisha sana..ukiweza funga siku 7 ukiomba kila siku. Mungu ni mwaminifu sana.

Na kwa kuwa mwenza wako kakubari kusimama na wewe, shikamana nae..mfanye maombi na mungu atakufungua. Au tafuta wachungaji wa kweli..maana sikuhizi waganga ndio wachungaji wengi mjini..usipokuwa makini..utazinguliwa tu..ukate tamaa.
 
Kuna uwezekano mkubwa sana hauko "possessed" na "evil spirits" tafuta msaada wa kisaikolojia huku ukimwomba Mungu, vijana wengi wanapata shida za kiakili na kisaikolojia (mf. Personality disorders, depression, stress, schizoid behavior nknk) sasa kwa vile jamii yetu haina uelewa Wa mambo haya, watu wanakimbilia kuaminishana uchawi, majini, mapepo, kulogwa n.k. ukipata mtaalamu mzuri wa magonjwa ya akili au ya kisaikolojia, utashangaa na utarudi kutushukuru.
Unachosema nakubaliana na wewe.
 
Back
Top Bottom