Nauliza utaratibu wa kubadili jina

Nauliza utaratibu wa kubadili jina

Pole sana kwa hiyo changamoto.

Ushauri wangu: usibadili jina kwa sababu tu baba yako hakutambui kama mwanaye.

Baba yako anaweza akawa hakutambui, lakini ndugu zake wanaweza wakawa wanajua ukweli kuwa wewe ni mtoto wa "baba yako"

Hata kama baba yako hakutambui kama mwanawe, ndugu zako hawataacha kukutambua kisa tu baba yako kakukataa

Isitoshe, kama yeye amekataa kukutambua, wewe amua kumtambua hata kama hamuwasiliani. Iwe mnawasliliana au hamuwasiliani, bado ataendelea kubaki baba yako. Hata ukibadili jina, bado utaendelea kubaki mwanaye wa damu ikiwa ndiye aliyekuzaa.

Kwa hiyo, usibadili jina kwa sababu hizo. Labda kama kuna sababu zinginezo.
Asante sana
 
Nilikuwa naitwa jina fulani, kutokana na Imani yangu ya Dini,jina nililopewa na wazazi wangu,
Baada ya kubadili Dini,mimechagua jina lingine linaloendani na imani yangu, Sasa nilitaka kubadirisha jina, kwenye cheti cha Nida na Paspoti naomba anayejua utaratibu wake anisaidie, Ninakaa Iringa mjini
Jina sio dini,

Vipi kama huko mbeleni ukataka kurudi kwenye imani yako ya mwanzoni? Je utabadiri tena jina?

Unaweza ukaitwa John na ukawa muislam safi au ukawa unaitwa Juma na ukawa mkristo safi.
 
Back
Top Bottom