Naweza kujenga nyumba kwa TZS Milioni 20?

Naweza kujenga nyumba kwa TZS Milioni 20?

vyumba vinne means one bed room, sebule moja, jiko na stoo moja na choo kimoja. ila vyote vinakuwa ndani

chumba kimoja cha msingi wa kozi tatu ni matofari 300 * 4 = 1200

au kozi tano ni matofari 500 * 4= 2000

maximum tofari 3000/50 = 60 mifuko ya cement. * 14000= 840,000
mafundi matofali + mchanga + machine+ kumwagilia= 900,000

fundi kujenga mpaka linta + kupiga linta na kuinua kozi za juu= 2,000,000

fundi kuezeka 600,000

mbao treated ( inategemea na design) maximum= 1,000,000

bati 28 geji 120 * 160,000= 2,300,000

dirisha moja 240000 * 10 = 2,400,000

milango 7 * 150,000= 1,050,000

kupiga ripu fundi + cement + mchanga = 800,000( ndani) + 800,000 ( nje)

gypsum = 60 * 14,000= 840,000

fundi gypsum + rangi= 600,000

tyles nyumba yote = 1,500,000

fundi tiles= 500,000

wiring vifaa= 1,500,000

fundi wiringi = 600000

pigeni jumla ni ngapi haya ni mahesabu ya juu sana
Ishirini haifiki inaishia kama 18m nimekubali
 
Maliwato vipi au ndio akagonge kwa jirani?
Choo ametaja
Mbona mwasahau maliwato jamani?

13289toilet_bowl.jpg
 
Jenga mkuu, tena ikiwezekana nenda na ndugu na jamaa muwe mafundi wasaidizi, kubeba zege, tofali, kuchanganya mchanga n.k. Boma lako litolee jasho, utabana matumizi na kupiga tizi hapo hapo, vifaa hakuna kutuma mtu, chukua quotes toka kwa fundi, kanunue mwenyewe..
 
Kwa kuwa kiwanja unacho millioni 20 mbona unahamia kwenye nyumba lakini finishing hutamaliza. Angalia mgawanyo wa gharama ( I assume uko Dar es Salaam na nyumba unayojenga ni ya mtu anayejenga nyumba yake ya kwanza):
  1. Matofali 5,000 @700=TZS3,500,000
  2. Mafundi (kujenga toka msingi mpaka kuezeka)=4,000,000/=
  3. Cement mifuko 150 @15,000=2,250,000/=
  4. Mbao zote TZS4,000,000/=
  5. Bati 60 @ 15,000=900,000/=
  6. Fundi umeme na vifaa vyake=5,000,000/=
  7. Finishing (madirisha na milango)=5,000,000/=
  8. Finishing (plastering + ceiling works)=5,000,000/=
1, Maji bado
2, Mchanga bado
3, Kokoto bado
4, Kibali cha kujenga bado.
5,Mashimo ya Maji machafu.
6, Nondo za linter.
Ni afadhali ukanunua machine ya Matofali ya kufunganisha. Ukafyatua wewe Na rafiki yako. Au ukanunua Matofali hayo. Ukatafuta Fundi wa kuyapanga.
 
Kwa Usimamizi Bora wa Ujenzi.

Kwa Ujenzi wa Majengo Bora

Kwa Gharama Nafuu

Pamoja na Ubora wa Hali ya Juu

Usisite Kutupigia

*EYES ON*

Real Estates Company

Tupo
DAR-ES-SALAAM-Makumbusho


Tunasimamia kila Hatua ya Ujenzi

Kuanzia
1.Vibali
2.Ramani za Nyumba
3.Upimaji wa Viwanja/Hati
4.Ujenzi wa Nyumba/Finishing
5.Kupangisha Nyumba za Makazi au Biashara

Tupigie:-
OMARI RAJABU
STAFF EYESON
DSM HEADQUARTERS

*MAKUMBUSHO COMPLEX*
1 st FLOOR
0715-908698(Call/SMS/Whatsapp)
0759-538688(Call/SMS)
 
Jamani siwezi kujenga nyumba ya vyumba vinne hapo Dar kwa milioni 20? Niambieni kama siwezi kabla sijaipoteza hii pesa...

Asante

Nunua kiwanja kilichopimwa Dar es Salaam upate na hati maeneo kama mbweni mwisho mwisho. Baada ya miaka mitatu utakiuza kwa gharama kubwa alafu hiyo hela utakayopata ndiyo ujengee nyumba.
 
Milioni 20 ni vihela vidogo sana.
Toa mchanganuo usiseme vihela vidogo kwa vile huna hata mia umkatishe mtu tamaa.au unadhani anataka kujenga masaki?au pale opposite na posta.au karibu na kempisky?
 
Unaweza kujenga mkuu tena vizuri,inategemea unajenga wapi,kama ni pale karibu na BOT haitoshi lakini kama ni nje ya mji unajenga vizuri,cha muhimu usianze kufanya chochote bila kupata quotation ili usikwame mahali.
 
Asanteni wote kwa input yenu,nyumba bado finishing,kwa experience yangu nyumba million 20 hazitoshi,ila zinasogeza kidogo,mbarikiwe wote and merry christmas
 
Asanteni wote kwa input yenu,nyumba bado finishing,kwa experience yangu nyumba million 20 hazitoshi,ila zinasogeza kidogo,mbarikiwe wote and merry christmas

Kwa ukubwa gani kwa maana y vyumba?
 
Inategemea nyumba ya namna gani. Kea nyumba za kisasa iliyokamilika chukua eneo la nyumba unayotaka kujenga (square meter) hala zidisha mara laki tano. Utapata makadirio mazuri ya gharama za ujenzi mpaka nyumba kukamilika.
 
Back
Top Bottom