Naunga mkono Uwanja wa Ndege wa Chato. Una justification, utakuwa kama Ggabolite au Yamoussoukro. Watalii watamiminika!

Mara paaa umeukwaa udc[emoji23]
 
Chezea fasihi wewe.nawaonea huruma wale wanaoshangilia kila kitu kwa hili bandiko wametoka zeeero walah!
mkuu tumemuelewa na sisi tunaendeleza tu fasihi ...jamaa anaandika kibabe sana yaani ka anakwenda ka anarudi ghafla akata konaaa
 
Kama fasihi ni shida kwako, kabla hujashangilia kama wale mazwazwa washangilia kila kitu, basi ili umuelewe PASKAL jaribu kujishughulisha kuelewa Ggabolite na YAMOUSSOUKRO ni nini, hapo utakua umeelewa uandishi uliotumika.
 
dereva wa basi na kondakta wanahusika mzee baba.
 
majibu ya kondakta kwa mzee wa watu aliyekuwa akisinzia, mh.... 'you un.... ed son of the b... you think this bus belongs to your grandfather?" miaka hiyo 2005 umenikumbusha mbali
 
Mkuu Paschal na wewe siku zingine sijui huwa unatumia kinywaji gani jioni? Mwanza kwenyewe hawana uwanja wa ndege, Mkulu akimaliza muda wake nani atakuwa anaenda Chattle?
inahitaji umakini wa juu sana kumwelewa mayala a.k.a njaa soma aya za juu mwanzo nadhani hao ndio utamwelewa anachokisema. Pili soma aya za mwisho huku chini utajua anasema nini
 
Justification Why Chato International Airport
Japo sijabahatika kuzisikia hoja kwa nini ni Chato International Airport, lakini mimi nimebahatika kufika Chato ile ya jamaa yangu fulani akiwa waziri, ndio alikuwa akimiliki the best hotel in town ya Chato ile. Kuna wakati nilikuwa na assignment ya mwezi mzima Biharamulo, lakini niliishi Chato, nikapanga kwenye hiyo the best hotel in Chato, ni hotel ya vijumba jumba vya detached suites.....

Haya ni matusi kwa JPM
 
Ninyi hamjawahi kumuelewa Mayala,hiki alichoandika ni vijembe kwa utawala,anawazodoa kitaalamu,soma in between lines,utaelewa anachomaanisha.

Gabolite ni uwanja wa ndege ulijengwa na Dikteta Mobutu Seseseko kijijini kwao,

Alipoondoka kijiji kimekuwa pori,hakuna ndege hata moja inayotua.

Paschal anamfananisha anaehenga Chato na Aliejenga Gabolite,ukisoma andiko la Paschal usisome kama gazeti,huyo jamaa anaandika kifasihi zaidi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

kwahiyo Chato kuna magorofa siku hizi?
 
Mwezi January nilipita hapo Chato! Dah! kichekesho ... ukifika stand kuu kuna mabinti sijui wa wapi, wamevishwa vitisheti vya rangi ya kijani wanazunguka magari kwa ajili ya kuwauzia mahindi yaliyochemshwa, maziwa mgando, viazi, gonja n.k. Yaani Chato ni hovyo kabisa labda pajengwe uwanja wa ndege ili watalii waweze kujionea hali duni ya watanzania.
Kwa hilo la kuonesha umaskini wa watanzania wanaoishi kwenye nchi tajiri naunga mkono hoja - uwanja ujengwe Chato.
Tofauti na hapo .... hayo ni maamuzi ya mtu mmoja ... iweje aamue kwa ajili ya wengi? Huo wa BUkoba uliamuliwa na wengi na sijui ni kwa nini ulicheleweshwa?
 
Aendelee kuwafumba watu wakati anajua wabongo wengi ni mbumbumbu! Hatari hiyo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…