Nawauliza CCM wenzangu, Katiba mpya ina ubaya gani?

Nawauliza CCM wenzangu, Katiba mpya ina ubaya gani?

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,137
Reaction score
17,908
Kila linapoletwa ubaoni na mezani suala la Katiba mpya, wanaCCM huwa mbele kuvuruga kwa kelele kupiga. Katiba ya sasa ya Tanzania iliandikwa mwaka 1977, takribani miaka 44 iliyopita. Katiba hiyo imeshafanyiwa mabadiliko mbalimbali zaidi ya kumi. Ndiyo kusema bila kuhema kuwa Katiba ya sasa ina viraka na mabaka ya uhakika.

Mwaka 2014, Rais na Mwenyekiti Mstaafu Kikwete alianzisha na kuusimamia mchakato wa Katiba mpya. Akampa wajibu mujarabu wa kutafuta jibu la kikatiba kaka yangu Jaji Joseph Sinde Warioba na Tume yake. Hata Bunge la Katiba liliundwa lakini likashindwa.

Kule kwenye Bunge la Katiba, CCM liliuteka mchakato na kuuvuruga bila uoga. Mchakato ukafia kwenye Katiba Pendekezwa ambayo hadi leo haijawahi kuendelezwa wala kuzungumzwa. Kila kiongozi anayeshika madaraka, tena kwa haraka, husema kuwa Katiba mpya si ajenda yake.

Hivi sasa CHADEMA na wapendakatibampya wengine wameanzisha vuguvugu lisilo na vurugu la kutaka Katiba mpya. Vuguvugu hilo linakutana na mkono wa chuma usio na huruma kutoka Serikalini na chamani-CCM ili likwame kama kuzimika kwa umeme. Tayari mamia wamekamatwa na/au kushtakiwa kwa makosa mazitomazito na ya kuogofya.

Kwanini CCM na Serikali yetu tunaikataa na kuichukia Katiba mpya kiasi hiki? Kuupenda Mwenge wa Uhuru na kuung'ang'ania kwa miaka yote hiyo si mfano wa kubaki na Katiba ya sasa. Katiba ya sasa ina mapungufu mengi. Ina maswali mengi kuliko majibu. Katiba mpya ni jambo jema. Haipaswi kuchukiwa na kupingwa kwa kiasi hiki. CCM tubadilike.

IGP Sirro, kwanini umezungumzia kesi ya Mbowe iliyopo Mahakamani?

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
Hofu yao wakiikubali nguvu yao yakubambikia itayeyuka.
 
Mbaya sana tu kwetu sisi.

1) Mtatutawanya na kutupunguzia umoja ambao ni nguvu yetu kwamaana ya Chama Chetu, Dola, Serikali, Mahakama na Tume ya Uchaguzi.

2) Sisi tumezoea kuingia bungeni kivyetuvyetu, na kwa malengo yetu. Sasa mkileta hiyo katiba inayosema mbunge lazima awe na angalua ka degree kamoja, na sisi tunajua sifa kubwa ni kujua kupiga taarabu, na kuandika jina,-- hii hapana kabisa. Tukitoka bungeni nani atalinda maslahi yetu?

3) Sisi bwana tumezoea bora liende. Mkianza kusema tuwajibishwe kama hatufanyi kazi zenye matokeo chanya,,, hapana. Hii hatutaki.
Hatujazoea kupimwa sisi.

4) Sisi ni miungu watu. tukisema lolote like kwa jina la kijani na njano, limetoka. mkituondolea huo ukuu, itakuwa mwisho wetu na vizazi vyetu, hatutaki.

5) Tunalindwa na ujinga wa watu. ninyi mkija na sera zenu za elimu bora, uwazi sijui nini na kuwafungua watu vichwani, watatupanda vichwani. hatutki kabisa.

6) Tumezoea kufanya makosa makubwa ya mikataba filishi, ufisadi, udanganyifu n.k. Tuanogopa kioo chenu hicho.

7). Sisi ni matajiri wa raslimali nyingi kama majumba na viwanja vya mipira vingi vilivyojengwa na serikali, tuliviatamia wakati tunatengeneza vyama vingi. Sasa hizi choko choko za kutaka kuzirudisha serikalini sijui nini, sisi hatutaki.

8). Kwanza kuna kitu hamkijui, vyama vingi ilikuwa ni kuwaridhisha mataifa makubwa yasitunyime misaada lakini siyo hoja yetu wala agenda yetu ya ndani. Ninyi wa vyama vingine ni raba stamp ya kutustahilisha na kutuheshimisha lakini ninyi siyo halisi. JITAMBUENI HIVO. HAYA, UNA LINGINE? KWA HERI MWALIMU.
 
🤣🤣🤣 Mzee tupatupa umeupiga mwingi sana kwa wanaCCM kuhusu katiba mpya maana wanaikataa kwa nguvu ya dola ila sio nguvu ya hoja 🤣🤣🤣
Umeniua zaidi ulivyopiga chenga ya kuvunja nyonga kwa kumalizia na suala la IGP Sirro kuzungumzia kukamatwa Mbowe kwa makosa ya ugaidi kitu ambacho kisheria ni suala lililo mahakamani sio polisi
 
🤣🤣🤣 Mzee tupatupa umeupiga mwingi sana kwa wanaCCM kuhusu katiba mpya maana wanaikataa kwa nguvu ya dola ila sio nguvu ya hoja 🤣🤣🤣
Umeniua zaidi ulivyopiga chenga ya kuvunja nyonga kwa kumalizia na suala la IGP Sirro kuzungumzia kukamatwa Mbowe kwa makosa ya ugaidi kitu ambacho kisheria ni suala lililo mahakamani sio polisi
Wenyewe wanaruka na kukanyagana
 
Kila linapoletwa ubaoni na mezani suala la Katiba mpya, wanaCCM huwa mbele kuvuruga kwa kelele kupiga. Katiba ya sasa ya Tanzania iliandikwa mwaka 1977, takribani miaka 44 iliyopita. Katiba hiyo imeshafanyiwa mabadiliko mbalimbali zaidi ya kumi. Ndiyo kusema bila kuhema kuwa Katiba ya sasa ina viraka na mabaka ya uhakika.

Mwaka 2014, Rais na Mwenyekiti Mstaafu Kikwete alianzisha na kuusimamia mchakato wa Katiba mpya. Akampa wajibu mujarabu wa kutafuta jibu la kikatiba kaka yangu Jaji Joseph Sinde Warioba na Tume yake. Hata Bunge la Katiba liliundwa lakini likashindwa.

Kule kwenye Bunge la Katiba, CCM liliuteka mchakato na kuuvuruga bila uoga. Mchakato ukafia kwenye Katiba Pendekezwa ambayo hadi leo haijawahi kuendelezwa wala kuzungumzwa. Kila kiongozi anayeshika madaraka, tena kwa haraka, husema kuwa Katiba mpya si ajenda yake.

Hivi sasa CHADEMA na wapendakatibampya wengine wameanzisha vuguvugu lisilo na vurugu la kutaka Katiba mpya. Vuguvugu hilo linakutana na mkono wa chuma usio na huruma kutoka Serikalini na chamani-CCM ili likwame kama kuzimika kwa umeme. Tayari mamia wamekamatwa na/au kushtakiwa kwa makosa mazitomazito na ya kuogofya.

Kwanini CCM na Serikali yetu tunaikataa na kuichukia Katiba mpya kiasi hiki? Kuupenda Mwenge wa Uhuru na kuung'ang'ania kwa miaka yote hiyo si mfano wa kubaki na Katiba ya sasa. Katiba ya sasa ina mapungufu mengi. Ina maswali mengi kuliko majibu. Katiba mpya ni jambo jema. Haipaswi kuchukiwa na kupingwa kwa kiasi hiki. CCM tubadilike.

IGP Sirro, kwanini umezungumzia kesi ya Mbowe iliyopo Mahakamani?

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Hawa jamaa UNAFIKI ni silaha yao. Wanahubiri democracy huku hawawezi kuitekeleza !!

Ccm imejisokota ndani ya vyombo vya dola & vya maamuzi . Kujitoa huko wakawa sawa na UMD au hata TADEA hawawezi. Mpaka watu waumizane kwanza .

Mwisho wamakuwa na nguvu kwa sababu wa Tanganyika wana asili ya kutokujali haki zao.
 
Back
Top Bottom