Dahhh uraibu wa kubeti sitokuja kuusahau, Yani wakati wenzetu wanaovuta sigara wanasema tunaskia arosto we unawaona kama wanaigiza hivi
Nashkuru Mungu nilifanikiwa kuacha tangu mwaka 2017, haikuwa kazi rahisi ata kidogo, ila baada ya kufanya tathmini ya pesa nilizompa muhindi na ambazo yeye kanikopesha niliona sina future nzuri
Huu mchezo unawalemaza vijana wengi Sana kipindi ambacho wapo chuo, maana hela ni uhakika ata kama hana Mkopo anajua atapiga kizinga nyumbani na watamtumia
ila baada ya kuingia mtaani ndio arosto inakolea sasa, usipokuwa makini unaweza kuanza kupita na vihela ambavyo vinazagaa zagaa sebuleni alafu case wanapewa madogo
Kuacha kubeti ni maamuzi Tu mkuu ata haiitaji ushauri wa mtu, me niliacha baada ya kujaribu kuhesabu pesa nilizomchangia muhindi, nikakuta yeye amechukua kama 2M yangu ndani ya semester 1, alafu me kanikopesha kama 800k
Nikawaza nilipotoa hela zote hizo ni wapi mbona me sina uwezo wa kupata 2M ambayo haina kazi, nikagundua nilikuwa napata kutoka vyanzo vya mapato vya wengine maana vizinga vilikuwa vingi Sana wakati nasoma utazani mtoto wa kike
Ndipo nilipojua huu ni ugonjwa na natakiwa kuutafutia Tiba kabla haujakomaa, sema me niliacha siku nzuri maana kesho yake nikampiga muhindi 700k kupitia Mkeka nilioweka usiku kabla ya kupiga mahesabu kama prof Asadd CAG, kesho yake nikaamkia Posta kumenya PC mpyaaaaa