Natumiaje mafuta ya kuku kutibu masikio

shadownet

Senior Member
Joined
Aug 4, 2015
Posts
133
Reaction score
677
Habari zenu..mimi ni kijana ambae nasumbuliwa na kutosikia vizuri since 2007, Nimeenda hospitali nyingi na kutumia dawa za vidonge lakini tatizo halikatatuliwa.

Naombeni msaada wenu kwa wenye ujuzi na haya mambo ya tiba asili mnishauri ni jinsi gani ya kupata mafuta ya kuku ili niweze kutibu masikio, ni kuku yupi anahitajika na je hayo mafuta nayapataje
Asanteni
 
Mkuu nani aliekwambia mafuta ya kuku ni tiba ya masikio???
Nenda kwa daktari ukachunguzwe kwa kina
Acha mchezo na mwili wako
Kama haliumi na tatizo ni kutosikia vzr kuna spika wanakupa ta masikioni tena ni bure
 
Nunua kuku wa kienyeji hasa jike,ukisha mwandaa tayari kwa kupikwa,mchemshe bila maji maana atakuwa na maji aliyooshewa,maji yakikauka ataanza kutoa mafuta,hayo mafuta utayachukua na kuyaacha yapoe kisha utakuwa unamimina tone moja moja masikioni.

KUMBUKA: Hutapata mafuta ya kutosha.

TAHADHARI: Sijawahi kutumia mafuta haya,ila nasikia yanasaidia

MBADALA: Tumia black seed oil,tone moja asubuhi na moja jioni. Kama yatakuwa yaliyoandaliwa kiasili ni vyema ukayachemsha kabla ya kuyatumia. Hii ni tiba ambayo nina uhakika nayo.
 
Hiyo black seed oil ni kitu gan mkuu? nieleweshe
 
Kuku wa kienyeji haswa tetea(jike) ndio huwa na mafuta. Kuku akishachinjwa wakati unamsafisha ndani ya tumbo utakuta hayo mafuta.

Ukishayatoa weka katika sufuria kisha weka jikoni ili yayeyuke halafu yakipoa unaweza kuyahifadhi katika chupa safi kwa matumizi. Weka matone machache ndani ya sikio linalouma.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…