Nawashauri Azam sports club wamchukue yule kocha wa Geita golden

kwisha

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2021
Posts
1,779
Reaction score
4,982
Kwa watu ambao wanajua tactics za mpira vizuri watakubaliana na mimi. Yule kocha wa Geita gold ni kocha mzuri sana na ana mpira wa kisasa zaidi. Ukicheki jinsi Geita Gold wanavyocheza.

Wangelikuwa timu ambayo ina wachezaji wakubwa zaidi kama young, simba, na Azam kuna watu ambao wangelikuwa wanakula goli 3 mpaka 5.

Ninachompendea yule kocha hanaga mambo ya pass sijui tik tak yeye anajua kushambulia tu awe amefungwa, awe amefunga awe amedroo yeye ni kushambulia tu huo ndo mpira wa kisasa mambo ya tik tak hata barcelona wenyewe wamesha sau tayari.
 
Mie nawashauri wamchukue Baraza
 
Wachezaji wa AZAM wote wana vitambi sijui wanafanya mazoezi ya aina gani jana nilikuwa namuangalia ajibu naona anaanza kutoka kitambi na yeye yule kipa wao chigonya alikuwa na kitambi na yule wa zanzibar ana kitambi kocha wao kaanza kunenepa kiufupi AZAM hawana pressure ya matokeo.
 
Azam sio timu ya wananchi ukilinganisha na yanga, simba, mbeya city, n.k.

Na ukiwa mchezaji, kocha au mfsnyakazi wa club ya azam lazima unenepe na kutokujituma kwani hakuna pressure ya matokeo. Mashabiki wenyewe wa kukodi, nani atakusukuma kufanya vzr.

Mfsno kolo mwenyewe kuepusha lawama za matokeo kaamua mechi za awali ziwe za lupaso ili angalau apate chemistry maanaanajua akizingua mechi mbili za away hata kwa sare tu kelele zake sio za nchi hii ukizingatia kua watu wana hasira za mayele.
 
Uko sahihi kabisa. Hata Ajibu naye ndani ya muda mfupi tu aliokaa Azam, aliota kitambi cha ajabu! Azam kuna tatizo bila shaka.
 
hana sifa za kufundisha timu zinazocheza championship au confederation
 
Sifa anazo,Geita walisema ana leseni A ya CAF....Minziro hata mimi naona anafaa....msomali out.
hana sifa za kufundisha timu zinazocheza championship au confederation
 
unaeza shangaa akapewa timu kali ongala,kocha msaidizi
Msomali hana mbinu mbadala za kutafuta ushindi,hizi mechi mbili walizocheza zinafanana na mechi walizopoteza hapo Azam complex, timu inaishiwa maarifa hana la kuelekeza na wachezaji wanabaki kupiga backpass nyingi zisizo na faida.
 
AZAM kila sehem imejaa uswahili mwingi, wanapeana kazi kiswahili swahili hakuna anayejihis yupo responsible na kazi yake...
All in all nilisoma sehem kwamba Bakhresa alianzisha team ya Azam ili watoto wake wajiburudishe nayo kuisimamia hiyo team kama sehem ya burudani, baada ya mtoto wake mmoja kufia ktk mbio za magari (langalanga) akawakataza waache mchezo wa magari wajiburudishe ktk mpira... Maybe ndio maana hawapo serious sana kuisimamia team coz they've nothing to lose...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…