Naumia, nami ni binadamu

Nimekuelewa
 
Hata ukikaa kimya na kunyamaza bado watasema tu.
Sikushauri kurudisha pesa kwa waliokusaidia vinginevyo endapo mtu aseme ndio anachokihitaji kurudishiwa pesa zake.

Hata baada ya kuandika huu uzi wataendelea kusema tu. Hautawazuia na hilo lipo nje ya uwezo wako.

Ukiweza, watendee wema wenye uhitaji.
 
Ni Mungu pekee awezae kuubadili moyo wako na kuufanya kuwa mgumu,
Kwani akikaa ndani yako na utaenenda kwa jinsi ya kiroho.
Wanadamu hawata kutenda kitu.

Lakini ukitegemea uwezo wako mwenyewe, wanadamu lazima wakuvyoge vyoge na kukuumiza.
 
Masikini pole sana mama, ndio walimwengu tulivyo. Usiwe ma moyo mwepesi wa kubeba mambo kiasi hicho dear. Hii dunia ina mengi na hayo ndio kwanzaaa kumekucha. I feel yo pain na nafikiri niliona hivyo vijembe kutoka kwa wawili wa waliokusaidia ila usipate taabu maana nafikiri tayari unawafahamu ni watu wa aina gani. Haupaswi kuwapa nafasi kabisa ya kuizuia furaha yako.

Hauna haja ya kurudisha hizo pesa, ichukulie tu kama funzo kwako na endelea na maisha yako. Mshukuru Mungu uko na afya njema sasa, muombe azidi kukupa afya ili upambane ufikie malengo yako.
 
Unaumia sababu unawapa attention...! Tenda wema uende zako sasa wao wametenda na hawakuondoka walibaki hapo na wewe ukaona ubaki pale badala ya kuondoka zako uwaache pale. Pole aggyjay kwa masaibu.
 
Ushauri wangu usirudishe ulichosaidiwa kama waliokusaidia hawajadai utakuwa unakosea. Hao wanaokudhihaki kwa shida ulizopitia kipindi cha nyuma iko siku yao. Hakuna anayependa kusaidiwa ila inafika mahali akili inagota kabisa unashindwa ufanye nini kutatua shida yako. Ipo siku yao ni heri wakaomba msamaha saa hii kuliko watacholipwa na Mungu wanaemuamini. Nimeandika haya kwa uchungu sababu nimewahi kupitia changamoto kama zako nimesaidiwa sana hata sasa bado nasaidiwa napokwama.
 
Write your reply... Ama hakika, umenisikitisha sana, au kuna baadhi yao walikusaidia wakijua watapata kitu kutoka kwako lakini ukawabania?

sikiaaaa sasa! hamna kurudisha hata mia hapo hao wanafik tu, kama vp change na username yako wasikuzoee tena_ na usiwe na mawasiliano nao hao ni wahuni sista.

nimetamani sana kujua mengi kuhusu wewe, ama hakika historia yako imenigusa sana.

KING OF THE JUNGLE!
jtj
 
Sawa mkuu
 
Asante mkuu,hasa ukiangalia wengine wanashusha shutuma,halafu si za kweli kabisa.its embarrassing.
Kuna watu wana dharau.
 
Sawa mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…