NATO na SCO zinatofautiana katika kudumisha amani na utulivu

NATO na SCO zinatofautiana katika kudumisha amani na utulivu

Yoyo Zhou

Senior Member
Joined
Jun 16, 2020
Posts
126
Reaction score
215
无标题.jpg
96e170fe87dcbf86ea9f2c361b56b4e7u5.jpg
Mkutano wa 24 wa Baraza la Viongozi wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Ushirikiano ya Shanghai (SCO) umefanyika hivi karibuni huko Astana, Kazakhstan, ukiwa na kauli mbiu ya “Kuimarisha Mazungumzo ya Pande Mbalimbali na Kutafuta Amani na Maendeleo Endelevu”. Mkutano huo umezingatia usalama wa kikanda na ushirikiano wa kiuchumi, na kutoa wito wa kukuza usalama, utulivu, maendeleo na ustawi, na kuhimiza ujenzi wa jumuiya ya binadamu yenye hatma ya pamoja.

Baada ya siku chache, nchi wanachama wa Jumuiya ya Mkataba wa Atlantiki ya Kaskazini (NATO) zilikutana huko Washington, ili kusherehekea miaka 75 tangu kuanzishwa kwa jumuiya hiyo. Kwenye mkutano huo, NATO ilitoa kauli zisizo za kweli kwamba China kuwa ni mhimizaji muhimu wa vita kati ya Russia na Ukraine. Kabla ya hapo, Katibu Mkuu wa jumuiya hiyo Jens Stoltenberg pia alidai kwamba China inapaswa kuwajibika na vita hivyo. Wachambuzi wanaona kuwa, madhumuni ya kisiri ya NATO kufanya hivyo ni kupata kisingizio cha kuingia barani Asia.

Zikiwa jumuiya za kikanda, katika miaka ya hivi karibuni, SCO na NATO zimekuwa na mwelekeo tofauti na kufanya maamuzi tofauti kabisa katika kudumisha usalama na utulivu wa kikanda na kimataifa.

Tangu kuanzishwa kwake miaka 23 iliyopita, SCO imetoa mchango mkubwa katika kukuza amani, utulivu, maendeleo na ustawi wa kikanda. Kutoka kwenye kushirikiana kupambana na “nguvu tatu za uovu” ambazo ni ugaidi, ufarakanishaji na misimamo mikali, kuzuia kwa pamoja kuenea kwa dawa za kulevya, kufanya mazoezi ya kijeshi ya pamoja ya kupambana na ugaidi, na kuanzisha mifumo ya mikutano katika ngazi zote, hadi kuhimiza utatuzi wa suala la Afghanistan, uwezo wa SCO kutatua suala la amani na usalama umeendelea kuboreka, na kuanzisha utaratibu mzuri katika kukabiliana na changamoto za kikanda. Jambo la kupongezwa zaidi ni kwamba, badala ya kutegemea hatua za kinguvu, SCO inazingatia zaidi maendeleo ya kiuchumi katika kutatua migogoro na kudumisha amani na usalama.

Kwa upande wa NATO, jumuiya hiyo iliyoanzishwa baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia, ina historia ya miaka 75, ilikuwa ikipingana na Jumuiya ya Warsaw Pact iliyoongozwa na Umoja wa Kisovieti. Baada ya kuvunjwa kwa Umoja wa Kisovieti na kumalizika kwa vita baridi, NATO ambayo ilipaswa kutoweka kabisa, imeendelea kutumika, na kuanzisha vita mara kwa mara duniani, na kuwa tishio kubwa kwa amani ya dunia. Katika miaka kadhaa iliyopita, vita nyingi zilizotokea duniani ikiwemo katika nchi za Kosovo, Iraq, Afghanistan, Libya zimeanzishwa na jumuiya hiyo. Vita inayozidi kupamba moto kati ya Russia na Ukraine pia ni matokeo ya moja kwa moja ya NATO kupanua nguvu yake katika eneo la mashariki.
 
Hii ni ishara tosha kwamba Marekani inafikia sasa inakaribia kilele cha tamati katika uongozi wake wa dunia.

Kwa wengi wasiojua, hii ni habari njema. Lakini ukweli ni kwamba wala siyo!

Historically, giants have never gone down without a desperate fight - in which they would rather drag all others down with them.
 
Back
Top Bottom