Navutiwa sana na simulizi za uhalisia wa maisha, msimuliaji akiwa mhusika

Navutiwa sana na simulizi za uhalisia wa maisha, msimuliaji akiwa mhusika

MwananchiOG

JF-Expert Member
Joined
Apr 4, 2023
Posts
1,970
Reaction score
4,037
Binafsi huwa ninapenda sana simulizi ambazo zina uhalisia wa maisha ya kila siku tunayoishi hususan kwetu sisi wapambanaji na watafutaji wa kila siku. Yaani simulizi ambazo msimuliaji ndiye mhusika na anasimulia kuhusu experience yake katika jambo au mambo fulani sanasana masuala ya utafutaji pesa, utajiri,hustle za maisha aliyoyapitia mpaka kufanikiwa au kufanikisha jambo fulani, ujasusi kidogo sio mbaya n.k Binafsi sivutiwi kabisa na simulizi za mapenzi, au kama zikichomekewa basi zisizidi sana (tatizo siku hizi wasimuliaji wengi wanalazimishia story za mahaba ndani ya simulizi zao) kitu ambacho kinaondoa kabisa uhalisia.

Sivutiwi na simulizi zilizokaa mtindo wa riwaya mfano wa hekaya za abunuasi.Unakuta msimuliaji anasimulia kuhusu maisha ya mtu mwingine! Wakati mwingine majina hayana uhalisia, utasikia mara franfurt, Jean pierre mara safari kuelekea New Orleans! au zile utasikia "Elliot Craig aliruka sarakasi na kumyatulia risasi Brown Carter" Hizo huwa naona zinekaa kitoto na kisekondari sana 😄

Binafsi navutiwa na ninapata mafunzo na hamasa za kimaisha nikisoma simulizi za baadhi ya waandishi humu jf kama UMUGHAKA, Analyse, SteveMollel, (kuna ile simulizi moja ya "Laana za maiti") mwandishi simkumbuki, Na simulizi zingine kama Magofu ya Rhapta (japo mwandishi alianza kuingiza mapenzi) n.k Kuna moja nimesoma juzi kati japo ameishia njiani (kutoka kwenye utajiri mpaka kuishi kwenye lindi la umasikini!)
by Poker n.k n.k

Sasa naendelea na msako kutafuta simulizi zingine za aina hii 😎
 
Sama
Samahani mkuu. Hivi zile simulizi za efm huwa hufuatilii?

Unakuta jibaba limeshika simu ya kitochi linasikiliza simulizi efm na haliko ladhi kukosa mwendelezo.

(samahani sio wewe mtoa mada)
 
Sama

Samahani mkuu. Hivi zile simulizi za efm huwa hufuatilii? Unakuta jibaba limeshika simu ya kitochi linasikiliza simulizi efm na haliko ladhi kukosa mwendelezo.(samahani sio wewe mtoa mada)
Nilikuwa nazipenda na nazikubali sana kipindi wahusika wenyewe/wahanga walipokuwa wanasimulia wao wenyewe!.

Kulikuwa na simulizi kali sana mfano kuna dada mmoja alisimulia walivyotekwa wakiwa kwenye gari kutoka arusha kuja DSM nyingine msela mmoja alisimulia alivyopitia harakati za wizi ukabaji n.k

Lakini tangu walipomkabidhi yule mdada sijui Veronica Frank asimulie kwa niaba ya wahusika sifuatilii tena! Wameharibu! Sijui kwanini wameamua kufanya hivyo
 
Sama

Samahani mkuu. Hivi zile simulizi za efm huwa hufuatilii?

Unakuta jibaba limeshika simu ya kitochi linasikiliza simulizi efm na haliko ladhi kukosa mwendelezo.

(samahani sio wewe mtoa mada)
Hua siwaelewi watu wanaosikiliza hy kitu
 
Sama

Samahani mkuu. Hivi zile simulizi za efm huwa hufuatilii?

Unakuta jibaba limeshika simu ya kitochi linasikiliza simulizi efm na haliko ladhi kukosa mwendelezo.

(samahani sio wewe mtoa mada)
Huwa nasikitika sana kuona mwanaume anasikiliza kile kipindi cha simulizi cha E-FM

Au wale wanaume wanaosikiliza vipindi vya mapenzi usiku. Eti dume zima linakaa linamsikiliza malaya Diva the Bawse
 
Hata hao uliowataja huenda walitunga pia ila ili kupata uungwaji mkono wakasema ni wao wenyewe.

Ile ni sanaa, labda kama umeanza kusoma story jf ila watunzi wengi wa riwaya walio mahiri unaweza kudhani yeye ni mhusika mkuu.

Na wapo wenye lifestory nzuri ila kusimulia hawajui, kinabaki kua ni kipaji cha wachache.

Mapenzi hayakwepeki kwa watafutaji, usizichukie story za mapenzi ni unkwepabo kwenye simulizi za hustles.
 
Hata hao uliowataja huenda walitunga pia ila ili kupata uungwaji mkono wakasema ni wao wenyewe.

Ile ni sanaa, labda kama umeanza kusoma story jf ila watunzi wengi wa riwaya walio mahiri unaweza kudhani yeye ni mhusika mkuu.

Na wapo wenye lifestory nzuri ila kusimulia hawajui, kinabaki kua ni kipaji cha wachache.

Mapenzi hayakwepeki kwa watafutaji, usizichukie story za mapenzi ni unkwepabo kwenye simulizi za hustles.
Kama wakifanya hivyo mbona fresh tu, kwa sababu wanaongeza ubunifu na mvuto.Hata ukisoma unajua unamsoma yeye sio unasoma simulizi unayosimuliwa na msimuliaji kuhusu maisha ya mhusika mwingine!

Kuhusu mapenzi ni kweli haiepukiki lakini isichukue 95% ya simulizi husika(kama haihusiani na mapenzi) maana naona wasimuliaji wengi wanalazimisha kuingiza hadithi za mapenzi ya kihindi hata kama sio muhimu.
 
Kama wakifanya hivyo mbona fresh tu, kwa sababu wanaongeza ubunifu na mvuto.Hata ukisoma unajua unamsoma yeye sio unasoma simulizi unayosimuliwa na msimuliaji kuhusu maisha ya mhusika mwingine!

Kuhusu mapenzi ni kweli haiepukiki lakini isichukue 95% ya simulizi husika(kama haihusiani na mapenzi) maana naona wasimuliaji wengi wanalazimisha kuingiza hadithi za mapenzi ya kihindi hata kama sio muhimu.
Bila kuweka hizo mambo ni ngumu kupata wafatiliaji wengi, wavumilie tu.
 
Subiria na Isidingo ya jf toka kwa SM 🤠🤠

Cc Smart911
Isidingo ccy😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂
Hivi huko kijijini ccy unalima nin maan kijijini ukae ww kupauka upauke ww alafu watu wa town ndio tunahangaika.
 
Isidingo ccy😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂
Hivi huko kijijini ccy unalima nin maan kijijini ukae ww kupauka upauke ww alafu watu wa town ndio tunahangaika.
Ndiwooo sis isidingo make kuna wahusika wanakufa na wengine wanazaliwa upyaaa yanii🤠!

Nalima sis na kilimo kinanipausha balaaaa kama unavoonaa 🤣!

Naona wa so called wa mujini mnahahaa na wakijijini Sio kidogoooooo!

Cc Smart911
 
Back
Top Bottom