Mie naongea kueleza uhalisia wa mambo na nasimama wanaoendesha Vitz ambao wanadharauliwa sana.
Usimdharau mtu kwa vitu unavyoviona. Kuna jamaa mmoja Kariakoo karibu na kituo cha Mwendokasi uwa anapanda daladala kuja kwenye biashara yake. Yule jamaa kwa siku anauza zaidi ya milioni 10 na ukimuona utadhani Mbwiga fulani tu
Wanavaa tishirt za jezi au formsix wakishapiga na kaptura zile za draftidrafti au zile kaptura za pocket pembeni, kuta wanavaa visendoz na soksi na miwani juu, walipokaa vingereza vingi utahisi mipango ya kweli kumbe ni swaga tu hua nacheka sana
Kuna mwanasiasa kasema mkishanunua IST na VItz na kuanza kuvaa kaptura fupi weekend mnajiona mmepatia sana maisha, mnajihisi ni middle class kumbe ni masikini wenye nafuu! Mjumbe hauwawi, weekend njema!