...Nawaona wajumbe wa Bunge la Katiba wakifungasha virago na kuondoka Dodoma

...Nawaona wajumbe wa Bunge la Katiba wakifungasha virago na kuondoka Dodoma

Bizney

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2013
Posts
454
Reaction score
48
Ndugu zangu wadau wana Jf na watanzania wenzangu

Kwa kinachoendelea Dodoma kama busara haikutumika, tutegemee wajumbe wa bunge la katiba wakifungasha virago na kuodoka zao bila kukamilisha kilicho wapeleka dodoma. Hii inatokana na vifungu namba 37 na 38 kutokufikiwa mwafaka mpaka sasa, watanzania tulitaraji kazi hiyo ingehitimu leo, lakini pamoja na mwenyekiti wa muda kuunda kamati maalumu ya maridhiano na mwafaka, bado mpaka sasa hakuna kilichofikiwa na badala yake wale walioona bunge la leo jioni tumeshuhudia mwenyekiti akivivuka vifungu hivyo nilivyovitaja cha 37 na 38 kuwa kamati ya maridhiano na mwafaka bado haijamaliza kazi yake.

Ndugu kimbuka vifungu hivi ndo vile vinavyo amua upigaji kura ya WAZI au ya SIRI.Hapa ndo naona watanzania wenzetu wajumbe wa bunge maalumu la katiba wanashindwa kuafikiana na baadhi kuanza kuondoka zao makwao. Kama mtanzania mwenye mapenzai mema na taifa letu kwa imani zaetu tuombe kwa ajiri ya taifa letu kama kuna watu wenye nia ovu washindwe.

UPDATES

Wadau awali nilidhani nijambo la kawaida lakini sasa kwa kinachoendelea Dodoma kuna kila sababu zinazotaia shaka kuwa huenda ni ya ccm si njema katika zoezi zima la mchakato wa katiba mpya.

Ndugu zangu tukumbuke kuwa utamaduni wetu wa upigaji kura kitambo sasa umekuwa ni wasiri, jambo linalo mpa uhuru mutu kuammua atakakacho, si mbali ni majuzi tu tumeshuhudia mwenyekiti wa muda bwana Kificho akipatikana katika mchakato wa upigaji kura uliohusisha kura ya siri. Kwanini zinajengeka hisia kuwa nia ya ccm ni OVU? Ni kwa sababu utamaduni wetu wa upigaji kura umekuwa ni wa siri, sasa wenzetu wanatuondoa kwenye utamaduni tulio uzoea na kutuambia kuwa huo ndo msimamo wao.
Kama mtakumbuka mwenyekiti wa muda aliunda kamati maalum kwa ajiri ya mwafaka na maridhiano na mashauriano, katika kamati hiyo inamuhusisha waziri mkuu Mh Pinda, mwenyekiti wa CUF Lipumba na mwenyekiti wa CDM Mbowe, katika hali isiyo ya kawaida ukweli ni kwamba wenzetu hawa wa kamati ya maridhiano walishindwa kufikia maridiano kwa kilichoitwa msimamo wa CCM. Pia mtakumbuka kuwa juzi Bunge liliahirishwa mpaka jana mchana saa9 Alasiri ili kutoa muda kwa kamati ya maridhiano kufikia mwafaka, kwa vifungu vilivyo achwa wazi makusudi bila kupitishwa, vikiwemo vile vyenye ukakasi ambavyo ni kifungu cha 37 na 38 vinavyo amua upigaji kura SIRI au WAZI.

Tunaambiwa kuwa kikao cha wabunge wa CCM kilicho kaa juzi saa 2 usiku na kukamilisha mazungumuzo saa 5:30 kilikuwa na lengo la wajumbe wa kamati ya maridhiano kutoa mrejesho juu ya kilicho fikiwa kuhusu uamuzi wa upigaji kura ya SIRI au WAZI, mwnyekiti wa kikao hicho alikuwa ni waziri mkuu Mizengo Pinda baada ya kufungua kikao alimkaribisha mjumbe wa Halimashauri kuu Mh Vuai Nahodha ili kutoa mrejesho wa maendeleo ya kamati ya mashauriano. Jambo alilo waambia wajumbe wa kikao hicho cha CCM kuwa kwa jinsi mazingira yalivyo nje na ndani suala la upigaji kura wa SIRI hauepukiki, na hapo ndo alisimama Ole Sedeka na kusema hawataki kisikia kura ya SIRI vinginevyo nikuiondoa CCM kwenye msimamo wa serikali 2. Seandeka alimwambia waziri mkuu kuwa kama atathubutu kuridhia upigaji kura wa SIRI awe tayari kuwajibishwa na chama. Na hapa ndo waziri mkuu wanatajwa kufunga kile kiao cha wabubge wa CCM kwa kusema kuwa kuanzia sasa msimamao wa chama ni kura ya WAZI na sivinginevyo.

Ndugu zangu hapa mtaona kwamba msimamo wa CCM ndo unatia shaka watu ndani na nje ya bunge la la katiba sasa wanaanza kuona ni wazi kuwa nia ya CCM katika hili si njema hata kidogo. katika misimamo huo wa CCM na makundi mengine wakiwemo wapinzani sitarajii mwafaka endapo kila kundi litasimama kideta kwa kile kinachoitwa msimamo usiyoyumbishwa. Nahapa ndo baadhi ya makundi yataamua kususa na kuondoka Dodoma. “Ukivuta nikavuta hakika itakatika”

Mungu ibariki Tanzania na watu wake.
 
...

Ndugu kimbuka vifungu hivi ndo vile vinavyo amua upigaji kura ya WAZI au ya SIRI.Hapa ndo naona watanzania wenzetu wajumbe wa bunge maalumu la katiba wanashindwa kuafikiana na baadhi kuanza kuondoka zao makwao. Kama mtanzania mwenye mapenzai mema na taifa letu kwa imani zaetu tuombe kwa ajiri ya taifa letu kama kuna watu wenye nia ovu washindwe.

Mkuu ondoa hilo neno "kama". Ni ukweli usiopingika kwamba nia ovu ipo kwenye hili swala la aina ya kura - siri Vs wazi. Utaratibu na aina ya upigaji kura katika taifa letu vinajulikana tangu enzi na enzi na ni somo ambalo vijana wetu wanafundishwa mashuleni (Civics). Jiulize kulikoni leo malumbano ya kijinga kwa swala lililo wazi namna hii!
 
Ni nchi ya wapumbavu na wazembe tu ndo inaweza kuamua watu wake wapige kura ya wazi. Mara zote wamekuwa ni wale madikteta wapumbavu. Madikteta welevu pia hawakuwahi kuchaguliwa kwa kura za wazi.
 
Sasa mimi nashangaa tena sana, watoe options zote anae taka kupiga kura ya wazi apige anae taka ya siri pia apige. Mimi napenda wapige za siri ndio demokrasia nzuri. Kuwa za wazi kunaweza leta uhasama baina ya pande mbili zinazo sagana.
 
Ndugu zangu wadau wana Jf na watanzania wenzangu

Kwa kinachoendelea Dodoma kama busara haikutumika, tutegemee wajumbe wa bunge la katiba wakifungasha virago na kuodoka zao bila kukamilisha kilicho wapeleka dodoma. Hii inatokana na vifungu namba 37 na 38 kutokufikiwa mwafaka mpaka sasa, watanzania tulitaraji kazi hiyo ingehitimu leo, lakini pamoja na mwenyekiti wa muda kuunda kamati maalumu ya maridhiano na mwafaka, bado mpaka sasa hakuna kilichofikiwa na badala yake wale walioona bunge la leo jioni tumeshuhudia mwenyekiti akivivuka vifungu hivyo nilivyovitaja cha 37 na 38 kuwa kamati ya maridhiano na mwafa bado haijamaliza kazi yake.

Ndugu kimbuka vifungu hivi ndo vile vinavyo amua upigaji kura ya WAZI au ya SIRI.Hapa ndo naona watanzania wenzetu wajumbe wa bunge maalumu la katiba wanashindwa kuafikiana na baadhi kuanza kuondoka zao makwao. Kama mtanzania mwenye mapenzai mema na taifa letu kwa imani zaetu tuombe kwa ajiri ya taifa letu kama kuna watu wenye nia ovu washindwe.

sehemu yeyote ikiwepo ccm lazima pawe na vurugu zisizo kuwa na maana.sababu ccm karibu wote hawana akili.
 
Sasa mimi nashangaa tena sana, watoe options zote anae taka kupiga kura ya wazi apige anae taka ya siri pia apige. Mimi napenda wapige za siri ndio demokrasia nzuri. Kuwa za wazi kunaweza leta uhasama baina ya pande mbili zinazo sagana.

Rekebisha hilo neno Mkuu! Ni kati ya makatazo tunayoomba Katiba Mpya iyazuie waziwazi.
 
Katiba isipo patikana CCM itakuwa imevuruga mchakato hivyo inatakiwa kikosi maalumu cha jeshi kiundwe kikawaue wajumbe waliotoka CCM. CCM ni hatari mara mia ya shetani hata shetani mwenyewe anaishangaa CCM kwa ukatili na upumbafu wake
 
Kura siri, mikataba wazi, msimamo ni upi sasa , kweli upinzani Tanzania bado
 
lengo lao kuongeza siku tu hakuna lolote si wamenyimwa laki saba sasa watafanya kila wawezalo hawa kupe ili waongezewe siku,
 
Ndugu zangu wadau wana Jf na watanzania wenzangu

Kwa kinachoendelea Dodoma kama busara haikutumika, tutegemee wajumbe wa bunge la katiba wakifungasha virago na kuodoka zao bila kukamilisha kilicho wapeleka dodoma. Hii inatokana na vifungu namba 37 na 38 kutokufikiwa mwafaka mpaka sasa, watanzania tulitaraji kazi hiyo ingehitimu leo, lakini pamoja na mwenyekiti wa muda kuunda kamati maalumu ya maridhiano na mwafaka, bado mpaka sasa hakuna kilichofikiwa na badala yake wale walioona bunge la leo jioni tumeshuhudia mwenyekiti akivivuka vifungu hivyo nilivyovitaja cha 37 na 38 kuwa kamati ya maridhiano na mwafa bado haijamaliza kazi yake.

Ndugu kimbuka vifungu hivi ndo vile vinavyo amua upigaji kura ya WAZI au ya SIRI.Hapa ndo naona watanzania wenzetu wajumbe wa bunge maalumu la katiba wanashindwa kuafikiana na baadhi kuanza kuondoka zao makwao. Kama mtanzania mwenye mapenzai mema na taifa letu kwa imani zaetu tuombe kwa ajiri ya taifa letu kama kuna watu wenye nia ovu washindwe.
zigawiwe karatasi wakati wa kupiga kura anaetaka kura ya siri apokee karatasi asiyetaka asipokee alafu mwenye karatasi apige kwenye karatasi na aliyekataa karatasi aulizwe ajibu kwa wazi, ili mradikaratasi ziwe na idadi inayoeleweka na ziwe maalum
 
Yatupasa kuombea taifa letu ili kupita vyema ktk kipindi hiki kigumu cha mchakato wa katiba mpya, vinginevyo tutavurugana mapesa yatateketea bule na kusifanyike lolote, huku tukibaki hatuelewani.
 
Back
Top Bottom