Natetemeka/Kigugumizi nikiongea Kiingereza

Natetemeka/Kigugumizi nikiongea Kiingereza

Wadau hii hali inanikuta nikitaka kutema yai sijui kwa nini tena nikiwa kwenye kadamnasi napata ubaridi zaidi. Msaada jamani naaibika mwenzenu.
** Tena nikiona mademu ndo jasho linanitoka mwili mzima, nifanyeje wadau?
From Chato? right?
 
Wadau hii hali inanikuta nikitaka kutema yai sijui kwa nini tena nikiwa kwenye kadamnasi napata ubaridi zaidi. Msaada jamani naaibika mwenzenu.
** Tena nikiona mademu ndo jasho linanitoka mwili mzima, nifanyeje wadau?
Hiko kiingeledha kiongee kwa kiswahili....imeisha hiyoo
 
Kuna siku nilienda ofisi fulani nilikuwa na shida na marketing manager katika hiyo ofisi kubwa tu.
Baada ya kumweleza secretary kwa ufupi akaenda kuniitia bwana.
Yule jamaa alikuwa mzungu inaonesha anatokea london mjini kabisa kwa akina blair, kingereza chake kilikuwa hakieleweki yaani anacharaza kama cherehani, labda akiongea ufanye kuandika kwanza. Yaani ilikuwa aibu pale.
Ili kujinasua, nikatema yai broken mfulululizo bila kumpa nafasi ya kuongea halafu nikasema thank you, nikamwambia secretary utamwelekeza vizuri kama nilivyokwambia eeh!
Ndio maana hiyo lugha siipendagi kabisa.
Mkuu! 😀😀😀😀
 
Back
Top Bottom